Mikutano Ya Utumishi Kwa Julai
Juma Linaloanza Julai 3
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 17: “Fuliza Kulinda.” Maswali na majibu.
Dak 18: “Tumia Broshua Mbalimbali Katika Huduma Yako.” Zungumzia pamoja na wasikilizaji utoaji uliodokezwa. Toa maelezo mafupi juu ya sehemu zenye kupendeza za hizi broshua. Panga uwe na maonyesho mawili au matatu ya kuonyesha jinsi zinavyoweza kutolewa. Tia moyo pitio la utoaji huu kwenye mikutano ya utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Wimbo 213 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 10
Dak 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak 15: “Je, Vikumbusha vya Yehova Vyatuamsha Kiroho?” Maswali na majibu.
Dak 18: “Watoto ‘kwa Kuazimwa’—Zoea Hili Ni la Hekima Kadiri Gani?” Hotuba ishughulikiwe na mzee kuhusu habari iliyo katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1988, kurasa 28-30. Tafadhali fanya malinganisho na utumizi wa mahali penu juu ya kanuni kuhusu zoea la kupeleka watoto kwenye shule za bweni.
Wimbo 154 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 17
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 20: “Fanya Ziara za Kurudia kwa Maangusho Yote ya Broshua.” Ndugu aliyegawiwa sehemu hii atazungumza pamoja na wahubiri wengine watatu sababu ya umaana wa kufuatia kupendezwa na maangusho. Wanapitia utoaji uliodokezwa na kutoleana wonyesho wa jinsi yanavyoweza kutumiwa. Tia moyo wale wanaoongoza mikutano ya utumishi wa shambani mwisho-juma huu wapange kuwe na maonyesho ya utoaji ulioonyeshwa katika habari hii.
Dak 15: Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani. Hotuba ikitolewa na mzee anayeongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo. Tia moyo jitihada kubwa ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia madokezo yaliyotolewa katika Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 89-91. Unaweza kutia ndani mambo yaliyoonwa mafupi ya kwenu.
Wimbo 164 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 24
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia “Tutajifunza Kitabu Upeo wa Ufunuo Tena.” Kumbusha wote umaana wa kujifunza masomo mapema na kuhudhuria kwa ukawaida.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu. Au toa hotuba juu ya “Kuonyesha Upendo wa Kikristo kwa Wazee-Wazee,” ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1994, kurasa 27-30.
Dak 20: Jirani Watafikiri Nini? Hotuba na onyesho inayotegemea Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1974, kurasa 201-203 (Kiingereza). Toa hotuba juu ya ni kwa nini mara nyingi sisi husongwa na jirani walimwengu. (Shughulikia ukurasa 201 na fungu la kwanza kwenye ukurasa 202.) Kisha panga uwe na onyesho linaloonyesha wenzi wa ndoa walio na uzoefu kwenye funzo la Biblia wakiwa na familia yenye kupendezwa karibuni inayotishwa na jirani walimwengu ambao wanapinga kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. (Pitia mambo makuu katika sehemu iliyobaki ya hiyo makala.) Kazia sababu ambazo kwa nini familia yenye kupendezwa karibuni haipaswi kuvunjika moyo au kuacha.
Wimbo 169 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 31
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak 15: “Uwe Mwenye Kujenga.” Mazungumzo na hotuba ikitolewa na mzee.
Dak 20: Pitia Toleo la Fasihi la Agosti. Taja broshua zenye kurasa 32 ambazo zaweza kutumiwa. Alika wahubiri waeleze mambo yaliyoonwa yenye kupendeza wakitoa broshua wakati wa Julai. Toa onyesho la kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? Uliza swali linalotokezwa katika fungu la kwanza Sehemu ya 1. Pata itikio la mwenye nyumba juu ya mawazo yaliyoonyeshwa katika mafungu 2-4. Eleza kwamba hiyo broshua yaonyesha kwamba Mungu kweli anatujali na kwamba twaweza kufurahia maisha yasiyo na kuteseka katika ulimwengu mpya wake unaokuja. Jitolee kurudi kwa mazungumzo zaidi. Wote wanaoongoza mikutano ya utumishi wa shambani mwisho-juma huu wapaswa kupanga kuwe na mhubiri anayestahili atoe wonyesho wa utoaji huu.
Wimbo 179 na sala ya kumalizia.