Wimbo 1
“Bariki Yehova, Ee Nafsi Yangu”
1. Bariki Yehova nafsi
—Midomo sifu jina lake—
Asameheye makosa,
Huondoa huzuni yote.
Haoni hasira upesi,
Kazi zake zaonyesha.
Wote wachao Yehova,
Wataziona fadhili.
2. Kama vile baba, Mungu,
Ajua sisi ni mavumbi,
Na kama ua kondeni,
Sisi tutanyauka mara.
Fadhili za Yehova Mungu
Ni kwa wale watiifu.
Tukikumbuka agizo,
Haki yatutegemeza.
3. Yehova amekiweka,
Kiti cha Ufalme mbinguni.
Anavitawala vyote;
Ameonyesha nguvu zake.
Mubarikini, malaika;
Lisifuni jina lake.
Jeshi lote barikini.
Bariki Yehova, nafsi.