Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai
Juma Linaloanza Julai 5
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yafaayo kutoka kwa Huduma ya Ufalme Yetu. Uwe na wahubiri wawili au watatu waliojitayarisha kutoa maelezo ya jinsi wanavyotumia vizuri matoleo ya zamani ya magazeti.
Dak 15: “Kutoa Broshua Ili Kutafuta-tafuta Wenye Kupendezwa.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Broshua zinazorejezewa katika fungu la tano ni: Je! Uamini Utatu? Je! Kweli Mungu Anatujali? na Serikali Itakayoleta Paradiso. Julisha kutaniko juu ya akiba ya broshua zilizoko, na uulize watoe maelezo juu ya ni broshua zipi zitakazofaa hasa eneo la kwenu na maeneo ya mbali. Tia moyo kina ndugu kwa idili washiriki kikamili kutoa broshua wakati wa Julai. Pia taja kwamba mara nyingi watu wanaochukua broshua hupenda kuchukua magazeti pia.
Dak 20: “Kutumia Broshua kwa Matokeo Katika Julai.” Zungumzia mambo makuu pamoja na kutaniko, na utoe wonyesho wa utoaji katika mafungu ya 3, 4, and 6. Tia moyo utayarishaji mzuri.
Wimbo 30 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 12
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na shukrani zozote za upaji wa hiari. Kumbusha kutaniko juu ya mipango ya utumishi wa shambani, na uzungumzie mambo mbalimbali ya kuongewa kutoka kwa magazeti.
Dak 20: “Kurudi Ili Kuchochea Kupendezwa Katika Biblia.” Baada ya utangulizi mfupi, toa wonyesho wa ziara ya kurudia kwa mtu aliyeonyesha kupendezwa lakini hakukubali fasihi. Pia, toa wonyesho wa jinsi kumrudia mtu aliyekuwa na shughuli nyingi mno asiweze kuongea lakini alikubali trakti Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu? Kwa kila kisa, onyesha jinsi mhubiri anavyoanzisha mazungumzo na kuchochea kupendezwa.
Dak 15: “Kujifunza Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi.” Maswali na majibu. Amsha idili kwa funzo la kitabu hiki litakaloanza juma la Agosti 2.
Wimbo 191 sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 19
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Pitia kifupi mipango ya kuhubiri maeneo ya mbali na maeneo yasiyogawiwa watu wakati wa Agosti. Watie moyo walio kwenye likizo washiriki katika utumishi wa painia msaidizi katika maeneo haya ya mbali.
Dak 15: “Je! Wewe Unaweza Kuufanya?” Zungumza na wasikilizaji. Hoji mapainia wa kawaida mmoja au wawili au mhubiri mmoja au wawili ambao hufanya upainia msaidizi mara kwa mara. Waache waeleze jinsi walivyofanya uamuzi wa kufanya mengi zaidi na jinsi wanavyopanga utendaji wao.
Dak 15: Hotuba ikitolewa na mzee juu ya usafi wa kibinafsi, ikitegemea Mnara wa Mlinzi wa Juni 1, 1989, kurasa 15-20. Hotuba hiyo inapaswa kushughulika na mambo ya kwenu yanayohusu Jumba la Ufalme, na mnapohudhuria kusanyiko la mzunguko na siku yakusanyiko la pekee na mikusanyiko ya wilaya. Ndugu anayeshughulikia sehemu hii anapaswa kuitoa kwa fadhili na kutumia uamuzi mzuri.
Wimbo 165 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 26
Song 170
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Mzee afikiria ripoti ya utumishi wa shambani wa Juni ya kutaniko, akipongeza na kutia moyo. Pia, zungumzia mambo ya kuongewa mawili au matatu kutoka kwa magazeti ya kutumiwa katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak 15: “Msalaba,” kitabu Kutoa Sababu, kurasa 214-218. Ifanywe kuwa ziara ya kurudia kwa mwenye nyumba ambaye alikubali broshua “Tazama!” Mwenye nyumba aelekezea ukurasa 17 wa broshua na kuuliza ni kwa nini inamwonyesha Yesu akiwa juu ya mti badala ya msalaba. Ndugu anatumia kitabu Kutoa Sababu kumsaidia mwenye nyumba awe na maoni ya Biblia.
Dak 20: “Kutumia Vema Mnara wa Mlinzi na Amkeni!” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Saidia wote kuthamini fursa nyingi ambazo huenda tukawa nazo kila siku za kuangusha magazeti, matoleo ya karibuni pamoja na ya zamani.
Wimbo 192 na sala ya kumalizia.