Matangazo
◼ Fasihi itakayotumiwa wakati wa Aprili na Mei: Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi. Juni: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? au Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Julai: Muunganisho wa vijitabu vitatu vya kurasa 32. TAARIFA: Makutaniko yatakayohitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) la kila mwezi litakalofuata.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa kushiriki katika kampeni ya mwaka huu ya maeneo ya mbali kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda wanaweza kutoa maombi yao sasa kupitia baraza la wazee (au halmashauri ya utumishi) la kutaniko lao. Katika mapendekezo yazo, halmashauri za utumishi zaombwa kutoa sababu za kupendekeza painia na kueleza kama yeye ni mseja au aliyeoa au kuolewa, mwanamume au mwanamke (ana watoto wangapi ikiwa anao) na ikiwa mwenye kuomba yuko huru kuhamia maeneo yasiyogawiwa mtu kwa kipindi cha miezi mitatu. Halmashauri za utumishi zitaelewesha wazi mambo hayo na kupeleka barua za maombi pamoja na mapendekezo yazo kwa Sosaiti kufikia Aprili 15, 1994.
◼ Hati za kisheria katika Kiingereza zinapatikana ili kusaidia wahubiri wanaohusika katika kesi zinazohusu haki za kumtunza mtoto na za kutembelea katika hali ambazo dini yetu inashambuliwa. Hati hizo zapasa kuombwa na baraza la wazee pekee katika hali za jinsi hiyo ikiwa ni wazi kwamba imani za kidini za mhubiri zinashambuliwa. Habari yenye kusaidia yaweza kupatikana kwa wale wanaokabili masuala ya kilimwengu juu ya haki za kumtunza mtoto au haki za kutembelea katika Amkeni! la Oktoba 22, 1988, kurasa 2-14, (Kiingereza), na chati inayopatikana katika Amkeni! la Oktoba 8, 1991, ukurasa 9.