Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/94 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 8/94 uku. 7

Matangazo

◼ Fasihi itakayotumiwa wakati wa Agosti: Yoyote ya broshua zenye kurasa 32 zifuatazo zaweza kutumiwa: Je! Kweli Mungu Anatujali?, Furahia Milele Maisha Duniani!, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Serikali Itakayoleta Paradiso, na Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? Septemba: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Oktoba: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Novemba: New World Translation of the Holy Scriptures pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) lao la kila mwezi litakalofuata. Tafadhali agizeni magazeti ya ziada kwa ajili ya ugawanyaji wa Oktoba.

◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza 1995 Calendar of Jehovah’s Witnesses pamoja na ombi lao la fasihi la Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kiingereza na Kifaransa.

◼ Kuanzia Agosti 29 hadi Septemba 1, Sosaiti itakuwa ikihesabu fasihi zote zilizomo Betheli. Kwa sababu ya kuhesabu huku, hakuna maagizo yoyote ya fasihi ya kutaniko yatakayofanyiwa upakizi au yatakayochukuliwa siku hizo.

◼ Ugavi wa kutosha wa fomu za kutumia wakati wa mwaka wa utumishi wa 1995 zinapelekwa kwa kila kutaniko. Fomu hizi hazipasi kutumiwa vibaya. Zapasa kutumiwa tu kwa kusudi lazo.

◼ Kila mtu anayeshirikiana na kutaniko apaswa kupeleka maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.

◼ Sosaiti haijazi maombi ya fasihi ambayo yamefanywa na wahubiri mmoja-mmoja. Wale wanaotaka kifaa wanaweza kumuuliza mtumishi wa fasihi, ambaye atatia ndani ya agizo la fasihi la kila mwezi la kutaniko. Mwangalizi-msimamizi anapaswa kupanga kuwe na tangazo kila mwezi kabla ya agizo la fasihi la kila mwezi la kutaniko halijapelekwa kwa Sosaiti ili kwamba wale wote wanaopendezwa kupata vifaa vya fasihi vya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi.

◼ Kila kutaniko litapokea fomu tatu za Orodha ya Vitabu (S-18-SW). Mwandishi wa kutaniko anapaswa kukutana na mtumishi wa fasihi mapema katika Agosti na kuweka tarehe ya kuhesabu fasihi zote zilizo akibani za kutaniko mwishoni mwa mwezi. Hesabu kamili yapaswa kufanywa ya fasihi zote zilizo akibani, na jumla ya hesabu zapasa kuingizwa kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu. Jumla ya hesabu ya magazeti yaliyopo yaweza kupatikana kutoka kwa mtumishi wa magazeti. Tafadhali pelekeni ile nakala ya kwanza kwa Sosaiti si baada ya Septemba 6. Wekeni nakala ya kaboni kwa ajili ya faili yenu. Nakala ya tatu yaweza kuwa ya kufanyia kazi. Kazi hiyo ya kuchukua hesabu ya orodha yapasa kusimamiwa na mwandishi, na fomu iliyokamilishwa ichunguzwe na mwangalizi-msimamizi. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi watatia sahihi fomu hiyo.

◼ Wahubiri wanaopanga kuanza utumishi wa upainia wa kawaida Septemba 1, 1994, wapaswa kujaza maombi bila kuchelewa.

◼ Mwandishi wa kutaniko atakusanya ripoti za utumishi kwa ajili ya kuingiza kwenye fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kundi (S-10-SW). Pia ataagiza kwa uangalifu mzee yeyote au mtumishi wa huduma ambaye anaweza kusaidia kukusanya ripoti. Hilo litahakikisha hesabu sahihi ya habari inayohitajika kutoka kwa kadi za Maandishi ya Mhubiri wa Kundi (S-21-SW). Fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kundi (S-10-SW) yapasa kujazwa kwa usahihi na unadhifu na ichunguzwe vizuri na halmashauri ya utumishi.

◼ Vichapo Vinavyopatikana:

Gujarati: Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? (Trakti Na. 19); Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?; Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kifaransa: Mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi ya 1975, 1976; New World Translation of the Holy Scriptures (Deluxe; DLbi12); Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!; Why Should We Worship God in Love and Truth?; Yearbook of Jehovah’s Witnesses—1994. Kihindi: Furahia Milele Maisha Duniani!; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?; Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? (kwa Wahindu); “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” (Broshua); Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani (kile kidogo); Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kiingereza: Disketi, ya GetVerse ya New World Translation of the Holy Scriptures ya inchi 51/4; New World Translation of the Holy Scriptures (bi12); Mabuku yaliyojalidiwa ya Amkeni! ya 1993; Mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi ya 1986, 1987, 1988, 1993; Seti ya kadi 10 za picha (cd-10); Watch Tower Publications Index 1991-1992. Kinyakyusa: Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Kirutoro: Furahia Milele Maisha Duniani! Kiteso: Furahia Milele Maisha Duniani! Punjabi: Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote; Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia (Trakti Na. 13); Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini? (Trakti Na. 14); Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani (Trakti Na. 15); Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa? (Trakti Na. 16).

◼ Kaseti Zinazopatikana:

Kiingereza: Kumsikiliza Mwalimu Mkuu (seti ya kaseti nne na kitabu kwenye kiwekeo).

◼ Vidiokaseti Zinazopatikana:

Lugha ya Ishara ya Kiamerika (ASL): “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Kiingereza: Mankind’s Oldest Modern Book.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki