Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/94 kur. 2-8
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 1
  • Juma Linaloanza Agosti 8
  • Juma Linaloanza Agosti 15
  • Juma Linaloanza Agosti 22
  • Juma Linaloanza Agosti 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 8/94 kur. 2-8

Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti

Juma Linaloanza Agosti 1

Wimbo 159

Dak 15: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Toa wonyesho wa mambo ya kuzungumzia kutoka magazeti ya karibuni yanayoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.

Dak 15: “Dumisha Mwelekeo Ufaao.” Maswali na majibu. Hoji kifupi painia au mhubiri wa muda mrefu ambaye ataeleza jinsi imewezekana kuwa na mwelekeo ufaao kujapokuwa kutojali na upinzani katika eneo.

Dak 15: “Broshua—Vifaa Vyenye Thamani kwa Huduma.” Zungumza na wasikilizaji. Panga kuwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri ya utoaji uliodokezwa. Onyesha baadhi ya broshua ambazo zitatolewa wakati wa Agosti. Kumbusha wasikilizaji wachukue nakala za kutumia katika utumishi wa shambani juma hili.

Wimbo 142 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 8

Wimbo 216

Dak 10: Matangazo ya kwenu.

Dak 15: “Wajue Ndugu Zako Vizuri.” Maswali na majibu. Karibisha wasikilizaji watoe maono mafupi ya kuonyesha jinsi waliweza kujuana na wengine kwa kutumia madokezo katika fungu la 6.

Dak 20: Kutoa Ushahidi wa Vivi-Hivi Zaidi. Kikundi cha wahubiri watatu au wanne wazungumzia jinsi ya kupanua ushiriki wao katika utendaji huu. Wakitumia Mnara wa Mlinzi, la Oktoba 15, 1987, kurasa 22-7, wapitia yale ambayo wengine wamefanya, nao wazungumza juu ya jinsi ya kupanga kufanya mengi zaidi ya kazi ya aina hii. Mwenyekiti awatia moyo wasikilizaji kufikiria jinsi wanavyoweza kushiriki utumishi huu.

Wimbo 182 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 15

Wimbo 166

Dak 5: Matangazo ya kwenu, kutia ndani ripoti ya hesabu na shukrani za upaji wa hiari.

Dak 15: “Kusitawisha Kupendezwa Katika Ziara za Kurudia.” Zungumza na wasikilizaji. Tia ndani maonyesho mawili ya dakika 3 ya kuonyesha jinsi utoaji huo unavyoweza kutumiwa kufanya ziara za kurudia. Tia moyo jitihada za kuanzisha mafunzo ya Biblia.

Dak 25: “Fulizeni Kutembea kwa Maendeleo Katika Kawaida Yenye Utaratibu.” Maswali na majibu.

Wimbo 96 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 22

Wimbo 218

Dak 10: Matangazo ya kwenu.

Dak 20: Naweza Kumkaribiaje Mungu? Wonyesho wa funzo la familia. Wazazi wazungumzia habari iliyo kwenye sura ya 39 ya kitabu Vijana Huuliza pamoja na watoto matineja. Shughulikia kichwa kidogo “Kujulisha Rasmi Peupe Urafiki Wako Pamoja na Mungu,” kurasa 315-18. Watoto walalamika juu ya kuona haya wanapoenda mlango kwa mlango na waeleza mikutano kuwa yenye kurudiwarudiwa na ni ya mara nyingi. Wazazi wasababu pamoja nao kwa njia ya fadhili, wakionyesha kanuni za Kimaandiko zinazoonyesha kwamba utendaji huu ni muhimu ikiwa watadumisha uhusiano mzuri pamoja na Yehova.

Dak 15: Mahitaji ya kwenu. Au toa hotuba juu ya makala “Kujishughulisha Sana na Habari Njema” katika Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 1991, kurasa 28-30.

Wimbo 184 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 29

Wimbo 199

Dak 13: Matangazo ya kwenu. Hoji mhubiri mmoja au wawili walioweza kufanya upainia msaidizi au walioweza kupanua utendaji wao wakati wa miezi ya karibuni. Eleza baadhi ya shangwe zilizoonwa.

Dak 15: “Je, Waweza Kujiunga Tena na Kundi Hilo?” Zungumza na wasikilizaji. Tia ndani maono yoyote ya kwenu kuonyesha jinsi mtu fulani ameweza kuingia tena katika utumishi wa painia au nyumba nzima imesaidia mshiriki mmoja wa familia kutumia vizuri fursa ya pendeleo hili.

Dak 17: Toa Kitabu Kuishi Milele Wakati wa Septemba. Tia moyo jitihada zenye idili za kuangusha kitabu hiki na kuanzisha mafunzo ya Biblia wakati wa Septemba. Kilitolewa katika 1982 nacho tangu wakati huo kimetumiwa kuwa kifaa cha msingi cha kuongoza mafunzo ya Biblia. Nakala zilizotolewa katika mkusanyiko wa wilaya zilikuwa na ujumbe huu: “Kitabu hiki kipya cha kujifunzia kina tu yale yahitajiwayo kuwasaidia wengine wengi washiriki tumaini lilelile tulilonalo. . . . Kina kweli zote za maana za Biblia wanazohitaji wapya kuelewa ili waweke maisha zao wakfu kwa Yehova na wamtumikie kwa kukubalika.” Matokeo yaonyeshwa kwa ongezeko la wahubiri kutoka 2,652,323 katika 1983 hadi 4,709,889 katika 1993. Karibisha watu mmoja-mmoja waeleze jinsi walivyojifunza kweli kwa kusoma kitabu hiki au jinsi walivyosaidia wengine kwa kuwafunza nacho. Wakati ukiruhusu, eleza sehemu nyingine za kitabu zinazoweza kuonyeshwa unapotoa toleo.

Wimbo 161 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki