Kutumia Vema Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
1 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni magazeti yenye thamani zaidi na yenye manufaa zaidi ambayo watu wanaweza kusoma leo. Kwa nini? Kwa sababu yana kweli za kiroho ambazo zaweza kuwa na matokeo mazuri ya milele kwa maisha ya watu. Hata hivyo, wengi hawatambui kikamili uhitaji wao wa kiroho, au hawajui ni wapi wanapoweza kuutoshelezea. Ni pendeleo letu kumwiga mtume Paulo kwa kusaidia watu wafungue macho yao kiroho.—Mt. 5:3; Mdo. 26:18.
2 Uwe Chanya na Utayarishe Vizuri: Inaelekea kuna watu wenye mfano wa kondoo katika eneo lenu ambao wataitikia kweli. Wengine huenda wakahitaji tu kitia-moyo chenye fadhili ili kusoma magazeti haya. Kwa hiyo, uwe chanya, na mwenye kusihi unapotoa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Uwe na magazeti ya kutosha na utumie kwa manufaa kila fursa ya kuyagawa, hata unapotoa vichapo vingine.
3 Ni nini linaloweza kutufanya tuwe na matokeo zaidi tunapogawa magazeti? Kwanza, ni lazima tuyathamini sisi wenyewe. Tunapaswa kujua makala zilizomo katika magazeti tunayotoa, na hilo litazidisha uhakika wetu na tamaa yetu ya kuyatoa. Kumbuka wazo hilo unapoyasoma kwa mara ya kwanza. Uwe macho kuchagua mambo ya kuonyesha katika huduma. Jiulize mwenyewe: ‘Makala hii ingempendeza nani hasa? Je! mke wa nyumbani, kijana, au labda mfanya biashara angeithamini? Je! jambo hili lingemvutia mwanafunzi, mtu aliyeoa au kuolewa, mtu anayehangaika juu ya mazingira?’ Ili tuwe wenye mafanikio kikweli, tunapaswa kuweza kupendekeza magazeti kwa msingi wa ujuzi na furaha yetu binafsi ya makala zayo za wakati unaofaa.
4 Tumia Vema Matoleo ya Zamani: Kumbuka, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hayapotezi thamani yayo, hata kama yote hayajaangushwa kwa mwezi mmoja au miwili ya tarehe yao ya kutolewa. Habari iliyo ndani yayo haipungui umaana wakati unapopita, na hatupaswi kusita kutoa nakala za zamani ikiwa ziko katika hali nzuri. Kuruhusu magazeti ya zamani yarundamane na kutoyatumia kamwe kwaonyesha ukosefu wa uthamini kwa zana hizi zenye thamani. Kila gazeti lina kweli ambazo zina nguvu za kuamsha na kutosheleza hamu ya kiroho. Badala ya kuweka kando matoleo ya zamani na kuyasahau, je, haingekuwa afadhali kufanya jitihada ya pekee kuyaacha mikononi mwa watu wenye kupendezwa?
5 Gazeti Amkeni! limesaidia wengi ambao hapo kwanza hawakuwa watu wenye mwelekeo wa kiroho waje kutambua uhitaji wao wa kiroho. Mnara wa Mlinzi ni zana kuu katika programu ya ulishaji kiroho wa watu wa Yehova. Magazeti haya yanapatana vizuri sana, na yanatimiza sehemu ya maana sana katika kuhubiriwa kwa habari njema.
6 Tunapotumia kwa manufaa kila fursa ya kuangusha magazeti, tunaweza kuwa na uhakika kamili kwa matokeo yayo mazuri ya kutimiza mahitaji ya kiroho ya wale wenye mfano wa kondoo. Tunataka kudumisha mwelekeo chanya, kujitayarisha vema, na kuwa wa kawaida katika huduma. Tukiwa wahubiri wa habari njema, sisi sote na tutumie vema magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa ukawaida.