Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/96 uku. 2
  • Msifuni Mungu Katika Patakatifu Pake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msifuni Mungu Katika Patakatifu Pake
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 3/96 uku. 2

Msifuni Mungu Katika Patakatifu Pake

1 Sifa ya utakatifu ni ya Yehova. (Kut. 39:30; Zek. 14:20) Ndiyo sababu Yehova amewaambia watumishi wake: “Lazima mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.” (1 Pet. 2:16, NW) Kwa kuwa Yehova Mungu ndiye Mwanzilishi wa kanuni na sheria zote za uadilifu (Yak. 4:12) naye ndiye msingi wa utakatifu wote, mtu yeyote au kitu chochote kilicho kitakatifu huwa hivyo kwa sababu ya Yehova na ibada yake. (it-1 kurasa 1127-1130) Kwa hiyo, sisi hukumbuka mahali petu pa ibada tunaposoma Zaburi 150:1: ‘Msifuni Mungu katika patakatifu pake.’

2 Udumishaji wa Jumba la Ufalme: Ni vizuri kuona kwamba makutaniko mengi yameanza kujenga Majumba ya Ufalme. Kujenga mahali pa ibada kwa Yehova ni jambo zuri, kudumisha mahali hapo pakiwa safi na penye uzuri ni utakatifu. (Isa. 64:11) Ndiyo sababu, uangalifu wa daima wapaswa kukaziwa, na jitihada nyingi yapaswa kuwekwa ili kuboresha hali ya Jumba la Ufalme na mazingira yalo.

3 Watu Wanaoweka Kielelezo: Tulipokea shauri zuri sana katika Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1993, kuhusu udumishaji na utunzaji wa Jumba la Ufalme. Twaona kuwa jambo linalofaa na la lazima kuandaa miongozo tuliyopewa kuhusu jambo hili.

4 “Wazee na watumishi wa huduma huweka kielelezo kwa bidii katika kuonyesha staha kwa Jumba la Ufalme. Kwa kawaida kuna mzee mmoja au wawili na watumishi wa huduma wanaopewa mgawo wa kuratibu mambo yanayohusu utunzaji wa Jumba la Ufalme. Mahali ambapo zaidi ya kundi [kutaniko] moja linatumia jumba lilelile, halmashauri ya wazee husimamia mambo hayo:

5 “Ingawa watu fulani wamepewa mgawo hususa wa kutunza wajibu huo mbalimbali, watumishi wa huduma na wazee wote wanapaswa kuonyesha kupendezwa kikweli na jumba. Wanatambua kwamba Jumba la Ufalme limewekwa wakfu kwa Yehova na hutumiwa kwa ajili ya ibada yake.

6 “Wazee hawapaswi kukawia-kawia wakati marekebisho yanapohitaji kufanywa. (2 Mambo ya Nyakati 24:5, 13; 29:3; 34:8; Nehemia 10:39; 13:11) Katika baadhi ya makundi [makutaniko] ukaguzi wa kawaida wa Jumba la Ufalme hufanywa ili kushughulika upesi na marekebisho yoyote yanayohitajiwa. Orodha zinawekwa ili kuhakikisha kwamba vifaa vinavyohitajiwa vyapatikana na vyafikika kwa urahisi. Ikiwa kuna mahali maalumu pa kuwekea vifaa, vyombo vya kufanyia kazi, na vyombo vya kusafishia, wazee na watumishi wa huduma wote wanapaswa kuonyesha kupendezwa na hali yavyo, wakihakikisha kwamba vyote vimewekwa kwa unadhifu. Wale wanaofanya kazi kwenye kaunta za fasihi na magazeti wanaweza kuonyesha kupendezwa kwao kwa kuhakikisha upesi kwamba makatoni matupu hayachafui jumba.

7 “Kwa kuweka kielelezo kizuri, wazee na watumishi wa huduma wanaweza kuwasaidia wengine kundini [kutanikoni] wadhihirishe bidii kwa ajili ya Jumba la Ufalme. (Waebrania 13:7) Wote wanaweza kuonyesha staha kwa kushiriki sehemu fulani katika kusafisha jumba na kwa kuonyesha kupendezwa kikweli na sura yalo ya ujumla.

8 “Yesu alisema hivi kwenye Mathayo 18:20: ‘Walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.’ Naam, Yesu anapendezwa na yale tunayofanya tunapokusanyika pamoja ili kumwabudu Yehova. Hilo latia ndani mikutano yoyote inayofanywa kwenye nyumba za faragha na mikutano mikubwa kama vile mikusanyiko au makusanyiko.

9 “Kwa mamilioni ya Mashahidi wa Yehova, hapana mahali palipo karibu zaidi na moyo wao kuliko mahali pao pa kawaida pa ibada, Jumba la Ufalme. Wanaonyesha staha ifaayo kwa mahali hapo. Wanadhihirisha roho ya bidii katika kupatunza, na wanajitahidi sikuzote kupatumia ifaavyo.” Wewe pia na ufuate lile himizo: ‘Msifuni Mungu katika patakatifu pake.’—Zab. 150:1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki