Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/95 uku. 1
  • Kudumisha Muungamano Wetu wa Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kudumisha Muungamano Wetu wa Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Kinacholeta Umoja wa Kweli Miongoni mwa Wakristo?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Umoja wa Kikristo Unamletea Mungu Utukufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Dumisheni Muungano Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Umoja Unatambulisha Ibada ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 4/95 uku. 1

Kudumisha Muungamano Wetu wa Ufalme

1 Ufalme wa Mungu ni serikali halisi, yenye nguvu na mamlaka. Huo ulikuwa kichwa cha mahubiri ya Yesu. (Mt. 4:17) Kufundisha wengine na kutolea ushahidi Ufalme kulikuwa sehemu kubwa ya huduma ya Yesu. Alitufundisha kusali kwa ajili ya Ufalme na kuendelea kuutafuta kwanza. (Mt. 6:9, 10, 33) Kubaki tukiwa karibu na Yehova na tengenezo lake, kutimiza agizo letu la kuhubiri, na kujitenga na ulimwengu hutuwezesha kudumisha muungamano wetu wa Ufalme. Kwa vitendo vyetu na maneno yetu, twaonyesha kwamba tupo upande wa ule Ufalme.—Yn. 18:37.

2 Tangu 1914, Ufalme umekuwa halisi kwa mamilioni ya raia. Muungamano unaoonyeshwa na raia hawa wa Ufalme watofautiana kabisa na ulimwengu uliogawanyika. Twapaswa kufanya Ufalme uwe halisi maishani mwetu ikiwa utakuwa kichocheo chenye kuunganisha. Ni nini kiufanyacho kuwa halisi kwetu?

3 Kama vile serikali nyinginezo, Ufalme huo una idadi ya sheria. Lakini, watofautiana kwa kuwa sheria zake zapatikana katika Biblia. Usomaji wa kawaida wa Neno la Mungu hutupa vikumbusha vinavyohitajika vya yanayotakwa kwetu tukiwa raia za Ufalme. Funzo la kibinafsi la vichapo vyetu na mwelekezo kutoka kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” hutusaidia kutumia sheria za Mungu katika maisha zetu za kila siku. (Mt. 24:45) Tunapofanya matumizi hayo ya kibinafsi, Ufalme huendelea kuwa halisi kwetu, ukituvuta karibu pamoja katika udugu wa ulimwenguni pote, ukitufanya kuwa familia yenye muungamano ya waabudu chini ya utawala wa Yesu.

4 Muungamano Kupitia Kuhubiri Ufalme: Agizo letu ni kuhubiri habari njema za Ufalme “hata mwisho wa nchi.” (Mdo. 1:8) Kuhubiri “kwa moyo mmoja” hutuunganisha tunapojitahidi “kumtukuza” Yehova. (Rum. 15:5, 6) Kushiriki kwa bidii na wafanyakazi wenzetu ulimwenguni pote huimarisha imani yetu na kuruhusu roho ya Yehova ifanye kazi kwetu ili tutimize mapenzi yake. ‘Kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana’ hutufanya ‘tuimarike, tusitikisike.’—1 Kor. 15:58.

5 Katika nchi nyingi Shetani hujaribu kukengeusha muungamano wetu kwa kuvuruga kazi yetu ya kuhubiri. Yeye hutumia kila njia aipatayo ili kuanzisha kutopatana na kutokeza kutoelewana, ili kujaribu kufanyiza mashindano na mabishano. (Mit. 6:19; Gal. 5:19-21, 26) Yeye angetaka tujihusishe na ugomvi wa ulimwengu na hata tujiunge na masuala ya kisiasa na ya kijamii. (Yak. 3:14-16) Maandiko hutusihi tukinze athari yake; ama sivyo, atatumeza tukiwa windo lake. (1 Pet. 5:8, 9) Uhalisi wa tumaini la Ufalme haupaswi kuruhusiwa ufifie kutoka mioyoni na akilini mwetu.

6 Kudumisha muungamano wetu kwahitaji akili timamu na hekima kutoka juu. Magumu yatokeapo, hasa ikiwa yanahusu ndugu zetu, lazima tuonyeshe matunda ya roho ili kuendeleza amani. Vitabia vya kilimwengu, kama vile kiburi, wivu, na kujivuna, ni vyenye kugawanya na lazima vishindwe. (Efe. 4:1-3; Kol. 3:5-10, 12-14) Twahitaji kuweka akili zetu zikiwa zimejazwa na mawazo chanya, yenye kujenga. Ufalme ni halisi katika maisha zetu! Lakini twapaswa kuwa wenye bidii nyingi kuufanya uwe hivyo!—Efe. 6:11, 13.

7 Uhalisi wa tumaini letu ajabu la Ufalme hutuunganisha katika roho ya umoja ambayo haitakoma kamwe.—Zab. 133:1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki