Habari za Kitheokrasi
◆ Katika Februari 11, 1991, shirika Association of Jehovah’s Witnesses of Mozambique lilitambuliwa rasmi katika nchi hiyo.
◆ Togo iliripoti kilele kipya cha wahubiri 5,582 katika Februari, ongezeko la asilimia 15. Vijapokuwa vizuizi, wahubiri walikuwa na wastani wa saa 15.7 na mapainia wasaidizi walikuwa na wastani wa saa 64.7 katika utumishi wa shambani.
◆ Bahamas ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,219 katika Februari. Maendeleo mazuri yanafanywa katika mradi wa ujenzi wa tawi jipya.
◆ Cyprus ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,314 katika Februari, pamoja na kilele kipya katika mafunzo ya Biblia.
◆ St. Lucia iliripoti kilele kipya cha wahubiri 465 katika Februari.
◆ Visiwa vya Solomon vilikuwa na kilele cha wahubiri 809 katika Februari.
◆ Tahiti ilikuwa na kilele cha 40 mfululizo cha wahubiri, kukiwako 1,246 walioripoti. Hesabu ya mafunzo ya Biblia ilifikia 1,578, kilele kingine.
◆ Trinidad walikuwa na kilele chao cha tatu cha wahubiri kwa mwaka wa utumishi, 5,950 wakiripoti katika Februari.
◆ Samoa Magharibi ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 234 katika Februari kikiwa ongezeko la asilimia 14.