Kikumbusha kwa Mwandishi na Mwangalizi wa Utumishi
Kila mwaka tangazo katika toleo la Februari la Huduma ya Ufalme Yetu huelekeza mwandishi na mwangalizi wa utumishi “kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida.” Ni nini kusudi la pitio hilo? Ni kuamua ni nani ambao huenda wakahitaji msaada ili kutimiza takwa la saa kabla ya mwaka wa utumishi kuisha.
Mapainia wa kawaida wanatakiwa kutolea huduma saa 1,000 kila mwaka. Kufikia mwisho wa Februari, mapainia wengine hupata kwamba wamerudi nyuma katika saa, na hilo laweza kuongoza kwenye kuvunjika moyo. Mara nyingi wazee waweza kuwasaidia mapainia, wakiwapa kitia-moyo na madokezo yenye kutumika. Hilo laweza kuamua kama mapainia watatimiza kwa mafanikio matakwa yao ya saa ya mwaka huo au wataacha upainia.
Kwa hakika mapainia watathamini ufikirio wa kweli wa wazee kuhusu jambo hili. Kutaniko litanufaika pia kwa kuwa na mapainia walio na furaha katika huduma yao, wakishikamana na mgawo wao kwa uaminifu.