Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/95 uku. 7
  • Msifuni Yehova kwa Shangwe Siku kwa Siku!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msifuni Yehova kwa Shangwe Siku kwa Siku!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Waliotengwa Wawe Wasifaji Wenye Shangwe Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu
    Mwimbieni Yehova
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Enyi Vijana, Msifuni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 9/95 uku. 7

Msifuni Yehova kwa Shangwe Siku kwa Siku!

1 Mbingu zenye kutisha hutangaza utukufu wa Yehova “siku moja baada ya siku nyingine.” (Zab. 19:1-3, NW) Ikiwa viumbe visivyo hai, ambavyo havina sauti humtolea Yehova sifa daima, je, sisi wanadamu wenye akili hatupaswi kuhisi kusukumwa kuinua sauti zetu katika kumsifu yeye nyakati zote kwa sababu ya sifa zake na mambo ambayo ametimiza yasiyoweza kufananishwa? Ni nani anayestahili zaidi sifa yetu yenye shangwe kuliko Muumba wetu mtukufu?—Zab. 145:3, 7.

2 Siku kwa Siku: Mtunga-zaburi aliyepuliziwa aliandika hivi: “Simulieni siku kwa siku habari njema ya wokovu utolewao naye. Kwa kuwa Yehova ni mkubwa na apaswaye kusifiwa sana sana.” (Zab. 96:2, 4, NW) Je, hili lahusu mapainia peke yao? La! Je, hili lamaanisha kwamba sisi sote twapaswa kuongea na wengine juu ya Yehova wakati wowote na popote tuwezapo, hata siku ambazo hatushiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba? Ndiyo! Uhitaji wa kumsifu Yehova kila siku na kuongea na wengine juu ya njia yake ya wokovu ni jambo la haraka. Ni lazima watu wajue kwamba Yehova ndiye Mfalme wa Milele na kwamba Yeye amempa Mwana Wake, Yesu Kristo, aliyetukuzwa, utawala wa ulimwengu. Kumpenda Yehova na watu kutatufanya tuendelee kuongea juu ya ujumbe huu na juu ya maandalizi yake kwa ajili ya wokovu popote ambapo watu waweza kupatikana.—Zab. 71:15.

3 Kila siku ya huduma yake ya kidunia, Yesu Kristo aliweka kielelezo chema zaidi akiwa msifaji wa Yehova mwenye kusema mambo waziwazi. Yeye alisema hivi: “Nakusifu wewe hadharani, Baba, Bwana wa mbingu na dunia.” (Mt. 11:25, NW) Kwa kupatana na neno lake, popote alipokuwa, yeye alimsifu Yehova hadharani. Na popote ambapo umati ulikuwa ukikusanyika—iwe ni katika masinagogi, kwenye hekalu Yerusalemu, juu mlimani, au ufuoni—yeye alimsifu Yehova. Tukifuata nyayo za Yesu kwa ukaribu kwa kudumisha kila siku, utendaji wenye upatano katika kumtukuza Yehova hadharani, tutakuwa na matokeo yenye shangwe na furaha.

4 Kuuitikia Wito Huo: Je, wewe utauitikia wito wa kumsifu Yehova hadharani kila siku? Kumbuka, umri si kizuizi. Zaburi 148:12 hualika wanaume vijana, mabikira, wanaume wazee, na wavulana wamsifu Yehova. Vijana, je, mtamsifu Yehova miongoni mwa wanashule wenzenu na walimu wakati wa muhula huu mpya wa shule? Watu wazima, je, wale mnaofanya kazi nao mahali ambapo mmeajiriwa husikia juu ya Yehova na makusudi yake, wakati ambapo kunakuwa na pindi ifaayo ya kuongea pamoja? Sisi sote twapaswa kufanya jambo la kuongea juu ya Yehova liwe sehemu kubwa ya maisha yetu kama vile kupumua na kula kulivyo. Hata ikiwa watu wenye ubaridi hawasikilizi yale tunayosema, kuna Mmoja anayesikiliza, naye atatuthawabisha.—Mal. 3:16.

5 Mwisho wa mfumo huu ukaribiapo, wito huu watoka hadi kwenye miisho ya dunia: “Sifuni Yah, enyi watu!” (Zab. 106:1, NW) Mpaazo wetu wa sifa na uwe wenye sauti kubwa zaidi kila siku ipitapo ili wote wapate kujua kwamba Yule ambaye jina lake ni Yehova ndiye Aliye Juu Zaidi Sana juu ya dunia yote.—Zab. 83:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki