Mafunzo Juu ya Maandiko Yenye Pumzi ya Mungu na Habari ya Msingi Yayo
Funzo Namba 7—Biblia Katika Nyakati za Ki-Siku-Hizi
Historia ya sosaiti za Biblia; kazi ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi katika kuchapa na kutangaza Biblia; kufanyizwa kwa New World Translation.
1. (a) Mawasiliano ya kimungu yalitolewa kwa makusudi gani, na kwa hiyo kwa nini mengine hayakuandikwa? (b) Ni maagizo gani ya moja kwa moja ambayo Yehova aliwapa wengi wa manabii, na yakiwa na mafaa gani kwetu sisi katika “siku za mwisho”?
MAANDIKO Matakatifu, vile vitabu 66 vilivyopuliziwa na Mungu tuvijuavyo leo kuwa Biblia, vina ‘neno la Yehova’ lililoandikwa. (Isa. 66:5) Kwa karne nyingi “neno” hilo lilitiririka bila kizuizi kutoka kwa Yehova mpaka kwa manabii na watumishi wake duniani. Mawasiliano hayo ya kimungu yalitimiza kusudi layo la wakati huo na pia yalitoa miono-kimbele yenye nguvu ya matukio ambayo yalikuwa ni hakika yatukie wakati ujao ulio mbali. Sikuzote haikupasa manabii wa Mungu waandike ‘neno la Yehova’ walilopokezwa. Kwa kielelezo, baadhi ya semi za Eliya na Elisha zilizotolewa kwa ajili ya kizazi cha wakati wao huenda ikawa hazikuhifadhiwa kwa kuandikwa. Kwa upande mwingine, manabii Musa, Isaya, Yeremia, Habakuki, na wengine walipokea maagizo ya moja kwa moja ‘waandike’ au ‘waandike katika kitabu au chuo’ ‘neno la Yehova’ walilofunuliwa. (Kut. 17:14; Isa. 30:8; Yer. 30:2; Hab. 2:2; Ufu. 1:11) “Maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu” yalihifadhiwa kwa njia hiyo, pamoja na miandiko mitakatifu mingine, ili kuamsha uwezo wa kufikiri waziwazi wa watumishi wa Yehova na hasa ili kutoa mwongozo kuhusu “siku za mwisho.”—2 Pet. 3:1-3.
2. Ni vipindi gani katika historia vimetambulika kwa utendaji ulioongezeka katika kunakili na kutafsiri Biblia?
2 Kunakili kwingi kwa Maandiko ya Kiebrania yaliyopuliziwa na Mungu kulifanywa kuanzia wakati wa Ezra na kuendelea. Kuanzia na karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu, Biblia ilinakiliwa na kunakiliwa tena na Wakristo wa mapema na ilitumiwa katika kutoa ushahidi kuhusu makusudi ya Yehova kuhusiana na Kristo Wake katika marefu na mapana yote ya ulimwengu uliojulikana wakati huo. Wakati uchapaji wa kutumia mashine ulipokuwa wa kawaida (kuanzia karne ya 15 na kuendelea), mchocheo zaidi ulitiwa katika kuzidisha na kutawanya nakala za Biblia. Utafsiri mwingi na pia uchapaji ulifanywa na vikundi vya kibinafsi katika karne ya 16 na ya 17. Mapema katika 1800, Biblia nzima-nzima au ikiwa sehemu-sehemu ilikuwa imetokea katika lugha 71.
SOSAITI ZA BIBLIA
3. Ni jambo gani limechangia sana ongezeko katika utawanyaji wa Biblia tangu mwanzo wa karne ya 19?
3 Mwendo uliongezwa katika kazi hiyo katika karne ya 19 na ya 20, wakati sosaiti za Biblia zilizokuwa zimetoka kuundwa zilianza kushiriki katika kazi kubwa sana ya kutawanya Biblia. Mojawapo ya sosaiti za Biblia za mapema zaidi ilikuwa Sosaiti ya Biblia ya Uingereza na Nchi za Nje, ambayo ilifanywa tengenezo katika London katika 1804. Kufanywa tengenezo kwa sosaiti ya Biblia hiyo kulitokeza kusimamishwa kwa sosaiti nyinginezo nyingi zaidi.a
4. (a) Ni takwimu gani zinazotoa uthibitisho kwamba neno la uhai limeenea dunia yote? (b) Ni habari gani yenye msaada imetolewa katika chati katika ukurasa 322 juu ya tafsiri tofauti-tofauti za Biblia zilizoorodheshwa? Toa kielezi cha hilo kwa kurejezea tafsiri ya Biblia fulani hasa.
4 Kwa kuwapo sosaiti za Biblia nyingi hivyo zenye kutenda kazi, kazi ya kueneza Biblia ilisitawi sana. Kufikia mwaka 1900, Biblia nzima-nzima au ikiwa sehemu-sehemu ilikuwa imetokea katika lugha 567, na kufikia 1928, katika lugha 856. Kufikia 1938 alama ya elfu moja ilipitwa, na sasa Biblia yapatikana katika lugha zaidi ya 1,900. Neno la uhai lenye kuburudisha la Yehova limeenea dunia pote! Kwa hiyo, imewezekana kwa wanadamu wa mataifa yote kujibu mwito huu: “Sifuni Yehova, nyinyi nyote mataifa, na acheni vikundi vyote vya watu visifu yeye.” (Rum. 15:11, NW) Chati katika ukurasa 322, “Baadhi ya Tafsiri za Biblia Zenye Kuongoza Katika Lugha Saba Kubwa,” yatoa habari zaidi juu ya utawanyaji wa ki-siku-hizi wa Biblia.
5. Ni nini kilicho cha maana hata zaidi kuliko utawanyaji wa Biblia, hata hivyo Mashahidi wa Yehova wanashukuru kwa ajili ya nini?
5 Ingawa kuwezesha Biblia ipatikane kwa umati wa dunia ni kazi ya kupongezeka, kutumia Biblia hizo ili kufanya watu waelewe Biblia ni kazi iliyo ya maana hata zaidi. Kufanya neno hilo ‘lieleweke’ ndilo lililokuwa jambo la maana katika nyakati za Kiyahudi na za mapema za Ukristo, wakati ambapo Biblia chache zilipatikana, na bado hilo ndilo jambo la maana zaidi kufanya. (Mt. 13:23; Neh. 8:8) Hata hivyo, kazi hiyo ya kufundisha vikundi vya watu wa dunia yote Neno la Mungu imeharakishwa na utawanyaji mkubwa wa Biblia. Mashahidi wa Yehova leo wanapokaza mwendo mbele kwa kazi yao ya elimu ya Biblia yenye kuzunguka tufe lote, wanashukuru kwamba mamilioni ya Biblia yanapatikana sasa katika mabara na lugha nyingi.
MASHAHIDI WA YEHOVA WAKIWA WATANGAZAJI WA BIBLIA
6. Mashahidi wa Yehova wametambulishwa na utendaji gani leo na pia katika nyakati za kale?
6 Mashahidi wa Yehova ni watu wenye kutangaza Biblia. Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Ezra. Ndivyo ilivyokuwa katika siku za wanafunzi wa mapema wa Yesu Kristo, ambao waliujaza ulimwengu wa kale kwa nakala zao za Biblia zilizoandikwa kwa mkono kwa kadiri kubwa hivi kwamba urithi mkubwa tuliopokea wa miandiko yao ya hati unazidi ule wa fasihi nyinginezo zote za kale. Sasa, katika nyakati hizi za ki-siku-hizi, utendaji uo huo wenye nguvu wa kutangaza Biblia ni kitambulisho cha Mashahidi wa Yehova.
7. Mashahidi wa Yehova waliunda shirika gani? wakati gani? na ni jinsi gani walianza kusitawisha huduma yao wakati huo?
7 Katika 1884, Mashahidi wa Yehova waliunda shirika la kuendesha kazi yao ya kutangaza Biblia, shirika hilo sasa lajulikana kuwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Hapo kwanza Biblia zilinunuliwa kutoka kwa sosaiti nyingine za Biblia ili zitawanywe tena na Mashahidi hao, ambao hata wakati huo walikuwa wakisitawisha kile kitambulisho chao cha huduma ya nyumba kwa nyumba. King James Version ya 1611 katika Kiingereza ilitumiwa kama tafsiri yao ya msingi kwa ajili ya funzo la Biblia.
8. (a) Watch Tower Bible and Tract Society imetendaje kulingana na jina layo? (b) Sosaiti imetumiaje tafsiri nyingi za Biblia, na kwa kusudi gani?
8 Kwa kutenda kulingana na jina layo, Watch Tower Bible and Tract Society imeshiriki katika kutawanya Biblia, na pia kutangaza vitabu, trakti, na fasihi nyingine za Kikristo. Hilo limekuwa kwa kusudi la kuagiza katika mafundisho sahihi ya Neno la Mungu. Elimu layo ya Biblia imesaidia wapenda uadilifu wajiondoe kutoka mapokeo ya dini bandia na falsafa ya kilimwengu na kurejea kwenye uhuru wa kweli ya Biblia kama ulivyofunuliwa kupitia Yesu na wanenaji wengine wa Yehova waliojitoa. (Yn. 8:31, 32) Tangu wakati ambao gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) lilipoanza kutangazwa katika 1879, vichapo vya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi vimenukuu, kutaja, na kurejezea tafsiri nyingi tofauti za Biblia. Hivyo, Sosaiti imetambua thamani yazo zote na imetumia vizuri zote hizo kuwa zenye thamani katika kuondosha vurugu la kidini na kutokeza ujumbe wa Mungu.
9. Sosaiti iliingiaje katika uwanja wa kutangaza Biblia?
9 Biblia za Rotherham na Holman. Katika 1896 Mashahidi wa Yehova, kupitia Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, waliingia kwenye uwanja wa kuwa watangazaji na watawanyaji wa Biblia. Katika mwaka huo haki za kuchapa zilipatikana kutoka kwa mtafsiri wa Biblia Mwingereza Joseph B. Rotherham za kutangaza katika United States hariri yake ya kumi na mbili iliyosahihishwa ya New Testament. Kwenye ukurasa wenye kichwa wa nakala hizo zilizochapwa, kulikuwako jina la Watch Tower Bible and Tract Society, Allegheny, Pennsylvania, makao makuu ya Sosaiti yakiwa huko wakati huo. Katika 1901 mipango ilifanywa ya uchapaji wa kipekee wa Holman Linear Bible, yenye maandishi ya maelezo ya pambizoni kutoka vichapo vya Sosaiti vya 1895 mpaka 1901. Maandishi-awali yenyewe ya Biblia yalikuwa ya King James Version na Revised Version ya Maandiko ya Kiebrania na Kigiriki. Hariri yote hiyo ya nakala 5,000 ilikuwa imekwisha tawanywa kufikia mwaka 1903.
10. Sosaiti ilikuja kuwa watangazaji wa tafsiri gani ya Maandiko ya Kigiriki katika 1902?
10 The Emphatic Diaglott. Katika 1902 Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ilikuja kuwa wenyeji wenye haki ya kunakili, watangazaji na watawanyaji pekee wa The Emphatic Diaglott. Tafsiri hiyo ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitayarishwa na mtafsiri aliyezaliwa Uingereza Benjamin Wilson, wa Geneva, Illinois. Ilikamilishwa katika 1864. Ilitumia maandishi-awali ya Kigiriki ya J. J. Griesbach, pamoja na tafsiri halisi ya mistari ya kati ya mistari ya Kiingereza na tafsiri ya Wilson mwenyewe kwenye upande wa kulia ikitumia ishara zake za pekee za kutia mkazo.
11. Ni wakati gani Sosaiti ilipochapisha “Hariri ya Wanafunzi wa Biblia,” na ndani yayo mlikuwa nini?
11 Hariri ya Wanafunzi wa Biblia. Katika 1907 Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ilitangaza Biblia ya “Hariri ya Wanafunzi wa Biblia.” Buku hilo lilikuwa na uchapaji ulio wazi wa Tafsiri ya King James ya Biblia na ilitia ndani maandishi mazuri sana pambizoni, pamoja na nyongeza yenye kusaidia sana iliyofanyizwa na Mashahidi wa Yehova. Nyongeza hiyo, ambayo baadaye ilikuja kupanuliwa kuwa kurasa zaidi ya 550, iliitwa “Kitabu cha Walimu wa Biblia Waberoya pia ilichapishwa ikiwa kitabu kilicho peke yacho. Ilikuwa na maelezo mafupi juu ya mistari mingi ya Biblia, ikiwa na marejezo kwenye Mnara wa Mlinzi na kwenye vitabu vya mafundisho vya Sosaiti, na muhtasari wa vichwa vya mafundisho pamoja na maandiko makuu ili kurahisisha mahubiri yao kwa wengine. Hiyo ilifanana na kichapo cha baadaye cha Sosaiti “Make Sure of All Things.” Pia ndani kulitiwa faharisi ya vichwa, maelezo ya maandishi-awali magumu, orodha ya vifungu vya maandiko yaliyochafuliwa, faharisi ya Andiko, kronolojia ya kulinganisha, na ramani 12. Biblia hiyo bora sana ilitumikia Mashahidi wa Yehova kwa makumi mengi ya miaka katika kazi yao ya kuhubiri peupe.
SOSAITI YA KUCHAPA BIBLIA
12. Ni wakati gani Sosaiti ilipoingia katika uwanja wa uchapaji wa Biblia?
12 Kwa miaka 30 Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ilihusisha makampuni ya nje kufanya uchapaji halisi wa Biblia zayo. Hata hivyo, katika Desemba 1926, The Emphatic Diaglott ikawa tafsiri ya kwanza ya Biblia kuchapwa kwenye matbaa za Sosaiti yenyewe kule Brooklyn, New York. Uchapaji wa hariri hiyo ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ulichochea tumaini kwamba Biblia kamili ingechapwa katika matbaa za Sosaiti siku fulani.
13. (a) Biblia ya kwanza kamili kuchapwa na Sosaiti ilikuwa ipi, nayo ilitolewa kwa mara ya kwanza wakati gani? (b) Ilikuwa na misaada gani?
13 King James Version. Vita ya Ulimwengu 2 ilikazia uhitaji wa utangazaji wa kujitegemea wa Biblia yenyewe. Pambano hilo la tufe lote lilipokuwa limechacha kabisa, Sosaiti ilifaulu kununua mabamba ya kuchapia ya Tafsiri kamili ya Biblia ya King James. Ilikuwa mnamo Septemba 18, 1942, katika Ulimwengu Mpya Kusanyiko la Kitheokrasi la Mashahidi wa Yehova, kituo kikuu cha kusanyiko kikiwa kule Cleveland, Ohio, kwamba msimamizi wa Sosaiti akanena juu ya habari, “Kutokeza ‘Upanga wa Roho.’” Ukiwa upeo wa mhadhara huu, yeye alitoa kwa mara ya kwanza Biblia kamili ya kwanza iliyochapwa katika kiwanda cha Brooklyn cha Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi. Katika nyongeza yayo ilitoa orodha ya majina na maana yayo, “Konkodansi ya Maneno na Semi za Biblia” iliyotayarishwa kipekee na misaada mingine. Kichwa cha kufaa kilitolewa katika sehemu ya juu ya kila ukurasa. Kwa kielelezo, “Nadhiri yenye bidii ya Yeftha” kilichukua mahali pa “Nadhiri yenye harara ya Yeftha” kwenye Waamuzi 11, na “Kuwapo kwa kabla ya kuwa binadamu na uzawa wa kibinadamu wa Neno la Mungu” kilitokea kwenye Yohana sura 1.
14. Ni tafsiri gani ya Biblia iliyofanyiwa maendeleo ambayo ilichapwa na Sosaiti katika 1944, nayo Biblia hiyo ina sehemu zipi?
14 American Standard Version. Tafsiri nyingine ya Biblia yenye maana ni American Standarad Version ya 1901. Ina sehemu yenye kupongezwa zaidi ya kutafsiri jina la Mungu kuwa “Yehova” karibu mara 7,000 katika Maandiko ya Kiebrania. Baada ya majadiliano marefu, Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi iliweza kununua, katika 1944, matumizi ya mabamba ya kuchapia ya Biblia ya American Standard Version yote ipate kuichapa katika matbaa zayo yenyewe. Mnamo Agosti 10, 1944, kule Buffalo, New York, jiji kuu la makusanyiko 17 yenye kuendelea wakati mmoja ya Mashahidi wa Yehova yaliyounganishwa pamoja kwa waya za simu za kibinafsi, msimamizi wa Sosaiti alipendeza sana wasikilizaji wake wengi kwa kutoa kwa mara ya kwanza hariri ya Watch Tower ya American Standard Version. Nyongeza yatia ndani “Konkodansi ya Maneno, Majina, na Semi za Biblia” iliyo msaada mkubwa sana na iliyopanuliwa. Hariri ya mfukoni ya Biblia iyo hiyo ilitangazwa katika 1958.
15. Ni tafsiri gani iliyotokezwa na Sosaiti katika 1972?
15 The Bible in Living English. Katika 1972 Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ilitokeza The Bible in Living English, ya hayati Steven T. Byington. Hiyo hutafsiri kwa upatani jina la kimungu kuwa “Yehova.”
16. Kwa hiyo Mashahidi wa Yehova wanashiriki kazi gani maradufu?
16 Kwa hiyo, si kwamba tu Mashahidi wa Yehova wanahubiri habari njema za Ufalme wa Mungu uliosimamishwa katika nchi na visiwa zaidi ya 200 katika dunia yote bali pia wamekuja kuwa wachapaji na watangazaji, kwa kiwango kikubwa, wa kile Kitabu kisichokadirika bei chenye ujumbe wa Ufalme, Maandiko Matakatifu yaliyopuliziwa na Yehova Mungu.
NEW WORLD TRANSLATION OF THE HOLY SCRIPTURES
17. (a) Tafsiri hizo nyingi zimekuwaje zenye mafaa, hata hivyo zina kasoro gani? (b) Tangu 1946, msimamizi wa Sosaiti alikuwa amekuwa akitafuta nini?
17 Mashahidi wa Yehova hukiri tegemeo lao juu ya tafsiri zote nyingi za Biblia ambazo wamezitumia katika kujifunza ukweli wa Neno la Mungu. Hata hivyo, tafsiri zote hizo, hata ile iliyo ya karibuni zaidi, zina kasoro zazo. Kuna kutopatana au matumizi ya maneno yasiyoridhisha, ambayo yana dosari ya mapokeo ya kidhehebu au falsafa za kilimwengu na kwa hiyo hazipatani kabisa na kweli takatifu ambazo Yehova amefanya ziandikwe katika Neno lake. Hasa tangu 1946, msimamizi wa Watch Tower Bible and Tract Society alikuwa akitafuta kwa bidii tafsiri ya lugha za awali yenye uaminifu—tafsiri yenye kueleweka kwa wasomaji wa ki-siku-hizi kama ambavyo maandishi ya awali yalivyokuwa yenye kueleweka kwa makabwela wenye kutumia akili, wa kipindi cha uandishi wa Biblia yenyewe.
18. Sosaiti ilikujaje kuwa watangazaji na wachapaji wa New World Translation?
18 Mnamo Septemba 3, 1949, katika makao makuu ya Sosaiti, Brooklyn, msimamizi alitangazia Baraza la Wakurugenzi kuwapo kwa Halmashauri ya Tafsiri ya Biblia ya New World na kwamba ilikuwa imekamilisha tafsiri ya ki-siku-hizi ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Hati ya halmashauri hiyo ilisomwa, ambayo kwayo halmashauri hiyo iliipa Sosaiti umiliki, usimamizi, na utangazaji wa hati ya tafsiri, kwa kutambua kazi ya Sosaiti isiyo ya farakano ya kusogeza mbele elimu ya Biblia duniani kote. Visehemu vya hati hiyo vilisomwa pia, kuwa vielelezo vya asili na ubora wa tafsiri hiyo. Wakurugenzi hao kwa kauli moja walikubali zawadi ya tafsiri hiyo, na mipango ikafanywa ya kuichapa mara moja. Upangaji chapa ulianza mnamo Septemba 29, 1949, na kufikia mapema kiangazi cha 1950, makumi ya maelfu ya nakala yalikamilishwa yakiwa yamefungwa kwenye jalada.
19. (a) New World Translation ilitokeaje katika sehemu zayo? (b) Ni jitihada gani iliyokuwa imefanywa katika kutayarisha mabuku hayo?
19 Kutoa kwa mara ya kwanza New World Translation Katika Visehemu Vyayo. Ilikuwa mnamo Jumatano, Agosti 2, 1950, siku ya nne ya kusanyiko la kimataifa kule Yankee Stadium, New York, kwamba wasikilizaji 82,075 wa Mashahidi wa Yehova wenye mshangao kamili walikubali kwa moyo utoaji wa kwanza wa New World Translation of the Christian Greek Scriptures. Kwa kutiwa moyo na karibisho lenye idili la hapo kwanza, na pia semi za baadaye zenye uthamini kuhusu mafaa ya tafsiri hiyo, Halmashauri hiyo ilianza kazi kubwa ya kutafsiri Maandiko ya Kiebrania. Hiyo ilitokea katika mabuku matano ya ziada, yaliyotolewa kwa mara ya kwanza yakifuatana kuanzia 1953 mpaka 1960. Jumla hiyo ya mabuku sita ilifanyiza maktaba ya Biblia yote katika Kiingereza cha ki-siku-hizi. Kila buku pia lilikuwa na misaada yenye thamani ya funzo la Biblia. Akiba kubwa ya habari za Kimaandiko ilitolewa kwa mwanafunzi wa Biblia wa ki-siku-hizi kwa njia hiyo. Jitihada yenye bidii ilikuwa imefanywa ili kutumia kila chanzo chenye kutegemeka cha habari za maandishi-awali ili New World Translation iweze kueleza kwa uwazi na kwa usahihi ujumbe wenye nguvu wa Maandiko ya awali yaliyopuliziwa na Mungu.
20. Hariri ya kwanza ya New World Translation ilikuwa na misaada gani yenye thamani katika (a) vielezi-chini, (b) marejezo ya pambizoni, na (c) dibaji na nyongeza?
20 Miongoni mwa misaada ya funzo la Biblia katika hariri ya kwanza yenye sehemu sita ya New World Translation ulikuwa mkusanyo wenye thamani kubwa wa vielezi-chini vya maandishi-awali, vyenye kueleza chanzo cha matumizi ya maneno hayo. Katika maandishi hayo hoja zenye nguvu za kutetea Maandiko zilitolewa. Mfumo wenye thamani wa mfululizo wa marejezo ulitiwa ndani pia. Mifululizo hiyo ya maneno yenye maana ya kimafundisho ilikusudiwa kuelekeza mwanafunzi kwenye mfuatano wa maandishi-awali makuu juu ya habari hizo. Kulikuwako marejezo ya kutoka sehemu mbalimbali katika mapambizo ya kurasa. Hayo yalielekeza msomaji kwenye (a) maneno yanayofanana, (b) mafikira, mawazo, na matukio yenye kufanana, (c) habari ya kiwasifu, (d) habari ya kijiografia, (e) utimizo mbalimbali wa unabii mbalimbali, na (f) manukuu ya moja kwa moja katika au kutoka sehemu nyingine za Biblia. Katika mabuku hayo kulikuwako pia dibaji zenye maana, vielezi vya baadhi ya hati za kale, nyongeza na faharisi zenye msaada, na ramani za mabara na vituo vya Biblia. Hariri hiyo ya kwanza ya New World Translation ilitoa hazina kubwa ya funzo la Biblia la kibinafsi na kwa ajili ya Mashahidi wa Yehova kufundisha kwa mafaa watu wenye mioyo ya ufuatiaji haki. Hariri ya pekee ya wanafunzi, iliyotangazwa katika buku moja katika uchapaji wa nakala 150,000, ilitolewa kwa mara ya kwanza Juni 30, 1963, wakati wa kufungua “Habari Njema za Milele” Kusanyiko la Mashahidi wa Yehova kule Milwaukee, Wisconsin, U.S.A.
21. (a) Hali za kutolewa kwa mara ya kwanza kwa New World Translation iliyosahihishwa zilikuwa nini? (b) Ni zipi zilizokuwa baadhi ya sehemu zayo?
21 Hariri Iliyosahihishwa ya Buku Moja. Katika kiangazi cha 1961, kwenye mfuatano wa makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova yaliyofanyiwa United States na Ulaya, hariri iliyosahihishwa ya New World Translation of the Holy Scriptures kamili ikiwa buku moja lenye kuchukulika ilitolewa kwa mara ya kwanza kwa ajili ya utawanyaji. Ilikubaliwa kwa shangwe na mamia ya maelfu waliohudhuria makusanyiko hayo. Ikiwa imetiwa kwenye jalada la kitambaa cha kijani-kibichi, ilikuwa na kurasa 1,472 na konkodansi nzuri sana, nyongeza juu ya vichwa vya Biblia, na ramani.
22, 23. Ni hariri gani zaidi zimekuja kutolewa kwa mara ya kwanza, na baadhi ya sehemu zazo ni zipi?
22 Hariri Zaidi. Katika 1969 The Kingdom Interlinear Translation of the Greek Scriptures ilitolewa kwa mara ya kwanza, na hariri ya pili ikatolewa katika 1985. Buku hilo linatoa tafsiri ya halisi ya Kiingereza ya maandishi-awali ya Kigiriki yaliyohaririwa na Westcott na Hort na pia tafsiri ya Kiingereza cha ki-siku-hizi cha hariri ya 1984 ya New World Translation. Kwa njia hiyo inafungulia mwanafunzi wa Biblia mwenye kuchukua kwa uzito yale ambayo Kigiriki cha awali husema kwa msingi au kwa halisi.
23 Hariri ya pili iliyosahihishwa ya New World Translation ilitolewa kwa mara ya kwanza katika 1970, na hariri ya tatu iliyosahihishwa yenye vielezi-chini ilifuata katika 1971. Kwenye “Ongezeko la Ufalme” Mikusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova, iliyofanywa katika 1984, hariri ya mrejezo iliyosahihishwa ilitolewa katika Kiingereza. Hilo latia ndani kufanywa kikamili kuwa ya kisasa na kusahihisha marejezo (ya kutoka sehemu mbalimbali zilizomo) ya pambizoni ambayo hapo kwanza yalikuwa yametolewa katika Kiingereza kuanzia 1950 mpaka 1960. Ikiwa imekusudiwa kwa mwanafunzi wa Biblia anayechukua mambo kwa uzito, ina marejezo ya pambizoni zaidi ya 125,000, vielezi-chini zaidi ya 11,000, na konkodansi yenye mambo mengi, ramani, na makala 43 za nyongeza. Pia katika 1984, hariri ya ukubwa wa kawaida ya sahihisho la 1984, yenye marejezo ya pambizoni lakini bila ya vielezi-chini, ilitolewa.
24. (a) Ni nini baadhi ya faida za hariri ya kawaida na ya marejezo? (b) Toa kielezi cha matumizi ya vichwa vya kila ukurasa.
24 Baadhi ya Faida. Ili kusaidia msomaji apate kwa upesi habari yoyote inayotakwa, hariri ya kawaida na ya mrejezo zina kichwa kila ukurasa kilichofanyizwa kwa uangalifu juu ya kila ukurasa. Vichwa hivyo vya kila ukurasa hueleza habari iliyo chini, navyo vimepangwa hasa ili kusaidia mhubiri wa Ufalme apate kwa upesi maandishi katika kujibu maswali anayoweza kuulizwa. Kwa kielelezo, huenda akawa anajaribu kupata shauri juu ya kuzoeza watoto. Akija kwenye ukurasa 860 (hariri ya kawaida) katika Mithali, anaona kifungu cha mwisho cha msingi, “A good name” (Jina jema). Kwa kuwa hicho ndicho kifungu cha mwisho cha kichwa, chaonyesha kwamba habari hiyo itaonekana baadaye kwenye ukurasa huo, na hapo ndipo atakapoipata, kwenye Mithali 22:1. Andiko linalotambulishwa na sehemu ya kwanza ya kichwa cha ukurasa huo katika ukurasa 861, “Train up a boy” (Zoeza mvulana), analiona mapema kwenye ukurasa huo, kwenye mstari 6. Sehemu ile nyingine ya kichwa yasomwa hivi, “Not spare the rod” (Kutoacha fimbo). Habari hiyo iko karibu na chini ya safu ya kwanza, katika mstari 15. Vichwa hivyo vya kila ukurasa vyaweza kuwa msaada mkubwa kwa mhubiri wa Ufalme anayejua kwa ujumla ni wapi maandishi anayotafuta yalipo. Vyawezesha kufungua Biblia kwa upesi.
25. Ni utumishi gani wa konkodansi umetayarishwa, nao waweza kutumiwa kwa kazi gani?
25 Mwishoni mwa hariri ya kawaida na ya mrejezo ya Biblia hii, kuna sehemu inayoitwa “Bible Words Indexed” (Maneno ya Biblia Yafaharisiwa). Hapo panapatikana maelfu ya maneno yenye maana ya Biblia pamoja na mistari ya muktadha. Hivyo utumishi wa konkodansi watolewa, kutia ndani maneno mengi mapya, yenye kusimulia yanayotumiwa katika maandishi-awali hayo. Kwa wale waliozoea tafsiri za maneno ya King James Version, msaada umetolewa kwa kuonyesha mabadiliko mengi ya maneno ya kale zaidi ya Biblia mpaka kwa semi za ki-siku-hizi zaidi za Biblia. Chukua kwa kielelezo, neno “grace” (neema) katika King James Version. Hilo limeorodheshwa katika faharisi, likirejezea mwanafunzi kwa “undeserved kindness” (fadhili zisizostahilika), uneni wa kisasa unaotumiwa katika tafsiri hiyo mpya. Faharisi ya maneno yawezesha kupata maandishi ya Andiko juu ya habari za msingi za kimafundisho, kama vile “nafsi” au “ukombozi,” yanayounga mkono funzo la kirefu la moja kwa moja kutoka kwa miandiko ya Biblia. Mhubiri wa Ufalme anayetakwa ahubiri juu ya yoyote ya habari hizo angeweza bila kukawia kutumia visehemu vifupi vya muktadha vilivyoonyeshwa katika konkodansi hiyo. Kuongezea hayo, mitajo mikubwa imeorodheshwa kwa majina yenye kutokeza, kutia ndani sehemu za kijiografia na pia watu maarufu wa Biblia. Msaada mkubwa sana umetolewa kwa njia hiyo kwa wanafunzi wa Biblia wote wanaotumia tafsiri hii.
26. Toa kielezi cha moja ya njia ambazo nyongeza ya New World Translation ni msaada.
26 Nyongeza ya kiusomi yatoa habari zaidi sahihi yenye mafaa kwa kufundisha. Makala za nyongeza zimepangwa kwa njia ambayo zaweza kutumiwa kuwa msaada katika kueleza mafundisho ya msingi ya Biblia na mambo yanayohusiana. Kwa kielelezo, katika kushughulika na habari “nafsi,” nyongeza, chini ya vichwa vinane tofauti-tofauti, yaorodhesha maandishi ya andiko yanayoonyesha njia mbalimbali ambazo katika hizo neno “nafsi” (Kiebrania, neʹphesh) hutumiwa. Michoro na ramani imetolewa pia katika makala za nyongeza. Reference Bible ina nyongeza yenye mambo mengi zaidi na pia vielezi-chini vinavyosaidia ambavyo vina habari ya maana ya maandishi-awali iliyo rahisi kueleweka. Hivyo, New World Translation ni yenye kutokeza kwa ajili ya utumishi mwingi ambao inatoa wa kuwapa kwa upesi wasomaji wayo maarifa sahihi.
27, 28. Eleza na kutoa kielezi cha jinsi New World Translation huonyesha matamshi ya majina.
27 Msaada Katika Kutamka Majina ya Biblia. Katika maandishi-awali ya Kiingereza yenyewe, hariri zote za New World Translation hutoa msaada katika matamshi ya majina. Mfumo huo wafanana na ule uliobuniwa na mtaalamu mmoja kwa ajili ya Revised Standard Version ya 1952. Jina limegawanywa kwa silabi zinazotenganishwa kwa nukta au kwa alama ya lafudhi (ʹ). Alama hiyo ya lafudhi hufuata silabi ambayo mkazo mkubwa wapasa kuwekwa katika kutamka neno hilo. Endapo silabi iliyo na lafudhi yamalizika na irabu, basi irabu hiyo yavutwa katika kutamkwa. Endapo silabi yamalizikia na konsonanti, basi irabu katika silabi hiyo ni fupi katika kutamkwa.
28 Kama kielelezo, angalia Ayubu 4:1, NW (Kiingereza). Hapa pasema juu ya “Elʹi·phaz the Teʹman·ite.” Ingawa katika visa vyote viwili lafudhi iko penye silabi ya kwanza, herufi “e” yapasa kutamkwa tofauti katika visa hivyo viwili. Katika “Elʹi·phaz” alama ya lafudhi iliyopo baada ya konsonanti “l” yafanya irabu “e” kuwa fupi, kama vile katika “enzi.” Na hali, katika “Teʹman·ite” kuwa kwa lafudhi moja kwa moja baada ya irabu “e” kwaifanya kuwa “i”, kama vile katika “ibada.” Wakati irabu hizi mbili “a” na “i” zinapounganishwa, kama katika “Morʹde·cai” katika Esta 2:5, NW, na “Siʹnai” katika Kutoka 19:1, NW, “ai” hutamkwa “ae” kama vile katika “babae.”
29. Je! New World Translation ni sahihisho tu la tafsiri za hapo mapema, na ni sehemu gani zinazounga mkono jibu lako?
29 Tafsiri Mpya. New World Translation ni tafsiri mpya kutoka lugha za awali za Biblia za Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Kwa vyovyote hiyo si sahihisho la tafsiri nyingineyo yoyote ya Kiingereza, wala hainakili tafsiri nyingineyo yoyote kwa habari ya mtindo, msamiati, wala mpangilio wa maneno. Kwa ajili ya kisehemu cha Kiebrania-Kiaramu, maandishi-awali yaliyochujwa vizuri na kukubaliwa kila mahali ya Biblia Hebraica ya Rudolf Kittel, hariri ya 7, ya 8, na ya 9 (1951-55), yalitumiwa. Chapa mpya ya maandishi-awali ya Kiebrania yajulikanayo kuwa Biblia Hebraica Stuttgartensia, yenye tarehe ya 1977, ilitumiwa kwa ajili ya kufanya habari iliyotolewa katika vielezi-chini vya New World Translation—With References kuwa ya kisasa. Ile sehemu ya Kigiriki ilitafsiriwa hasa kutokana na maandishi-awali ya Kigiriki yaliyosahihishwa na kutayarishwa na Westcott na Hort, yaliyotangazwa katika 1881. Hata hivyo, Halmashauri ya Tafsiri ya Biblia ya New World imeshauri pia maandishi-awali mengine ya Kigiriki, kutia ndani maandishi-awali ya Kigiriki ya Nestle (1948). Maelezo ya maandishi-awali hayo mazuri sana yaliyosahihishwa yametolewa katika Mafunzo 5 na 6 ya buku hili. Halmashauri ya tafsiri imefanya tafsiri ya kujikakamua na iliyo sahihi ya Biblia, na tokeo la hilo limekuwa maandishi-awali yaliyo wazi na yaliyo hai, yenye kufungua njia ya kuelewa Neno la Mungu kwa kina kirefu zaidi, kwa kuridhisha zaidi.
30. Ni nini kadirio la mchambuzi mmoja wa tafsiri hiyo?
30 Angalia kadirio la mchambuzi mmoja wa tafsiri hii: “Tafsiri za awali za Maandiko ya Kiebrania mpaka lugha ya Kiingereza ni chache sana. Kwa hiyo inatupa upendezi mwingi kukaribisha kichapo cha sehemu ya kwanza ya New World Translation [ya Maandiko ya Kiebrania], Mwanzo mpaka Ruthu. . . . Tafsiri hii kwa wazi imefanya jitihada ya pekee kuwe yenye kusomeka kabisa. Hakuna yeyote anayeweza kusema imepungukiwa katika upya na uasili. Matumizi ya maneno hayategemei kamwe tafsiri za awali.”b
31. Msomi mmoja wa Kiebrania alikadiriaje New World Translation?
31 Msomi wa Kiebrania Profesa Dakt. Benjamin Kedar wa Israeli, katika mahoji na mwakilishi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi alikadiria New World Translation kama ifuatavyo: “Katika utafiti wangu wa lugha kwa kukamatana na Biblia ya Kiebrania na tafsiri, mara nyingi mimi hurejezea hariri ya Kiingereza wa ile inayojulikana kuwa New World Translation. Katika kufanya hivyo, mimi huona hisia yangu ikithibitishwa tena na tena kwamba kazi hii yaonyesha jitihada yenye ufuatiaji-haki ili kufikia kuelewa maandishi-awali yaliyo sahihi kwa kadiri iwezekanayo. Ikitoa uthibitisho wa utaalamu mkubwa wa lugha ya awali, inatafsiri maneno ya awali katika lugha ya pili kwa njia yenye kueleweka bila ya kuondoka isivyo lazima kwenye muundo ule wa Kiebrania. . . . Kila taarifa ya lugha huruhusu nafasi fulani ya kufasiri au kutafsiri. Kwa hiyo suluhisho la kilugha katika chochote kile yaweza kujadiliwa. Lakini sijapata kamwe kugundua katika New World Translation nia yoyote yenye upendeleo ya kutia jambo katika maandishi-awali lisilokuwamo.”c
32. New World Translation ni halisi kwa kadiri gani, na hilo ni kwa mafaa gani?
32 Tafsiri ya Kihalisi. Uaminifu kuhusiana na kutafsiri waonyeshwa pia kwa uhalisi wayo. Hilo karibu lataka ulingani wa neno kwa neno kati ya matumizi ya maneno katika Kiingereza na maandishi-awali ya Kiebrania na Kigiriki. Katika kutokeza maandishi-awali katika lugha ambayo imetafsiriwa, kiwango cha uhalisi chapasa kuwa juu kwa kadiri nahau za lugha ya awali ziruhusuvyo. Zaidi ya hayo, uhalisi hutaka kwamba utaratibu wa maneno mengi yanayotumiwa uwe ule ule kama katika Kiebrania au Kigiriki, hivyo kuhifadhi mkazo wa miandiko ya awali. Kupitia tafsiri halisi, ladha, uzuri, na mpangilio wa maneno ya miandiko ya awali waweza kuwasilishwa kwa usahihi.
33. Kuondoka kwa kwa pindi kwa pindi kutoka maandishi-awali halisi kumeonyeshwaje?
33 Kumekuwako kuondoka kwa pindi kwa pindi kutoka maandishi-awali ya halisi, kwa kusudi la kuwasilisha kwa semi zenye kueleweka nahau ngumu za Kiebrania au Kigiriki. Hata hivyo, katika hariri ya mrejezo ya New World Translation, hizo zaonyeshwa msomaji kupitia vielezi-chini vinavyotoa tafsiri halisi.
34. (a) Matokeo ya kuondoka kwenye tafsiri halisi ni nini? (b) Toa kielezi.
34 Watafsiri wengi wa Biblia wameacha uhalisi kwa ajili ya kile wanachofikiria kuwa ni fahari ya lugha na umbo. Wanabisha kwamba tafsiri halisi hazina ladha, hazipendezi, na zina kizuizi. Hata hivyo, kuacha kwao tafsiri halisi, kupitia mihtasari na mafasirio, kumetokeza kuondoka kwingi kutoka taarifa sahihi za awali za ukweli. Kama ilivyo, kumetohoa mawazo yenyewe ya Mungu. Kwa kielelezo, mkuu wa kitovu cha chuo kikuu kimoja kikubwa cha Amerika aliyestaafu pindi moja alishtaki Mashahidi wa Yehova kwa kuharibu uzuri na fahari ya Biblia. Kwa usemi Biblia alimaanisha King James Version, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeheshimiwa mno kuwa kiwango cha Kiingereza cha kupendeza. Yeye alisema: ‘Aisee mmeifanyaje Zaburi 23. Mmeharibu mtiririko na upendezi wayo kwa “Je/ho/vah is/ my/ she/pherd” yenu. Silabi saba badala ya sita. Ni vibaya mno. Hakuna usawaziko. Hakuna mpangilio mzuri. King James imeiweka vizuri kwa silabi zayo sita zenye usawaziko—“The/ Lord/ is/ my/ shep/herd.”’ Pingamizi lilitolewa kwa profesa huyo kwamba lilikuwa jambo la maana zaidi kuitafsiri kwa njia ambayo Daudi, mwandikaji wa Biblia, aliisema. Je! Daudi alitumia neno la kawaida “Lord” (Bwana), au je! alitumia jina la kimungu? Profesa huyo alikubali kwamba Daudi alitumia jina la kimungu, lakini bado akabisha kwamba kwa ajili ya upendezi na fahari, neno “Lord” lingefaa. Hicho ni kisababu kisicho na msingi kama nini cha kuondoa jina lenye adhama la Yehova kutoka zaburi hii ya kumsifu!
35. Twaweza kumshukuru Mungu kwa ajili ya nini, na tumaini na sala yetu ni nini?
35 Maelfu ya tafsiri zimetoholewa kwa njia hiyo kwa msingi wa dhana ya kibinadamu ya upendezi wa lugha, tokeo likawa ukosefu mwingi wa usahihi katika tafsiri nyingi za Biblia. Shukrani zimwendee Mungu kwamba ametoa New World Translation, yenye maandishi-awali ya Biblia yaliyo wazi na sahihi! Jina lake tukufu, Yehova, na litakaswe katika mioyo ya wote wanaoisoma!
[Maelezo ya Chini]
a Miongoni mwa sosaiti za Biblia nyingi zilizofanyizwa tangu 1804 ni Sosaiti ya Biblia ya Amerika (1816), iliyoundwa kutokana na sosaiti za huko ambazo tayari zilikuwa zimekuwako, na pia Sosaiti ya Biblia ya Edinburgh (1809) na Sosaiti ya Biblia ya Glasgow (1812), zote mbili ziliunganishwa kuwa shirika moja (1861) katika Sosaiti ya Biblia ya Kitaifa ya Scotland. Kufikia 1820 sosaiti za Biblia zilikuwa zimeundwa pia katika Switzerland, Ireland, Ufaransa, Finland, Sweden, Denmark, Norway, Uholanzi, Iceland, Urusi, na Ujerumani.
b Alexander Thomson, The Differentiator, Juni 1954, ukurasa 131.
c Juni 12, 1989, imetafsiriwa kutoka Kijerumani.
[Chati katika ukurasa wa 322]
BAADHI YA TAFSIRI ZA BIBLIA ZENYE KUTOKEZA KATIKA LUGHA SABA KUBWA
Jina la Awali Maandishi-awali Jina la Kimungu Maandishi-awali
Tafsiri Ilitangazwa ya Msingi kwa Limetafsiriwa ya Msingi
Maandiko ya kwa Maandiko
Kiebrania ya Kigiriki
KIINGEREZA
Rheims-Douay* 1582-1610 Vulgate Bwana Vulgate
(ADONAI, mara mbili)
King James
Version* 1611 M BWANA Received
(Yehova, chache) Text
Young 1862-98 M Yehova Received
Text
English 1881-95 M BWANA Westcott
Revised* (Yehova, na Hort
chache)
Emphasised Bible 1878-1902 M Yahweh Westcott
(Ginsburg) na Hort,
Tregelles
American 1901 M Yehova Westcott
Stnaard na Hort
An American 1923-39 M BWANA Westcott
Translation (Yahweh, chache) na Hort
(Smith-Goodspeed)*
Revised 1946-52 M BWANA Westcott
Stnaard* na Hort,
Nestle
New English 1961-70 M (BHK) BWANA New
Bible* (Yehova, chache) eclectic
text
Today’s 1966-76 M (BHK) BWANA UBS
English Version
New King 1979-82 M (BHS) BWANA Majority
James Bible/ (YAH, chache) Text
Revised
Authorised Version
New Jerusalem 1985 M Yahweh Kigriki
Bible*
SPANISH
Valera 1602 M Jehová Received
Text
Moderna 1893 M Jehová Scrivener
Nácar-Colunga* 1944 M Yavé Kigriki
Evaristo Martín 1964 M Yavé Kigriki
Nieto*
Serafín de 1965 M (BHK) Yahvéh, Señor Nestle-
Ausejo* Alna
Biblia de 1967 M Yahveh Kigriki
Jerusalén*
Cantera- 1975 M (BHK) Yahveh Kigriki
Iglesias*
Nueva Biblia 1975 M Señor Kigriki
Española*
PORTUGUESE
Almeida 1681, 1750 M Yehova Received
Text
Figueiredo* 1778-90 Vulgate Senhor Vulgate
Matos Soares* 1927-30 Vulgate Senhor Vulgate
Pontifício 1967 M Javé Merk
Instituto
Bíblico*
Jerusalém* 1976, 1981 M Iahweh Kigriki
GERMAN
Luther* 1522, 1534 M HErr Erasmus
Zürcher 1531 M Herr, Jahwe Kigriki
Elberfelder 1855, 1871 M Jehova Received
Text
Menge 1926 M HErr Kigriki
Luther 1964, 1984 M HERR Kigriki
(revised)*
Bibel in 1967 M (BHS) Herr Nestle-
heutigem Alna,
Deutsch (Gute UBS
Nachricht)*
Einheitsübersetzung*
1972, 1974 M Herr, Jahwe Kigriki
Revidierte
Elberfelder 1975, 1985 M HERR, Jahwe Kigriki
FRENCH
Darby 1859, 1885 M Eternel Kigriki
Crampon* 1894-1904 M Jéhovah Merk
Jérusalem* 1948-54 Vulgate, Yahvé Vulgate,
Hebrew Kigriki
TOB Ecumenical 1971-75 M (BHS) Seigneur Nestle,
Bible* UBS
Osty* 1973 M Yahvé Kigriki
Segond Revised 1978 M (BHS) Eternel Nestle-
Alna,
Black,
Metzger,
Wikgren
Français 1982 M (BHS) Seigneur Nestle,
courant UBS
DUTCH (NETHERLANDS)
Statenvertaling 1637 M HEERE Received
Text
Leidse 1899-1912 M Jahwe Nestle
Vertaling
Petrus-Canisiusvertaling*
1929-39 M Jahweh Nestle
NBG-vertaling 1939-51 M HERE Nestle
Willibrordvertaling*
1961-75 M Jahwe Nestle
Groot Nieuws 1972-83 M Heer Nestle
Bijbel*
ITALIAN
Diodati 1607, 1641 M Signore Kigriki
Riveduta 1921-30
M Eterno Kigriki
(Luzzi)
Nardoni* 1960 M Signore, Jahweh Kigriki
Pontificio 1923-58 M Signore, Jahve Merk
Istituto
Biblico*
Garofalo* 1960 M Jahve, Signore Kigriki
Concordata* 1968 M (BHK) Signore, Iavè Nestle,
Merk
CEI* 1971 M Signore Kigriki
Parola del 1976-85 M (BHS) Signore UBS
Signore*
* Alama-nyota huonyesha kwamba Apocrypha ilitiwa ndani lakini huenda isiwemo katika chapa zote.
“M” hurejezea maandishi-awali ya Kimasora. Inapokuwa peke yake, hakuna chapa yoyote maalumu ya maandishi-awali ya Kimasora yanayotajwa moja kwa moja.
“BHK” hurejezea Biblia Hebraica ya Kittel.
“UBS” hurejezea The Greek New Testament, ya United Bible Societies.
“BHS” hurejezea Biblia Hebraica Stuttgartensia.
“Kigriki” huonyesha tafsiri iliyofanywa kutoka Kigiriki, lakini hakuna maandishi-awali maalumu yanayoonyeshwa.