Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/95 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 1/95 uku. 3

Matangazo

◼ Fasihi itakayotolewa wakati wa Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1982 ambacho huenda kutaniko likawa nacho akibani. Chaweza kutolewa kwa nusu-bei. Kupunguzwa kwa bei za painia pia ni nusu ya bei ya kawaida. Makutaniko yasiyo na vitabu vya zamani akibani yanapaswa kutoa Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? Februari: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani kitatolewa. Maangusho ya kitabu hiki yapaswa kufuatiwa na ziara za kurudia, na jitihada zapaswa kufanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Machi: Ufunuo Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayakubaliwi, toa magazeti hayo mawili au broshua yoyote yaweza kutumiwa (isipokuwa broshua Shule). TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa kufanya hivyo kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) lao la kila mwezi litakalofuata.

◼ Makutaniko yapaswa kufanya mipango ifaayo ili kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu Ijumaa, Aprili 14, baada ya jua kushuka. Ijapokuwa inapendeza kwa kila kutaniko kuwa na mwadhimisho wake wenyewe wa Ukumbusho, huenda isiwezekane sikuzote. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au mawili yaweza kujipatia utumizi wa jengo jingine jioni hiyo. Ukumbusho haupaswi kuanza kuchelewa mno hivi kwamba watu wapya wanaopendezwa waone ikiwa vigumu kuhudhuria. Zaidi ya hayo, ratiba haipasi kusongamana sana hivi kwamba hakuna wakati wa kusalimia wageni kabla na baada ya mwadhimisho, kufanya mipango ya usaidizi wa kiroho wenye kuendelea kwa wengine, au kufurahia badilishano la ujumla la kitia-moyo. Baada ya kufikiria mambo yote, wazee wapaswa kuamua ni mipango gani itakayosaidia vizuri zaidi wale wanaohudhuria Ukumbusho ili wanufaike kikamili kutokana na pindi hiyo.

◼ Jumapili, Aprili 23, 1995, hotuba ya pekee itatolewa katika makutaniko yote. Kichwa kitakuwa “Mwisho wa Dini Bandia U Karibu.” Hakikisha umealika wote wanaohudhuria Ukumbusho mwaka huu. Jitihada ya pekee itafanywa ili kusaidia mamilioni ya wanafunzi ambao mafunzo ya Biblia nyumbani yaongozwa pamoja nao. Habari itakayotolewa kufuatia mkutano siku hiyo itasukuma wao pamoja na ndugu zetu kwa ujumla watazamie kwa hamu kushiriki katika kugawanya trakti ya pekee. Wakati uleule, itaonyesha wazi matatizo wanayokabili watu mmoja-mmoja na uhitaji wa kutenda kwa kukata shauri kulingana na Neno la Mungu.

◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 5, hotuba mpya ya watu wote ya waangalizi wa mzunguko itakuwa “Ufundishaji wa Kimungu Hushinda Ulimwenguni Pote.” Huu utakuwa wonyesho wa slaidi ukikazia “Ufundishaji wa Kimungu” Mikusanyiko ya pekee ya kimataifa iliyokuwa wakati wa miaka ya utumishi ya 1993 na 1994. Katika maeneo ambamo slaidi hazitapatikana hadi tarehe ya baadaye, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba “Tumaini Katika Mungu wa Faraja Yote” na waendelee nayo hadi wakati slaidi zitakapopokewa. Makutaniko yote yatakapopata hotuba ya slaidi, waangalizi wa mzunguko wataendelea kutoa hotuba “Tumaini Katika Mungu wa Faraja Yote” hadi hotuba mpya itakayofuata ya mwangalizi wa mzunguko itakaporatibiwa kwa ajili ya mwanzoni mwa 1996.

◼ Kwenye Mkutano wa Utumishi juma la Januari 9, wahubiri wote waliobatizwa watakaokuwapo watakuwa na nakala ya kibinafsi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na Kadi ya Utambulishi kwa watoto wao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki