Matangazo
◼ Fasihi itakayotumiwa wakati wa Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi. Juni: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? au Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. TAARIFA: Makutaniko yatakayohitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) la kila mwezi litakalofuata.
◼ Kila mtu anayeshirikiana na kutaniko apaswa kupeleka maandikisho yote mapya na yenye kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu yeyote aliyewekwa naye apaswa akague hesabu ya kutaniko mnamo Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa kushiriki katika kampeni ya mwaka huu ya maeneo ya mbali kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda wanaweza kutoa maombi yao sasa kupitia baraza la wazee (au halmashauri ya utumishi) la kutaniko lao. Katika mapendekezo yazo, halmashauri za utumishi zaombwa kutoa sababu za kupendekeza painia na kueleza kama yeye ni mseja au aliyeoa au kuolewa, mwanamume au mwanamke (ana watoto wangapi ikiwa anao) na ikiwa mwenye kuomba yuko huru kuhamia maeneo yasiyogawiwa mtu kwa kipindi cha miezi mitatu. Halmashauri za utumishi zitaelewesha wazi mambo hayo na kupeleka barua za maombi pamoja na mapendekezo yazo kwa Sosaiti kufikia Aprili 15, 1994.