Habari za Kitheokrasi
Ailandi: Mfululizo wa 59 wa kilele cha wahubiri ulifikiwa Februari kukiwa na 4,093 wakiripoti. Ongezeko la wakati ujao laonekana lawezekana kukiwa na kilele kipya cha mafunzo ya Biblia nyumbani 2,682 yakiongozwa.
Ajentina: Kilele kipya cha wahubiri cha wakati wote cha 98,601 kilifikiwa Februari. Wakati wa mwezi huohuo, wanafunzi wapya 507 walibatizwa.
Benin: Kilele kipya cha wahubiri 2,967 kiliripotiwa katika Februari. Ukilinganishwa na utendaji wa mwaka mmoja uliopita, wahubiri wameongezeka kwa asilimia 13.8, saa kwa asilimia 6.1, uangushaji wa magazeti kwa asilimia 40.6, na mafunzo ya Biblia kwa asilimia 25.1.
Ekwedori: Wahubiri 23,176 walioripoti utumishi wa shambani wakati wa Februari waliongoza mafunzo ya Biblia nyumbani 42,219. Hilo lilikuwa ongezeko la wahubiri 2,180 na mafunzo ya Biblia 3,183 zaidi ya Februari ya mwaka uliopita.
Peru: Wahubiri 43,366 katika Peru waliripoti ziara za kurudia 369,437 na mafunzo ya Biblia nyumbani 68,090 katika Februari. Jumba la Kusanyiko jipya katika Lima liliwekwa wakfu kukiwa 21,240 waliohudhuria.
Tahiti: Ongezeko la asilimia 13 lilifikiwa Februari kukiwa na wahubiri 1,604 walioripoti. Huo ulikuwa mfululizo wa 64 wa kilele cha wahubiri katika Tahiti.
Zaire: Kujapokuwa masumbufu ya kiuchumi na ya kisiasa katika nchi hii, kina ndugu waliripoti kilele kipya cha wahubiri 71,098 Februari. Hilo lilikuwa ongezeko la asilimia 9 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita. Wahubiri wa kutaniko wanafanya wastani wa saa 16.8 katika utumishi wa shambani. Zaire sasa ina mapainia wa kawaida zaidi ya 6,000.
Aruba, Guadeloupe, Martinique, St. Kitts, na Visiwa vya Virgin vya U.S., vyote vikiwa eneo la Karibea, ziliripoti vilele vipya vya wahubiri katika Februari.