Habari Za Kitheokrasi
Afrika Mashariki: Kufikia sasa Mikusanyiko ya Wilaya 14 ya “Wapendao Uhuru” imefanywa katika nchi 5 katika eneo letu kukiwa na kilele cha hudhurio lililojumlishwa la 32,751 na 944 waliobatizwa.
Haiti: Wahubiri 7,209 walioripoti katika Novemba waliongoza mafunzo ya Biblia 14,281. Wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa mafunzo ya Biblia 1.3 kila mmoja.
Martiniki: Kilele kipya cha wahubiri 3,169 kilifikiwa katika Novemba. Hotuba ya mwangalizi wa eneo la dunia ilihudhuriwa na 5,046.
St. Lucia: Kilele kipya cha wahubiri 481 kilifikiwa katika Novemba.
Tahiti: Kilele kipya cha wahubiri 1,366 kilifikiwa katika Novemba, likiwa ongezeko la asilimia 10.
Thailandi: Kilele kipya cha wahubiri 1,232 kiliripotiwa katika Novemba, asilimia 6 zaidi ya mwezi uo huo mwaka jana.
Zaire: Kulikuwa na fujo katika Oktoba huku ghasia na uporaji mali zikitukia katika miji mingi. Kujapokuwa matatizo ya kiuchumi akina ndugu wanajishughulisha na kuhubiri habari njema. Programu ya msaada wa dharura wa chakula ilianzishwa katika Kinshasa ili kusaidia ndugu zetu; hilo limethaminiwa nao sana.