Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/95 uku. 1
  • Je, Vikumbusha vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Vikumbusha vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wavipenda Mno Vikumbusha vya Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Makumbusha na Maagizo ya Mungu wa Mfumo Mpya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vikumbusho Vya Yehova Ni Vyenye Kutegemeka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Je, Hatujapata Kuyasikia Hapo Awali?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 7/95 uku. 1

Je, Vikumbusha vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?

1 Mtunga-zaburi alimsifu Yehova, akisema: ‘Vikumbusha vyako ndivyo nihangaikiavyo.” (Zab. 119:99, NW) Neno la Kiebrania la “vikumbusha” hutoa wazo la kwamba Yehova hutukumbusha yaliyoandikwa katika sheria zake, kanuni zake, masharti yake, na amri zake. Tukiziitikia, zitatuamsha kiroho na kutufanya tuwe na furaha.—Zab. 119:2.

2 Tukiwa watu wa Yehova, kwa kawaida sisi hupokea onyo la upole na shauri. Mengi yalo tumeyasikia mbeleni. Ingawa twathamini kitia-moyo hiki, twaelekea kusahau. (Yak. 1:25) Kwa saburi Yehova hutoa vikumbusha vyenye upendo. Mtume Petro alirekodi baadhi ya hivi vikumbusha ili ‘kuamsha uwezo wetu mwangavu wa kufikiri kwamba tukumbuke amri za Bwana.’—2 Pet. 3:1, 2.

3 Kwa kurudia-rudia twakumbushwa umuhimu wa funzo la kibinafsi na uhudhuriaji wa mikutano. Hilo lafanywa kwa sababu utendaji huu ni wa muhimu kwa hali yetu ya kiroho.—1 Tim. 4:15; Ebr. 10:24, 25.

4 Ugumu mkubwa zaidi kwa wengine ni kutimiza agizo la Kikristo la kuhubiri. Huhitaji jitihada, azimio, na uvumilivu. Hata ingawa hutaka mengi upande wetu, twasaidiwa ‘kusimama imara’ ‘miguu yetu ikiwa imefungwa vifaa vya habari njema ya amani.’—Efe. 6:14, 15, NW.

5 Utumishi wetu wapaswa kuchochewa na zaidi ya kujua kwetu kwa kiakili tu kuhusu matakwa ya Yehova. Mtume Paulo atukumbusha kwamba moyo huandaa uchocheo tunaohitaji ili “kukiri hata kupata wokovu.” (Rum. 10:10) Ikiwa tuna imani yenye nguvu na ikiwa moyo wetu unaelekea vikumbusha vya Yehova, tutasukumwa kuongea kwa kutolea sifa jina lake.—Zab. 119:36; Mt. 12:34.

6 Tunapofanya bidii katika kutenda kazi njema, sisi hutazamia vilivyo kwamba kufanya hivi kutatuletea shangwe. (Mhu. 2:10) Paulo hufafanua shangwe kuwa tunda la roho ya Yehova, na twapaswa kuendelea kuzidi katika kuionyesha. (Gal. 5:22) Petro aliongezea kwamba “jitihada yote” itathawabishwa na huduma yenye matokeo, inayotokeza shangwe.—2 Pet. 1:5-8.

7 Tunapokabiliwa na ugumu, twapaswa kukumbuka msimamo imara wa mitume kama walivyotangaza: “Hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” (Mdo. 4:20) Twatiwa nguvu kuendelea tunapokumbuka kwamba ‘kwa kufanya hivyo tutajiokoa nafsi yetu na wale watusikiao.’—1 Tim. 4:16.

8 Hatukasiriki au kuudhika kwa sababu ya kupokea vikumbusha vya mara kwa mara. Badala ya hivyo, twathamini kwelikweli thamani yao yenye kushinda. (Zab. 119:129) Katika nyakati hizi ngumu, twashukuru kwamba Yehova aendelea kutukumbusha ili kutuamsha kiroho na kutuchochea tuwe wenye bidii katika kazi nzuri!—2 Pet. 1:12, 13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki