Mikutano Ya Utumishi Kwa Oktoba
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itaorodhesha ratiba ya Mkutano wa Utumishi kila juma la pindi ya mkusanyiko. Makutaniko yaweza kufanya marekebisho yanayohitajika ili kuyawezesha kuhudhuria “Hofu ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya na dakika 30 za pitio la mambo makuu ya programu hiyo juma linalofuata. Pitio la siku kwa siku la programu ya mkusanyiko wa wilaya lapasa ligawiwe mapema ndugu wawili au watatu wenye sifa za kustahili ambao wataweza kukazia fikira mambo yenye kutokeza. Pitio hili lenye kutayarishwa vizuri litasaidia kutaniko kukumbuka mambo makuu ya kutumia kibinafsi na kutumia shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yapaswa kuwa mafupi na yenye kulenga jambo kuu.
Juma Linaloanza Oktoba 3
Dak 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Shughulikia barua ya taw.
Dak 15: “Sasa Ndio Wakati.” Maswali na majibu. Tia maelezo juu ya kichwa kidogo “Fuatia Miradi ya Kiroho” kwenye ukurasa 5 wa Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1993.
Dak 18: “Hangaikia Kutoa Magazeti Wakati wa Oktoba.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga uwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri yakionyesha jinsi ya kutumia magazeti kuanzisha mazungumzo. Kazia umaana wa kutoa magazeti katika kila mlango ukiwa na mradi wa kupata maandikisho. Toleo likikataliwa toa magazeti ya karibuni ukiwa na mradi wa kuanzisha au kusitawisha njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida.
Wimbo 212 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 10
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na shukrani zozote za upaji wa hiari.
Dak 15: “Wazazi—Iweni Waungaji-Mkono!” Hotuba ikitolewa na mzee ikitegemea makala tatu za kwanza za Amkeni! la Agosti 8, 1994. Fanya habari hiyo ifae matumizi ya kwenu. Hoji kifupi mzazi ambaye amepata kuongea na walimu au wakuu wa shule. Kazia jinsi wazazi wanavyoweza kuwaunga watoto wao.
Dak 20: “‘Hofu ya Kimungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1994.” Nyongeza. Maswali na majibu ya mafungu 1-11, ikishughulikiwa na mzee. Toa uangalifu kwa “Vikumbusha vya Mkusanyiko wa Wilaya.”
Wimbo 108 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 17
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak 15: “‘Hofu ya Kimungu’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1994.” Nyongeza. Hotuba ikitegemea mafungu 12-23, ikishughulikiwa na mwandishi wa kutaniko. Tia ndani vikumbusha vingine vya mkusanyiko vilivyo vya lazima, kama vile, tikiti za chakula, mahali pa kulala na kadhalika.
Dak 20: “Wasaidie kwa Upendo Wale Wanaoonyesha Kupendezwa.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Panga kuwe na maonyesho mawili yakitumia utoaji uliopendekezwa.
Wimbo 156 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 24
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: Je, Una Agizo la Hesabu Fulani? Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni magazeti yenye misaada mikubwa ajabu katika kueneza ujumbe wa Ufalme. Twapaswa kuyatoa katika kila fursa. Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1984 ilipendekeza kwamba kila mhubiri awe na “agizo la magazeti” lililo kamili . . . kwa agizo la hesabu fulani la nakala za kila toleo.” La sivyo twaweza kujipata tukiwa hatuna matoleo ya karibuni ya kutoa na itulazimu tutegemee trakti au broshua. Itakuwa vizuri kwa kila mshiriki wa familia awe na agizo la hesabu fulani. Toa maagizo kwenye dawati la magazeti. Hakikisha unachukua magazeti yanapofika. Taja manufaa zitokanazo na kuwa na agizo la hesabu fulani.
Dak 20: “Utafuteni Ufalme wa Mungu Kwanza—Kwa Kumtolea Dhabihu za Sifa Sikuzote.” Maswali na majibu. Taja miradi fulani yenye manufaa tunayoweza kufuatia kibinafsi. Zungumzia njia tunazoweza kusaidia wengine zaidi.
Wimbo 171 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 31
Dak 12: Matangazo ya kwenu. Kukiwa na sikukuu za kilimwengu zinazokuja katika Desemba, tia moyo wote wafikirie juu ya kujiandikisha wawe mapainia-wasaidizi. Toa madokezo fulani ya jinsi twaweza kupata wakati wa kutosha kuufanya. Pia, toa wonyesho mmoja mfupi wa kutumia ili kutoa magazeti mwisho-juma huu.
Dak 15: Tusichoke Katika Kutenda Mema. Hotuba ikitolewa na mzee. Uchovu wa kiroho waweza kupunguza shangwe na bidii yetu katika utumishi wa Yehova. Pitia njia fulani za kufanya upya nguvu yetu ya kiroho ukitumia madokezo yaliyotolewa kwenye Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1986, ukurasa 19 (sanduku). Kazia tegemezo la moyo wote kwa utendaji wa kutaniko.
Dak 18: Toa New World Translation Katika Novemba. Kwa kuwa watu walio wengi tayari wana Biblia, twahitaji kuonyesha ni kwa nini New World Translation ni bora. Rejezea kwenye kitabu “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (kurasa 327-8, maf. 1-6). Eleza ni kwa nini jina la Yehova latumiwa, na utoe vielelezo fulani vya kuonyesha manufaa za kutumia lugha ya kisasa. Onyesha sehemu zenye kusaidia nyuma ya Biblia, kama vile ‘Maneno ya Biblia Yaliyoorodheshwa,’ ambayo yaweza kutumiwa kupata maandiko yanayofahamika kwa urahisi. ‘Ratiba ya Vitabu vya Biblia’ yaonyesha ni nani aliyeandika kila kitabu na wapi na ni lini kiliandikwa pamoja na wakati kilikamilishwa. Rejezea kitabu Kutoa Sababu (ukurasa 41, kichwa kidogo “Unabii wa Biblia unaeleza maana ya hali za ulimwengu”), na uzungumzie jinsi unavyoweza kuanzisha mazungumzo ya Kimaandiko yakitegemea Yohana 17:3 na Zaburi 37:10, 11, 29. Panga mhubiri mwenye sifa za kustahili atoe wonyesho wa jinsi New World Translation na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? vyaweza kutolewa katika eneo la kwenu.
Wimbo 136 na sala ya kumalizia.