Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?
1 Wengi wanapata mafanikio mazuri katika kuanzisha mafunzo ya Biblia kwa kutumia mfikio wa moja kwa moja katika kutolea watu fursa ya kujifunza Biblia. Mtu mmoja aliyekuwa amekataa fasihi mara kadhaa aliitikia kwa utayari alipotolewa funzo la Biblia. Yeye alijibu: “Mimi wakati wote nimetaka kujifunza Biblia.” Funzo la Biblia lilianzishwa, na familia nzima ikafanya maendeleo ya haraka.
2 Wote wanapaswa wafahamu umaana wa kuanzisha mafunzo. Ni lazima watu wafunzwe ili waweze kufanya maendeleo na kuwa wanafunzi wa Kristo. (Mt. 28:19, 20) Ili wafunzwe, wanahitaji kuwa na funzo la Biblia linaloongozwa pamoja nao. Mara nyingi mafunzo yanaweza kuanzishwa kwa kufanya tu utoaji wa kumwonyesha jinsi mwenye nyumba anavyoweza kujifunza zaidi kuhusu Biblia na ahadi za Mungu. Ndugu mmoja anayetumikia katika Betheli ya Brooklyn aliongoza mafunzo matano mwezi mmoja, akiwa ameanzisha yote hayo kwa trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Bila shaka, hangeweza kuongoza mafunzo hayo yote ya Biblia akiwa na kazi yake ya Betheli, kwa hiyo alianza kuwapa watu wengine mafunzo.
3 Ikiwa tunaliona kuwa jambo rahisi kuanzisha mafunzo, tunaweza kwenda pamoja na wahubiri wengine na kuwasaidia wapate mafunzo pia. Au tunaweza kuwapa wengine kundini baadhi ya mafunzo tunayoanzisha. Ikiwa ungependa kuongoza funzo la Biblia, kwa nini usijaribu kufanya utoaji wa funzo la Biblia kwa wale unaokutana nao katika huduma ya nyumba kwa nyumba? Katika kisa kimoja mhubiri alifanya ziara ya kurudia kwa msichana tineja ambaye hakuonyesha kupendezwa sana. Hata hivyo, mhubiri huyo alimtolea funzo la Biblia, naye akakubali. Sasa yeye amebatizwa, na dada yake na mume wa dada yake wanahudhuria mikutano pia.—Gal. 6:6.
4 Si kila mtu tunayeanzisha funzo naye ataendelea kujifunza. Si wote wanaojifunza watakubali kweli. Lakini wengine watakubali. Kadiri tunavyoanza mafunzo mengi zaidi, ndivyo inavyoelekea zaidi kwamba tutaweza kuwasaidia wengine wawe wenye kumsifu Yehova.