Matangazo
◼ Fasihi ya kutumiwa wakati wa Novemba: Toa New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1982 ambacho kutaniko laweza kuwa nacho akibani. Makutaniko ambayo hayana akiba ya vitabu hivyo yaweza kutoa Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Februari: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! waweza kutolewa. TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza bidhaa za kampeni zilizotajwa hapo juu yapaswa kufanya hivyo kwenye Fomu ya Kuomba Fasihi (S-14-SW) ya kila mwezi inayofuata.
◼ Marekebisho yamefanywa kwa tarehe za mkusanyiko wa wilaya Uganda: Mkusanyiko wa Kampala wa Kiingereza utafanywa Desemba 29-31, 1995. Mkusanyiko wa Kampala wa Kiganda na mkusanyiko wa Mbale yote miwili imeratibiwa kufanywa Januari 5-7, 1996.
◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza kitabu Kitabu-Mwaka cha Mashahidi wa Yehova—1996 pamoja na agizo lao la fasihi la Novemba. (Ona Orodha ya Bei, fungu 10.) Kitabu Kitabu-Mwaka kitapatikana katika Kiarabu, Kifaransa, na Kiingereza.