Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rs uku. 293-uku. 297
  • Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mtu Akisema—
  • Hatua Muhimu kwa Wapendao Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Tafsiri ya New World Translation Inathaminiwa na Mamilioni ya Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kuchapa na Kugawanya Neno Takatifu la Mungu Mwenyewe
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Tafsiri Bora ya Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
rs uku. 293-uku. 297

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Maana: Tafsiri ya Maandiko Matakatifu iliyotafsiriwa na halmashauri ya mashahidi watiwa-mafuta wa Yehova. Biblia hii ilitafsiriwa katika Kiingereza cha kisasa moja kwa moja kutoka lugha za Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Watafsiri hao walisema hivi kuhusu kazi yao: “Watafsiri wa kitabu hiki, ambao wanamwogopa na kumpenda Mungu aliye Mtungaji wa Maandiko Matakatifu, wanatambua kwamba wana wajibu wa pekee kwake wa kupitisha mawazo na matangazo yake kwa usahihi kadiri inavyowezekana. Wanatambua pia kwamba wana wajibu kwa wasomaji wanaofanya uchunguzi, ambao wanaitegemea tafsiri ya Neno lililoongozwa na roho ya Mungu Aliye Juu Zaidi kwa ajili ya wokovu wao wa milele.” Mwanzoni tafsiri hii ilitolewa sehemu-sehemu, kuanzia mwaka wa 1950 mpaka mwaka wa 1960. Chapa za lugha nyingine zimetegemea tafsiri ya Kiingereza.

“Tafsiri ya Ulimwengu Mpya” inategemea nini?

Ili kutafsiri Maandiko ya Kiebrania, maandishi yaliyotumiwa yanatoka katika Biblia Hebraica ya Rudolf Kittel, chapa za 1951-1955. Chapa iliyorekebishwa ya mwaka wa 1984 [Kiingereza] ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliboreshwa kupatana na chapa ya Biblia Hebraica Stuttgartensia ya mwaka wa 1977. Zaidi ya hayo, Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi na tafsiri nyingi za zamani katika lugha nyingine vilitumiwa. Kuhusu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, kwa ujumla maandishi ya Kigiriki ya mwaka wa 1881 yaliyoandikwa na Westcott na Hort yalitumiwa, lakini maandishi mengine kadhaa yalichunguzwa na vilevile tafsiri nyingi za zamani katika lugha nyingine.

Watafsiri walikuwa nani?

Walipokuwa wakitoa kama zawadi haki za kuchapisha tafsiri yao, washiriki wa Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya waliomba kwamba majina yao yasitajwe. Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania imeheshimu ombi lao. Watafsiri hao hawakuwa wakijitafutia umashuhuri bali walitaka tu kumheshimu Mungu aliye Mtungaji wa Maandiko Matakatifu.

Kwa miaka mingi, halmashauri nyingine za kutafsiri zimefuata maoni kama hayo. Kwa mfano, maandishi kwenye jalada la Chapa ya Marejeo (1971) ya New American Standard Bible yanasema: “Sisi hatukutumia jina la msomi yeyote kwa ajili ya marejeleo wala mapendekezo kwa sababu tunaamini kwamba Neno la Mungu linapaswa litegemee sifa zake lenyewe.”

Je, kweli tafsiri hiyo ni ya kitaalamu?

Kwa kuwa watafsiri wamesema majina yao yasitajwe, swali hilo haliwezi kujibiwa kuhusiana na kiwango cha masomo yao. Ni lazima tafsiri hiyo ipimwe kwa msingi wa sifa zake yenyewe.

Hii ni tafsiri ya aina gani? Kwanza, ni tafsiri sahihi, hasa iliyo ya moja kwa moja kutoka zile lugha za kwanza. Hiyo si masimulizi ya kijuu-juu tu, ambapo watafsiri wanaacha mambo fulani wanayoona kwamba si muhimu kisha wanaongeza mawazo wanayoamini kwamba yatasaidia. Ili kuwasaidia wanafunzi, chapa kadhaa zinatoa vielezi-chini vingi vinavyoonyesha maneno mbalimbali ambayo yanaweza kutafsiriwa kwa usahihi katika njia zaidi ya moja, pia orodha ya hati hususa za kale ambazo ni msingi wa tafsiri fulani.

Huenda mistari fulani haisemi kama vile ambavyo mtu fulani amezoea. Ni tafsiri ipi iliyo sahihi? Wasomaji wanaalikwa wachunguze hati zinazounga mkono ambazo zimetajwa katika vielezi-chini vya chapa ya Marejeo ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, wasome maelezo yaliyotolewa katika nyongeza, na kulinganisha tafsiri hiyo na tafsiri nyingine mbalimbali. Kwa ujumla wataona kwamba watafsiri fulani wengine nao pia wameona uhitaji wa kueleza jambo hilo kwa njia hiyohiyo.

Kwa nini jina Yehova limetumiwa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo?

Kumbuka kwamba Tafsiri ya Ulimwengu Mpya siyo Biblia pekee inayofanya hivyo. Jina la Mungu linapatikana katika tafsiri za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiebrania, katika vifungu ambapo manukuu yamefanywa moja kwa moja kutoka Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na roho ya Mungu. Biblia The Emphatic Diaglott (1864) ina jina Yehova mara 18. Tafsiri za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika angalau lugha nyingine 38 pia zinatumia namna ya jina la Mungu katika lugha zao.

Jinsi ambavyo Yesu Kristo alikazia jina la Baba yake inaonyesha kwamba yeye binafsi alilitumia kwa uhuru. (Mt. 6:9; Yoh. 17:6, 26) Kulingana na Jerome wa karne ya nne W.K., mtume Mathayo aliandika Injili yake kwanza katika Kiebrania, na Injili hiyo inanukuu vifungu vingi kutoka Maandiko ya Kiebrania vilivyo na jina la Mungu. Waandikaji wengine wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo walinukuu kutoka Septuajinti ya Kigiriki (ambayo ni tafsiri ya Maandiko ya Kiebrania katika Kigiriki, iliyoanzwa karibu mwaka wa 280 K.W.K.), ambayo nakala zake za kwanza zina jina la Mungu katika herufi za Kiebrania, kama inavyoonyeshwa na visehemu vya chapa hiyo ambavyo vimehifadhiwa.

Profesa George Howard wa Chuo Kikuu cha Georgia aliandika hivi: “Kwa kuwa Tetragramu [herufi nne za Kiebrania za jina la Mungu] ilikuwa bado imeandikwa katika nakala za Biblia za Kigiriki zilizofanyiza Maandiko ya kanisa la kwanza, ni jambo linalopatana na akili kuamini kwamba waandikaji wa [A]gano [J]ipya, wakati wa kunukuu kutoka Andiko, walihifadhi Tetragramu ndani ya maandishi ya Biblia.”—Journal of Biblical Literature, Machi 1977, uku. 77.

Kwa nini inaonekana mistari fulani inakosekana?

Mistari hiyo, inayopatikana katika tafsiri fulani, haimo katika hati za kale zaidi zilizopo za Biblia. Tafsiri hii inapolinganishwa na tafsiri za kisasa, kama vile The New English Bible na Jerusalem Bible ya Kikatoliki, huonyesha watafsiri wengine pia wametambua kwamba mistari hiyo haipaswi kuwa katika Biblia. Katika visa fulani, mistari hiyo ilichukuliwa kutoka sehemu nyingine ya Biblia na kuongezwa kwenye maandishi yaliyokuwa yakinukuliwa na mwandishi.

Mtu Akisema—

‘Ninyi mna Biblia yenu wenyewe’

Unaweza kujibu hivi: ‘Wewe una tafsiri gani ya Biblia? Je, ni... (taja kadhaa katika lugha yenu)? Kuna tafsiri nyingi.’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Niko tayari kutumia tafsiri yoyote unayopenda. Lakini labda utapenda kujua kwa nini hasa mimi naipenda Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Ni kwa sababu ina lugha ya kisasa, yenye kueleweka, pia kwa sababu watafsiri walishikamana sana na yaliyo katika lugha za kwanza za Biblia.’

Au unaweza kusema: ‘Jambo unalosema linafanya nihisi kwamba lazima una Biblia nyumbani mwako. Wewe hutumia tafsiri gani ya Biblia?... Ungependa kuileta?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Kwetu sote, bila kujali tafsiri tunayotumia, katika Yohana 17:3 Yesu alikazia jambo muhimu la kukumbuka, kama unavyoweza kuona hapa katika Biblia yako mwenyewe. . . . ’

Pia unaweza kusema: ‘Kuna tafsiri nyingi za Biblia. Mashahidi wa Yehova huwatia moyo watu watumie tafsiri mbalimbali ili kulinganisha na kuwasaidia wanafunzi wafahamu maana halisi ya Maandiko. Labda unajua kwamba hapo mwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Kwa hiyo tunathamini yale ambayo watafsiri wamefanya ili kuitafsiri katika lugha yetu. Wewe unatumia tafsiri gani ya Biblia?’

Pendekezo lingine: ‘Inaonekana wewe unalipenda Neno la Mungu. Kwa hiyo nina hakika utapenda kujua tofauti moja kubwa kati ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na tafsiri nyingine. Inahusu jina la mtu aliye mashuhuri zaidi anayetajwa katika Maandiko. Unamjua huyo ni nani?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, unajua kwamba jina lake la kibinafsi linapatikana katika Biblia ya Kiebrania cha zamani mara 7,000 hivi—zaidi ya jina lingine lolote?’ (2) ‘Je, kuna tofauti yoyote ikiwa tunalitumia au hatulitumii jina la kibinafsi la Mungu? Je, una rafiki wowote wa karibu kwelikweli ambao hujui majina yao? . . . Ikiwa tunataka kuwa rafiki za Mungu, ni muhimu kwanza tulijue jina lake. Tafadhali ona jambo ambalo Yesu alisema katika Yohana 17:3, 6. (Zab. 83:18)’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki