Sanduku la Swali
● Je! inafaa kuandikia Sosaiti au ofisi za tawi zayo ili kupata anwani za watu ambao ungependa kuandikiana barua nao kuhusu biashara na mambo mengine ya kibinafsi?
Anwani zote zilizomo katika faili za Sosaiti au katika faili za kundi ni za siri na haziwezi kutolewa kwa utumizi wa kibinafsi. Kwa hiyo, mtu yeyote asiandikie Sosaiti au ofisi za tawi zayo akiomba habari hiyo.
Lazima kundi likazie fikira kusudi lalo na kazi inayohusu kujiweka kwetu wakfu kwa Yehova kwa nafsi nzima na kufanya mapenzi yake. Sosaiti wala kundi halitajiingiza kutegemeza au kuendeleza utendaji wa kibiashara. Mambo kama hayo yanapasa kuonwa kuwa ya kibinafsi kabisa, utendaji wa kibiashara wa mtu mwenyewe. Wahubiri ambao wanataka kuwasiliana na akina ndugu katika majiji mengine au hata nchi za ng’ambo yawapasa wajitafutie wenyewe njia ya kufanya hivyo.