Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 12/1 uku. 23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Watoto ‘Kwa Kuazimwa’ Zoea Hili Ni la Hekima Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Wazazi, Fikieni Moyo wa Mtoto Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 12/1 uku. 23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

◼ Ni jambo la hekima kadiri gani kupeleka mtoto wako akaishi na watu wa ukoo walimwengu kwa sababu tu wanaweza kumpa mtoto huyo faida za kimwili?

Maandiko yanaonyesha kwamba wazazi wana pendeleo na daraka la kuwatunza watoto wao, kutia kuwapa uangalizi wa kiroho unaohitajiwa. Kungekuwa kukosa hekima kwa mume na mke Wakristo kupuza mgawo huo waliopewa na Mungu ili tu mtoto apate faida za kimwili kwa kuishi na mtu wa ukoo asiye Mkristo.

Katika nchi nyingine ni jambo la kawaida sana kupeleka mtoto akaishi na watu wa ukoo kwa vipindi virefu. Mara nyingi jambo hilo hufanywa na wazazi wanaoishi katika maeneo yaliyo mbali peke yake ambako mipango ya elimu ni michache. Wanampeleka mtoto kwa watu wa ukoo katika mji fulani (au shule ya bweni) ili mtoto huyo apate elimu bora zaidi au afaidike na hali ya juu ya maisha. Kwa kawaida mtoto huyo anatazamiwa afanye kazi ya nyumbani au awalipe watu hao wa ukoo kwa njia nyingine kwa ajili ya kumruhusu katika nyumba yao.

Inadhaniwa mpango huo una faida nyingi za kimwili, lakini huenda zisiwe nyingi kama inavyodhaniwa. Mara nyingi mambo yaliyoonwa yameonyesha kwamba kuna matokeo mabaya juu ya mtoto anapoondolewa kutoka kwa mazingira anayofahamiana nayo na kulazimishwa akaishi na watu wa ukoo mbali na wazazi wake. Mara nyingi, badala ya mtoto huyo kutendewa sawa na watoto wengineo katika nyumba hiyo, yeye huonwa kuwa mfanyi kazi wa nyumbani na anabaguliwa. Unaweza kuwazia kwamba, kijana anapokuwa na sababu au asipokuwa nayo, ya kuhisi anadhulumiwa, wakati mwingi matokeo yanakuwa ni kushuka moyo na kuwa na uchungu. (Linganisha Mwanzo 27:30-41.) Mvurugo wa moyoni unatokea na ukosefu wa furaha unaweza kuingiliana na kadiri ya mambo anayojifunza, hata ingawa anahudhuria shule nzuri. Kwa hiyo je, kweli kweli anafaidika? Ukosefu wa utii ni jambo jingine linalotokea kwa kawaida mtoto anaponyimwa nidhamu ya kawaida inayohitajiwa kutoka kwa wazazi wenye upendo.

Mashauri ya Neno la Mungu yanasaidia kuzuia matokeo hayo mabaya. Jambo moja ni kwamba Biblia inawasihi wazazi wawatunze watoto wao wenyewe. Bila shaka, Yehova Mungu alitambua kwamba hali fulani zisizo za kawaida zingetokea ambamo katika hizo watu wengine licha ya wazazi wangelazimika kutunza watoto.a Kwa hiyo, yeye aliwashauri watumishi wake wawasaidie yatima au wale waliofiwa na wazazi wote wawili. (Kumbukumbu la Torati 14:28, 29; 16:9-14; 24:17-21; 26:12, 13; Zaburi 10:14; Yakobo 1:27) Lakini mkazo mkuu katika Maandiko ni kwa wazazi kuangalia mahitaji ya kimwili, kiroho na kimoyoni ya watoto wao wenyewe.​—Linganisha 1 Timotheo 5:8.

Mungu aliwashauri wazazi juu ya maneno yake hivi: “Yafunzeni vijana vyenu kwa kuyazungumza uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na [uamkapo].” (Kumbukumbu la Torati 11:18, 19) Je! wazazi wangeweza kufanya hivyo ikiwa kwa hiari yao waliwapeleka watoto mbali kwa watu wa ukoo kwa vipindi virefu? Hapana, wazazi wanahitaji kuwa na watoto wao ili wawape kwa ukawaida masahihisho na maagizo ya ki-mzazi, pamoja na mazingira ya upendo ambayo vijana wanahitaji. (Waefeso 6:4; Mithali 6:20) Kwa wazi, masilahi yenye kuendelea (hata ya milele) ya mtoto Mkristo hayangeendelezwa ikiwa angetumwa akaishi na watu wa ukoo walimwengu kwa ajili ya elimu ya kidunia, kwa hasara ya maagizo ya kiroho katika nyumba yake mwenyewe. Wakristo duniani pote wanajua kwamba katika mfumo huu wa mambo kumlea kijana amtumikie Yehova ni kazi ngumu, inayohitaji usimamizi wa ki-mzazi wakati wote. Hakika taraja la kufanikiwa lingepunguka ikiwa mtoto angepelekwa mbali na nyumba ya Kikristo kwa ajili ya faida za kimwili tu.

Kwa habari hiyo fikiria mfano wa Yesu, ambaye alilelewa katika mji ulio mbali peke yake wa Nazareti katika Galilaya. Wakiwa wanamtii Mungu, Yusufu na Mariamu walikaa na Yesu katika Nazareti, ambako ‘aliendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.’​—Luka 2:41-52.

Mfumo wa mambo uliopo unakazia elimu na kufanikiwa kifedha. Wazazi walimwengu wanasikiwa wakisema mambo kama, ‘Sitaki mwanangu akue awe tarishi.’ Hata wazazi Wakristo wanaweza kuambukiwa na maoni kama hayo kuhusu elimu na faida za kimwili. Lakini wazazi wanaotumaini hekima ya Yehova wataweka kwanza kwa watoto wao “msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli.”​—1 Timotheo 6:9, 19.

[Maelezo ya Chini]

a Hali inayotokea mara chache na inayohuzunisha ni ile ya msichana mchanga anayezaa mtoto baada ya kulalwa kinguvu. Wale wanaohusika hasa, msichana huyo na wazazi wake, wanaweza kuamua mwendo wa hekima ni nini kuhusiana na mambo yote yaliyopo, kutia hali ya kimwili na ya moyoni ya msichana huyo. Katika visa vingine kama hicho kitoto kimekubaliwa na kulelewa kwa upendo kwa njia ya Kikristo katika jamaa ya msichana huyo. Katika visa vingine wenzi wengine Wakristo wanaotaka kutunza mtoto, na wakiweza kufanya hivyo, wameruhusiwa kumlea mtoto huyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki