Wimbo 211
Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha
1. Huu wakati wa mavuno,
Pendeleo kubwa sana.
Malaika ni “wavunaji,”
Tunayashiriki pia.
Yesu ameanzisha mambo,
Kapanda mbegu “shambani.”
Mazao ni tayari kuvunwa;
Na tuvune kwa furaha.
2. “Ngano” ni tayari “ghalani.”
Na “magugu” yametengwa.
Wajaribu kutuzuia,
“Wanasaga” meno yao.
Watu wa Yehova kazini.
Muchana kutwa kazini.
Mavuno ya kondoo ni mengi,
Tusaidie daima.
3. Kupenda Mungu na jirani
Kunatuhimiza mbio.
Kuvuna kazi ya haraka,
Sasa wakati wa mwisho.
Tuchukue hatua sasa,
Kusaidia wengine
Furahi shambani kila siku,
Wapya watambue “ngano.”
4. Muvunaji Yesu aona,
Nafaka zimeshaiva,
Mashamba yetu ni “meupe”!
Na wengi wataka funzo!
Furaha zetu nyingi sana,
Tu washirika na Mungu.
Ni kazi ya furaha kabisa;
Tumupende na kuvuna.