Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/95 uku. 7
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 12/95 uku. 7

Sanduku La Swali

◼ Ni nani wawezao kutumiwa kusoma mafungu wakati wa Funzo la Kitabu la Kutaniko na Funzo la Mnara wa Mlinzi?

Huduma ya Ufalme Yetu ya Agosti 1977 na Julai 1980 (Kiingereza) zilieleza ni nani wanaostahili kuwa wasomaji. Ndugu waliobatizwa hutumiwa wapatikanapo. Wanapaswa kuchaguliwa kutoka miongoni mwa wazee wenye uwezo, watumishi wa huduma, na ndugu wengine waliobatizwa kutanikoni. Wale wanaopewa mgawo huo wapaswa kuweza kusoma kwa ufasaha, kwa kukazia maana vizuri na ubadilifu wa sauti. Wapaswa kuwa wenye idili na kuonyesha sifa za usemi zinazohitajiwa kama ionyeshwavyo katika kitabu Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, sura 6. (Linganisha Nehemia 8:8.) Pia wapaswa kuwa vielelezo vizuri katika mwenendo wao.

Kwa kuwa funzo la kitabu ni mkutano mdogo kuliko mikutano mingine, huenda kusiwe sikuzote na ndugu anayestahili, aliyebatizwa wa kusoma. Katika hali kama hizo, kiongozi wa funzo aweza kuamua kusoma mafungu yeye mwenyewe, au aweza kumwomba dada anayestahili, aliyebatizwa asomaye vizuri asaidie. Dada akisoma, haingekuwa lazima kwake kuvaa kitambaa cha kichwa, kwa kuwa hatumikii katika fungu la kufundisha. Bila shaka, aweza kufanya hivyo ikiwa ahisi starehe zaidi.

Kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi, yaelekea zaidi kuna ndugu wanaostahili wapatikanao wa kusoma. Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi apaswa kutengeneza ratiba ya wasomaji mapema na kuibandika kwenye ubao wa habari. Ni daraka la baraza zima la wazee kuchagua wale watakaogawiwa kusoma kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi. Ndugu akiwa hasomi vizuri, kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi apaswa kuchukua hatua ya kumpa onyo la upole lenye fadhili na usaidizi. Orodha ya wasomaji yaweza kurudiwa mara nyingi kama ihitajiwavyo ili kuhakikisha kwamba ubora wa kusoma unadumishwa ukiwa juu. Ndugu akiondoshwa kwenye orodha, apaswa kujulishwa sababu na sifa anazohitaji kufanyia maendeleo ili astahili tena.

Kama ni kusomea kikundi kidogo kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko au kutaniko zima kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi, yule aliyepewa mgawo apaswa kuchukua mgawo huu kwa uzito. (1 Tim. 4:13) Apaswa kuongea kwa usadikisho, akisoma kwa ustadi katika njia ambayo itaonyesha ifaavyo “maneno [sahihi] ya kweli.”—Mhu. 12:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki