Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi
Juma Linaloanza Machi 4
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu na Habari za Kitheokrasi.
Dak 15: “Mbariki Yehova ‘Mchana Kutwa.’” Maswali na majibu. Soma mafungu 2-5 kadiri wakati uruhusuvyo. Toa kitia-moyo kinachofaa kwa kazi ya upainia-msaidizi na upainia wa kawaida.
Dak 20: “Kutoa Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.” Kwa idili pendekeza kutoa kitabu kipya, hasa kwa wale ambao wameonyesha kupendezwa wakati uliopita. Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa, na uwe na wonyesho mmoja au mawili.
Wimbo 78 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 11
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak 20: “Nufaika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996—Sehemu ya 3.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Tia moyo wote wanaoweza wajiandikishe na kutimiza migawo yao kwa uaminifu. Eleza matakwa ya kutamka majina ya Biblia katika Kiingereza waziwazi, kama ipatikanavyo katika kitabu “Kila Andiko,” kurasa 325-326, mafungu 27-28. Pia eleza kwamba muunganisho wa “ch” katika majina hutamkwa kwa mkazo, kama “k” (Isipokuwa katika Rachel, ambapo “ch” hutamkwa kwa njia isiyo ya mkazo.) Onyesha usomaji mzuri kwa kuweka sehemu ya Kitabu Changu kutoka kaseti za Sosaiti, huku wasikilizaji wakifuata kwa kitabu chao.
Dak 15: Fanyeni Mambo Pamoja Mkiwa Familia. Baba aongea na familia yake vivi hivi kuhusu uhitaji wa kuwa pamoja, ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1993, kurasa 16-19. Kazia funzo la familia na kazi ya evanjeli. Onyesha jinsi familia za kisasa zinavyovunjika kwa sababu ya kutumia wakati mchache pamoja na kutokuwa na mapendezi yanayofanana. Kujifunza Neno la Mungu na kushiriki katika huduma pamoja ni baraka kwa familia ya Kikristo. Kazia uhitaji wa baba kupanga mambo haya vizuri na mama kuunga mkono. Watoto wapaswa kupendezwa na utendaji wa kiroho, kufanya kazi kwa ukaribu na wazazi. Familia itaunganishwa na itaimarishwa ili ikabiliane na misongo inayoongezeka kuelekea ulimwengu.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 18
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia wapaswa kuwatia moyo wapya ambao wanafanya maendeleo vizuri katika funzo lao la Biblia kufikia kuwa watangazaji wasiobatizwa. Wazazi pia wanaweza kusaidia watoto wao wawe watangazaji. Pitia utaratibu uliopendekezwa kwenye kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 97-100.
Dak 15: “Msifuni Mungu Katika Patakatifu Pake.” Hotuba itolewe na mzee ambaye ni mshiriki wa halmashauri ya udumishaji wa Jumba la Ufalme. Shughulikia yale yapaswayo kufanywa kwenu ili kutengeneza na kudumisha hali ya Jumba la Ufalme. Wazee wapaswa kuhakikisha wameweka katika agenda ya mkutano wao utakaofuata hali na udumishaji wa Jumba la Ufalme.
Dak 20: “Rudia Wale Walioonyesha Kupendezwa.” Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa, na uwe na maonyesho mawili mafupi. Tia moyo wote wafanye ziara za kurudia wakiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo katika kitabu Ujuzi.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 25
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Pitia “Vikumbusha vya Ukumbusho.” Eleza kwa nini ni jambo la maana kuhudhuria. (Ona Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1985, kurasa 16-18.) Pitia mipango ya kusaidia wazee-wazee, wagonjwa, na wapya watakaokuwepo. Zungumza juu ya mipango ya ziada ya utendaji wa utumishi juma hili linalokuja. Pia, pitia makala, “Mahali Wageni Huonyeshwa Ukaribishaji,” kwenye ukurasa wa 32 wa toleo la Amkeni! la Septemba 22, 1995.
Dak 15: Kupangia Siku ya Pekee ya Magazeti ya Mwezi wa Aprili. Mwangalizi wa utumishi apaswa kuandaa mambo hususa kwa utendaji wa siku ya pekee ya magazeti iliyopangwa kuwa Jumamosi, Aprili 6, 1996. Pangia mikutano yote ya utumishi wa shambani kwa siku yote. Onyesha eneo kwa ajili ya ushahidi wa barabarani na sokoni pamoja na huduma ya kawaida ya magazeti nyumba kwa nyumba. Tia moyo wote watumie magazeti ya kutaniko kutia ndani matoleo ya zamani.
Dak 15: “Utayarishaji—Ufunguo wa Mafanikio.” Maswali na majibu. Taja kwamba tutakuwa tukitoa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! miezi ya Aprili na Mei. Fanya matayarisho sasa kwa kuagiza nakala za ziada, karatasi za maandikisho, na kupanga kuunga mkono mipango ya kutaniko ya utendaji wa Siku ya Magazeti.
Wimbo 7 na sala ya kumalizia.