Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/95 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 8/95 uku. 7

Matangazo

◼ Fasihi ya kutumiwa wakati wa Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Septemba: Kitabu Kuishi Milele kitatumiwa, na jitihada zapasa kufanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani. Oktoba: Maandikisho ya Amkeni! au Mnara wa Mlinzi. Novemba: Toa New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa kufanya hivyo katika Agizo la Fasihi lao la kila mwezi litakalofuata (S-14-SW).

◼ Ugavi wa kutosha wa fomu za kutumia wakati wa mwaka wa utumishi wa 1996 zinapelekwa kwa kila kutaniko. Fomu hizi hazipaswi kutumiwa vibaya. Zapaswa kutumiwa tu kwa kusudi lazo.

◼ Kila kutaniko litapokea fomu tatu za Orodha ya Vitabu (S-18-SW). Mwandishi wa kutaniko anapaswa kukutana na mtumishi wa fasihi mapema katika Agosti na kuweka tarehe ya kuhesabu fasihi zote zilizo akibani za kutaniko mwishoni mwa mwezi. Hesabu kamili yapaswa kufanywa ya fasihi zote zilizo akibani, na jumla yapaswa kuingizwa kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu. Jumla ya hesabu ya magazeti yaliyopo yaweza kupatikana kutoka kwa mtumishi wa magazeti. Tafadhali pelekeni ile nakala ya kwanza kwa Sosaiti si baada ya Septemba 6. Wekeni nakala ya kaboni kwa ajili ya faili yenu. Nakala ya tatu yaweza kuwa ya kufanyia kazi. Kazi hiyo ya kuchukua hesabu ya orodha yapasa kusimamiwa na mwangalizi-msimamizi. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi watatia sahihi fomu hiyo.

◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza 1996 Calendar of Jehovah’s Witnesses pamoja na ombi lao la fasihi la Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kiingereza na Kifaransa.

◼ Kuanzia Agosti 29, 1995, hadi Septemba 1, 1995, Sosaiti itakuwa ikihesabu fasihi zote zilizomo. Kwa sababu ya kuhesabu huku, hakuna maagizo yoyote ya fasihi ya kutaniko yatakayofanyiwa upakizi au yatakayochukuliwa siku hizo.

◼ Wahubiri wanaopanga kuanza utumishi wa painia wa kawaida Septemba 1, 1995, wapaswa kujaza maombi bila kuchelewa.

◼ Mwandishi wa kutaniko atakusanya ripoti za utumishi kwa ajili ya kuingiza kwenye fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kutaniko (S-10-SW). Pia ataagiza kwa uangalifu mzee yeyote au mtumishi wa huduma ambaye anaweza kusaidia kukusanya ripoti. Hilo litahakikisha hesabu sahihi ya habari inayohitajiwa kutoka kwa Maandishi ya Mhubiri wa Kundi (S-21-SW). Fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kutaniko (S-10-SW) yapasa kujazwa kwa usahihi na unadhifu na ichunguzwe vizuri na halmashauri ya utumishi.

◼ Ziara za matembezi kwenye jengo la Betheli ya Nairobi zawezekana kila siku ya kazi kati ya saa 2:00 asubuhi na saa 6:00 mchana na kati ya saa 7:00 na 11:00 alasiri. Ziara ya matembezi ya wakati huu huchukua muda upatao zaidi ya nusu saa ili kukamilika hivyo hakikisha unakuwa na wakati wa kutosha kati ya vipindi vilivyoonyeshwa juu.

◼ Kwa sasa hakuna mipango ya ziara za matembezi mahali pa ujenzi wa Betheli mpya. Mtajulishwa mipango ifanywapo ya ziara za matembezi za mahali hapo.

◼ Kila baraza la wazee laombwa kupitia agizo la magazeti la kutaniko ili kuona kama kuna magazeti ya kutosha ya kutumiwa katika huduma na vilevile kwa makusudi ya funzo.

◼ Waandishi wa kutaniko wanakumbushwa kutoa S-3, Ripoti ya Funzo la Biblia, kwa kiongozi hususa wa Funzo la Kitabu la Kutaniko. Jambo hilo litaandaa usimamizi mzuri na usaidizi kwa sehemu ya huduma yetu ya mafunzo ya Biblia nyumbani.

◼ Mkusanyiko wa Wilaya wa Kiluganda umeratibiwa upya kuwa Desemba 1-3, 1995, Kampala.

◼ Wakati wa mwezi huu wa kwanza wa kampeni ya eneo lililo pekee wote wanatiwa moyo kutumia toleo la pekee la kitabu Kuishi Milele kama ilivyotangazwa katika barua ya tarehe 7 Juni 1995 ya Sosaiti kwa makutaniko yote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki