Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 9/1 kur. 28-30
  • Watoto ‘Kwa Kuazimwa’ Zoea Hili Ni la Hekima Kadiri Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto ‘Kwa Kuazimwa’ Zoea Hili Ni la Hekima Kadiri Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu kwa Nini Wao Wanaazima Watoto
  • Mambo ya Kufikiria
  • Yale Mahitaji Muhimu ya Kiroho
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Wazazi, Fikieni Moyo wa Mtoto Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 9/1 kur. 28-30

Watoto ‘Kwa Kuazimwa’ Zoea Hili Ni la Hekima Kadiri Gani?

“KAMA ujuavyo, Danieli, mimi nina watoto wengi,” akasema binamu ya Danieli. “Kwa hiyo nimeamua kugawanya baadhi yao miongoni mwa watu wa ukoo.” Akielekeza kidole kwenye msichana mchanga aliyekuwa amekuja naye, binamu huyo akasema: “Huyu ni wako.”

“Asante,” akasema Danieli. Hata hivyo, kwa ndani, yeye aliugua. Alikuwa ana watoto wa kumtosha yeye mwenyewe na hakutaka wala hakuhitaji zaidi. Lakini kulingana na desturi ya kwao, kukataa toleo hilo kungalifikiriwa kuwa kosa zito​—jambo lisilofikirika kwamba laweza kutendwa! Sasa Danieli akawa ana binti mwingine wa kutunza.

Katika mabara mengi yanayositawi, hususa katika Afrika, si jambo lisilo la kawaida kwa wazazi kuazima watoto wao kwa watu wa ukoo au marafiki kwa muda wa miezi, miaka​—na nyakati fulani kwa wakati usio dhahiri. Desturi hiyo huenda ikasikika kuwa ya kiajabu kwenye masikio ya watu wa Magharibi, lakini kwa kanuni inafanana na lile zoea la kupeleka watoto waende zao kwenye shule za kulala au kambi za majira ya kiangazi kukaa huko kwa muda mrefu. Ingawa hivyo, ni nini kinachochochea desturi ya kuazima watoto? Je! ni zoea la hekima?

Sababu kwa Nini Wao Wanaazima Watoto

Ingawa thamani za kimapokeo zinabadilika, kwa Mwafrika, watoto si mali ya wazazi peke yao. Bali, wao ni wa jamaa ya mlolongo. Akina shangazi, wajomba na ami, akina babu na nyanya, na wengine wanafikiriwa wote kuwa wana haki na mamlaka juu ya watoto. Kama vile mithali moja ya Afrika Magharibi inavyotaarifu: “Mtu mmoja ndiye huzaa, lakini wengi ndio humtunza mtoto.”

Tokeo ni kwamba, wakati hali za dharura zinapotokea, kama vile kifo cha wazazi wa mtoto, watu wa ukoo wanakuwa na utayari na nia ya kuchukua yule mtoto yatima. Hata hivyo, kwa kawaida sababu ya msingi ya kuazima watoto kwa watu wa ukoo ni ya kipesa. Wakati jamaa inapokuwa ni maskini na watoto ni wengi, huenda wazazi wakahisi kwamba mmoja au zaidi kati ya watoto atanufaika kwa kuishi pamoja na watu wa ukoo walio na mali kidogo. Wao wanawaza kwa kusababu kwamba mtu huyo wa ukoo ataona ni rahisi zaidi kupata karo ya shule, nguo, dawa, na chakula. Kwa hiyo si ukosefu wa upendo wa kiuzazi, bali ni tamaa ya kuandalia watoto wao vitu vilivyo bora zaidi inayosukuma wazazi fulani wakabidhi watoto wao kwa wengine.

Sababu nyingine ni tamaa ya kwamba watoto wapate elimu nzuri. Labda shule iliyo karibu zaidi iko mbali na maskani ya jamaa. Kwa kuwa huenda ikawa vigumu au huenda isiwezekane kwa jamaa nzima kuhama, huenda wazazi wakawaza kwa kusababu kwamba jambo bora zaidi lingekuwa kupeleka mtoto wao kwa watu wa ukoo wanaoishi karibu na shule fulani.

Kwa ujumla watu wa ukoo hufurahi kukubali watoto hao. Miongoni mwa mambo mengine, kupata kinywa kingine cha kulisha kunamaanisha pia kupata mikono mingine miwili ya kufanya kazi za hapo nyumbani. Na nyakati fulani wazazi wanasaidia gharama kwa kupeleka pesa au chakula.

Mambo ya Kufikiria

Ingawa ni kweli kwamba huenda kukawa kuna faida fulani za kielimu na kimwili za kuazima mtoto kwa wengine, kuna mambo mengine yanayostahili mfikirio wa uangalifu. Kwanza, ni jinsi gani mtoto huyo atajirekebisha apatane na hali za watunzaji wake wapya, na ni jinsi gani wao watajirekebisha wapatane na hali za mtoto? Nyakati fulani mipango kama hiyo inaendelea vizuri, na wale wazazi wapya wanafanyiza mahusiano imara yenye upendo pamoja na watoto wao wa kambo. Mathalani, mzee mmoja Mkristo katika Sierra Leone alikubali kuchukua mpwa wake wa kiume aliye yatima. Alipoulizwa miaka kadhaa baadaye juu ya mwana wake wa kambo, yeye alijibu hivi: “Mimi simfikirii Desmond kuwa mtoto wa kambo​—yeye ni mwana wangu. Yeye ni mnofu na damu yangu.”

Hata hivyo, si wote wanaoona watoto wao wa kambo kwa njia hiyo. Kutoa kielezi kimoja, katika jiji moja la Afrika Magharibi kulikuwa na fujo-fujo za wanaghasia. Risasi zilikuwa zikiruka hewani. “Fanya haraka!” akapiga yowe mke mmoja mshughulikia kazi za nyumbani, akiambia watoto wake wawili hivi: “Arthur, jifiche chini ya kitanda! Wewe, Sorie, tazama nje ya dirisha utuambie kuna nini!” Arthur alikuwa mtoto wake wa kiasili, lakini Sorie alikuwa mtoto wa kambo, au mtoto mtunzwa.

Ni jambo la kawaida watoto wa kiasili katika jamaa kutendewa afadhali zaidi. Tokeo ni kwamba, zile manufaa zinazotamaniwa sana huwa mara nyingi hazitimii. Mara nyingi mno watoto watunzwa wanafanyishwa kazi kupita kiasi, wananyimwa elimu, na ndio wanaokuwa wa mwisho katika mstari wa kupokea nguo na pia matibabu na ukaguzi wa meno yao. Alisema hivi misionari mmoja ambaye amefanya kazi katika Afrika kwa miaka zaidi ya 23: “Karibu sikuzote watoto watunzwa huwa ni watoto wa daraja la pili.”

Wazo jingine la kufikiria: Wakati mtoto anapoondoka kwenye maskani yao, kwa kawaida kunakuwa na gharama za hisia-moyo. Akili na mioyo ya watoto hugusika na kuvutiwa-vutiwa na mambo kwa urahisi. Tangu utoto mchanga wao wanatamani sana faraja na usalama wa uhusiano wa karibu pamoja na wazazi wao. Watoto kung’olewa kwenye maskani yao ili waende wakaishi pamoja na watu wasiowajua sana linaweza kuwa jambo gumu kupita kiasi.

Katika Sierra Leone mwanamke mmoja jina lake Comfort alipelekwa aende zake kuishi pamoja na shangazi yake akiwa na umri wa miaka tisa. Yeye anakumbuka hivi: “Ile miaka niliyotumia nikiwa mbali na maskani yetu ilikuwa migumu sana. Mimi nilihisi nikisikitika sana sana kutokuwa na jamaa yetu​—hasa ndugu na dada zangu. Ilikuwa kama kwamba wao walinikwangusha nitoke mahali nilipopaswa kuwa na wakaniweka mahali nisipopaswa kuwa. Ingawa shangazi yangu alinitendea vizuri, sikuweza kamwe kuongea naye kwa uhuru kadiri ile ile ambayo ningeweza kuongea na mama yangu mwenyewe. . . . Hata hali ije kuwa ngumu namna gani, mimi sitapeleka kamwe watoto wangu wakaishi pamoja na mtu mwingineye yote.”

Francis, mtu mmoja wa Afrika Magharibi ambaye pia alikua akiwa katika utunzaji wa mzazi wa kambo, alisema hivi: “Mimi najuta kwamba sikuweza kamwe kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na mama yangu halisi. Kidogo, mimi nahisi sisi wote wawili tulikosa jambo fulani la kuthamanika.”

Yale Mahitaji Muhimu ya Kiroho

Hata hivyo, jambo lililo na umaana mkubwa kuliko yote ni masilahi ya kiroho ya mtoto. Na Mungu katika hekima yake anaelekeza kwamba wazazi wenyewe ndio watunze mahitaji ya kiroho ya watoto wao. Akiambia wazazi Waisraeli, shauri la Mungu lilikuwa hili: “Maneno haya ambayo mimi naamuru wewe leo lazima yathibitike kuwa juu ya moyo wako; na wewe lazima uyakaze kikiki katika mwana wako na kunena juu yayo wakati wewe unapoketi katika nyumba yako na wakati wewe unapotembea barabarani na wakati wewe unapolala na wakati wewe unapoamka.” (Kumbukumbu 6:6, 7, NW) Vivyo hivyo mtume Paulo aliwaagiza baba Wakristo hivi: “Msiwe mnaudhi-udhi watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.”​—Waefeso 6:4, NW.

Lakini ni jinsi gani mtoto anavyoweza kulelewa “katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova” ikiwa yeye amepelekwa akaishi pamoja na watu wa ukoo? Basi, ni kutojali mambo ya wakati ujao kama nini kudhabihu masilahi ya kiroho ya mtoto kwa ajili ya manufaa za kimwili au za kielimu!

Namna gani juu ya kupeleka mtoto akaishi pamoja na waitikadi wenzetu? Ingawa hiyo ni afadhali kuliko kuwaazima kwa wasio waitikadi, kwa njia nyingi jambo hilo pia halitamaniki. Huenda bado mtoto akalazimika kukabiliana na marekebisho makubwa-makubwa ya kijamii, kihisia-moyo, na hali ya akilini. Watoto fulani wamekata tumaini au wakatumbukia katika kutotii na ushirika mbaya. Baadhi yao wamepoteza uthamini wote kwa mambo ya kiroho.

Kama vile wazazi wanavyojua sana, inataka ustadi, saburi, na wakati mwingi ili kukaza ndani ya mtoto upendo kwa Yehova. Ikiwa fungu hilo la kikazi ni gumu kwa wazazi asilia wa mtoto, ambao wanamjua kindani au tangu kuzaliwa, ni gumu kama nini kwa wazazi wawili kulea mtoto ambaye si wao wenyewe! Kwa kuwa uhai wa milele wa mtoto huenda ukawa hatarini, ni lazima wazazi wafikirie kwa uzito na kwa sala kama kuazima mtoto kwa mtu mwingine kunastahiki zile hatari zilizopo.

Hata hivyo, ni lazima wazazi Wakristo wajiamulie wenyewe jinsi watakavyotekeleza lile shauri la 1 Timotheo 5:8, NW; “Kwa uhakika ikiwa mmoja ye yote haandai riziki kwa ajili ya wale ambao ni wake mwenyewe, na hasa kwa ajili ya wale ambao ni washiriki wa watu wa nyumba yake, yeye amekataa uenyeji wa ile imani na ni mbaya kuliko mtu asiye na imani.” Ikiwa wao binafsi hawawezi kuandaa mahitaji ya kimwili ya mtoto, inawapasa wahakikishe kwamba mahitaji ya kiroho ya mtoto wao yanatimizwa kwa njia bora zaidi iwezekanayo chini ya mastakimu zilizopo.

Mtunga zaburi aliandika hivi: “Watoto ni kipaji kutoka kwa Mungu; wao ni thawabu yake.” (Zaburi 127:3, The Living Bible) Kwa hiyo tunza sana watoto wako, na waweke karibu na wewe. Wapende, na acha wao wakupenda wewe. Wasaidie kuwa wanaume na wanawake wa kiroho, kwa maana kufanya hivyo kutatokeza baraka yao ya milele. Labda wewe utaweza kusema hivi, kama vile Yohana alivyosema juu ya watoto wake wa kiroho: “Hakuna kisababishi kikubwa zaidi cha ushukuru ambacho mimi ninacho kuliko mambo haya, kwamba mimi nipaswe kuwa ninasikia kwamba watoto wangu wanaendelea kutembea katika ule ukweli.”​—3 Yohana 4, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki