Matangazo
◼ Fasihi itakayotumiwa wakati wa Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1982 ambacho kutaniko huenda likawa nacho akibani. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani akibani yatatoa kitabu Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? Februari: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani kitatolewa. Maangusho ya kitabu hiki yapaswa kufuatiwa na ziara za kurudia, na jitihada zapaswa kufanywa za kuanzisha mafunzo ya Biblia. Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa kufanya hivyo kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) lao la kila mwezi litakalofuata.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu yeyote aliyechaguliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko katika Desemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hili lifanywapo.
◼ Ukumbusho wa 1996 utakuwa Jumanne, Aprili 2, baada ya jua kushuka. Taarifa hii ya mapema ya tarehe ya mwadhimisho wa Ukumbusho wa 1996 inatolewa ili akina ndugu waweze kuhifadhi au kufanya maagano ya lazima kwa ajili ya majumba yapatikanayo wakati ambapo kuna makutaniko mengi yanayotumia Jumba la Ufalme na lazima wapate majengo mengine.
◼ Chapa za Mnara wa Mlinzi za Bengali, Gujarati, Kihindi, na Kinepali zitabadilika kutoka kuwa mara moja kwa mwezi hadi mara mbili kwa mwezi kuanzia Januari 1, 1995.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya 1994 kwenye agizo lao la fasihi la Desemba. Mabuku yaliyojalidiwa yatapatikana katika Kiingereza na Kifaransa. Hadi mabuku yatakapopatikana na upakizi umefanywa, haya yatakuwa “Yanayokuja” katika orodha ya upakizi ya kutaniko. Mabuku yaliyojalidiwa ni bidhaa za kuagizwa kipekee.—Ona Orodha ya Bei.
◼ Barua ya Sosaiti ya Agosti 1, 1993, iliyoandikiwa mabaraza yote ya wazee, ilielekeza kwamba nyongeza mbili zinazoshughulikia dharura za kitiba, zilizotokea katika matoleo ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1990 na Septemba 1992, zapasa kufanywa zipatikane kwa kila mtu mpya aliyebatizwa. Wazee watafuatia mwelekezo huu.