Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 3/1 uku. 14
  • Kuvuna Katika “Wakati wa Mwisho”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuvuna Katika “Wakati wa Mwisho”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “SYNTEʹLEIA” NA “TELOS”
  • “MAVUNO YA DUNIA YAMEIVA KABISA”
  • MAGUGU YAKUSANYWA ILI YATEKETEZWE KWA MOTO
  • ‘WENYE HAKI WANG’AA KWA UANGAVU KAMA JUA’
  • ‘MAVUNO YA DUNIA’ YAENDELEA
  • “Tazama! Mimi Nipo Pamoja Nanyi Siku Zote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Shamba Lenye Kuzaa Ngano na Magugu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Mfano wa Ngano na Magugu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 3/1 uku. 14

Kuvuna Katika “Wakati wa Mwisho”

“Mavuno ni umalizio wa mfumo wa mambo.”​—Mt. 13:39, NW.

1. Kwa sababu gani “mavuno” yaliyotabiriwa na Yesu yanatoa sababu yenye sehemu mbili za kufurahisha?

MAVUNO mazuri wakati wote ni sababu ya kuwa na furaha na kutolea shukrani. Unakuwa ni wakati wa kuvuna matunda ya kazi ngumu ya muda mrefu. Mavuno yaliyotabiriwa katika mfano wa Kristo ya “ngano” na “magugu” yangetoa sababu yenye sehemu mbili ili wanadamu wote wafurahi. Kwa sababu gani? Si kwa sababu tu ingemaanisha kukusanya hesabu inayotakiwa ya “wana wa ufalme,” au “watakatifu,” watakaoshiriki na Kristo katika “mamlaka yake ya milele,” kwa njia hiyo dunia ihakikishiwe kuwa na serikali nzuri, bali pia kwa sababu “mavuno” hayo yenyewe yangekuwa uthibitisho kwamba tunaishi katika “umalizio wa mfumo wa mambo” (conclusion of a system of things) na tunaishi katika mapambazuko ya taratibu mpya (new order) yenye haki.​—Dan. 7:14, 27, ZSB; Mt. 13:38, 39, NW; 2 Pet. 3:13, NW.

“SYNTEʹLEIA” NA “TELOS”

2. Kwa sababu gani neno “umalizio” linatafsiri vizuri zaidi neno la Kigiriki synteʹleia kuliko neno “mwisho,” na kwa hiyo synteʹleia hiyo inalingana na kipindi gani kinachotajwa katika Danieli?

2 Yesu hakusema kwamba “mavuno” ni “mwisho wa ulimwengu (dunia),” kama ambavyo tafsiri; nyingine za Biblia zinavyotaka tuamini. (Union Version; Zaire Swahili Bible; Habari Njema kwa Watu Wote) Tafsiri hizo hazitofautishi kati ya maneno mawili ya Kigiriki synteʹleia na telos. Kikieleza synteʹleia kitabu Expository Dictionary of New Testament Words cha W. E. Vine kinasema hivi: “Neno hilo halimaanishi kikomo, bali kuelekea kwa matukio kwenye upeo uliowekwa.” Kwa hiyo Yesu aliposema “mavuno ni umalizio [synteʹleia] wa mfumo wa mambo,” alikuwa akisema juu ya kipindi cha utendaji ambacho kingekuwa na mwanzo na mwisho. Kulingana na Mathayo 13:30, NW, Yesu alitaja “kipindi cha mavuno,” bila shaka akiwa anamaanisha kipindi cha wakati, kipindi ambacho Danieli alikitaja kuwa “wakati wa mwisho.” (Dan. 12:4) Kwa kupendeza, wakati watafsiri wa Septuagint Version ya Kigiriki walipoutafsiri mstari huo katika Danieli, walilitumia neno synteʹleia.

3. “Kipindi ha mavuno” kinahusiana na nini, na neno la Kigiriki telos linamaanisha na linahusu nini katika Mathayo 24:14?

3 Neno ilo hilo linatumiwa katika Mathayo 24:3, NW, mahali ambapo wanafunzi walimwuliza Yesu hivi: “Tuambie, mambo hayo yatakuwa wakati gani, na nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio [synteʹleia] wa mfumo wa mambo?” Kwa hiyo “kipindi cha mavuno” kinahusiana na kuwapo kusikoonekana kwa Kristo akiwa Mvunaji. Katika kulijibu ulizo la wanafunzi wake, Yesu alieleza juu ya vita vya mataifa yote, upungufu wa chakula, maradhi ya kuambukia, matetemeko makubwa ya ardhi, uvunjaji wa sheria na kuenea kwa woga. (Linganisha masimulizi yanayofanana na hayo katika Mathayo 24, Marko 13 na Luka 21) Kisha, akionyesha kwamba “kipindi cha mavuno” kingefikia mwisho, yeye aliongeza hivi: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho [telos] utakapokuja.” (Mt. 24:14, NW) Neno telos linamaanisha “mwisho,” “katika maana ya kimalizio, kikomo . . . sehemu ya mwisho, kifungo, umalizio sana-sana wa mambo ya mwisho, tendo la mwisho katika ulimwengu.”a

4. “Umalizio,” au “wakati wa mwisho,” ulianza wakati gani, na kwa hiyo ni jambo gani linaloweza kusemwa juu ya “mavuno”?

4 Mambo ya hakika ya historia ya kisasa tangu 1914, yakitimiza unabii wa Biblia, yanaonyesha kwamba mfumo wa mambo (system of things) uliopo umeingia ndani sana katika ‘wakati wake wa mwisho,’ au “umalizio” (synte’leia). Kwa kurudia kutaja maneno ya W. E. Vine, tunashuhudia “kuelekea kwa matukio kwenye upeo uliowekwa” au mwisho (telos). Kwa hiyo, “mavuno” ya mfano wa Yesu lazima yawe yanaendelea; kwa kweli, lazima yawe yanakaribia upeo wake. Je! matukio yaliyotabiriwa katika sehemu nyingine ya mfano huo yanaonekana tangu mwaka 1914?

“MAVUNO YA DUNIA YAMEIVA KABISA”

5. Wakati wa mavuno, “Mwana wa mtu” angewaagiza malaika zake wafanye nini?

5 Akiendelea na maelezo yake ya “mfano wa yale magugu katika shamba,” Yesu alisema hivi: “Mavuno ni umalizio wa mfumo wa mambo na wavunaji ni malaika. Kwa hiyo, kama ambavyo magugu yanavyokusanywa na kuteketezwa kwa moto ndivyo itakavyokuwa katika umalizio wa mfumo wa mambo. Mwana wa mtu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka ufalme wake vitu vyote vinavyoleta kukwazika na watu wanaovunja sheria, nao watawatupa katika joko lenye moto. Hapo ndipo kulia na kusaga meno yao kutakapokuwa.”​—Mt. 13:39-42, NW.

6. “Ngano” iliruhusiwa ikue kati ya nani?

6 Wale “wavunaji,” au malaika, wangetumwa na “Mwana wa mtu” katika “umalizio wa mfumo wa mambo,” ili wayang’oe magugu yatoke katikati ya wale “wana wa ufalme” wa kweli “vitu vyote vinavyoleta kukwazika na watu wanaovunja sheria.” Kama ambavyo makala inayotangulia ilivyoonyesha, kurudia kupanda “magugu”kwa Ibilisi wakati wa usiku kumetokeza uasi-imani ulio tengenezo, Ukristo wa uongo ukiongozwa na jamii ya viongozi wa kidini wenye kuonea waliokuja kuwa jamii ya “mtu wa kuasi” aliyetabiriwa na mtume Paulo. (2 The. 2:3-13) “Ngano” ya kweli iliachwa iendelee kukua katikati ya “magugu” mpaka “wakati wa mwisho.” Ndipo “Mwana wa mtu” angewaagiza “wavunaji” wake watenganishe wale “wana wa ufalme” na “wana wa yule mwovu.”

7. Ni unabii gani unaofanana na huo unaotusaidia tuutambue wakati wa mavuno?

7 Kazi hii ya kutenga ilianza wakati gani? Unabii unaofanana na huo wenye kupendeza hautuachi na shaka juu ya wakati jambo hilo lilipoanza. Unasema hivi: “Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa chake na katika mkono wake mundu mkali. Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya [dunia] yamekomaa. Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya [dunia], [dunia] ikavunwa.”​—Ufu. 14:14-16.

8. “Mwana wa mtu” anaelezwaje katika Ufunuo 14:14, na kwa hiyo lazima mavuno yawe yalianza baada ya tukio gani?

8 Hapa tunamwona “Mwana wa mtu,” Yesu Kristo, akiwa si kama mpanzi anayepanda “mbegu njema katika shamba lake” bali akiwa mfalme aliyetawaza akienda kwenye ‘mavuno ya dunia.’ Kuketi kwake juu ya wingu kunafananisha kuwapo kwake kusikoonekana. (Matendo 1:9-11; Ufu. 1:7) Kwa hiyo, lazima “mavuno” yatokee wakati wa kuwapo kwa Kristo, baada ya yeye kutawazwa na kupokea “mamlaka, na utukufu, na ufalme” kutoka kwa Yehova, yule “Muzee wa Siku.” (Dan. 7:13, 14, ZSB) Kwa hiyo mavuno, yalianza wakati fulani baada ya 1914 mwaka ule ambao ulikuwa ndio mwanzo wa “wakati wa mwisho,” au “umalizio wa mfumo wa mambo.”

9. Kazi ya kutenga ilianza wakati gani?

9 Baada ya 1914, ni wakati gani Mwana wa mtu ‘alipowatuma malaika zake wakatenge wale “wana wa ufalme” na wale “wana wa yule mwovu,” “ngano” ya kuigisha, yaani, “watu wanaovunja sheria” ambao ndani yao “mtu wa kuasi anatiwa, viongozi wa kidini wa Ukristo wa bandia? Lazima jibu lipatane na mambo ya hakika, nayo yanaonyesha kwamba katika mwaka 1919 ndipo wale “wana wa ufalme” waliotiwa mafuta wakazaliwa kwa roho, wanaofananishwa na “ngano” walipoanza kutengwa na “magugu” au Wakristo wa uongo, ambao walikuwa wameingilia na kufunika shamba la kidini la wanadamu. ‘Mavuno ya dunia’ yalikuwa yameiva nao wakati ulikuwa umefika kwa “Mwana wa mtu” kutii mundu wake na kuvuna. Mfano huu una onyesha wazi kwamba alifanya hivyo kupitia “wavunaji” wake, malaika.

MAGUGU YAKUSANYWA ILI YATEKETEZWE KWA MOTO

10. Kwa sababu gani ilikuwa vigumu kutambua ‘‘ngano” ya kweli wakati wa karne zote zilizopita, walakini ni tangu lini imewezekana kutambua wazi “ngano” na “magugu”?

10 Katika ‘mfano wake wa magugu katika shamba,’ Yesu alisema: “Katika kipindi cha mavuno nitawaambia wavunaji, Kwanza kusanyeni magugu myafunge katika matita ili myateketeze kwa moto.” (Mt. 13:30, NW) Kwa karne nyingi “ngano,” au “wana wa ufalme,” hawakuwa wanaonekana wazi kwa sababu ya “magugu” yenye kuzaana sana, au Wakristo waasi-imani, waliodai kuwa na tumaini la kimbinguni la kuwa warithi wa ule Ufalme. Ni baada tu ya 1919, wakati Wakristo waliozaliwa kwa roho kikweli walipokombolewa kutoka Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo ya Ibilisi, ndipo tofauti iliyo wazi ilipoonekana kati ya “ngano” na yale “magugu.”

11. Ni nani wanaotiwa katika “magugu,” nao wamefungwaje katika matita?

11 “Magugu” ya mfano yanatia Wakristo wote wa bandia, kutia waasi-imani wo wote wa kisasa wanaofundisha “vitu vinavyoleta kukwazika,” pamoja na “watu wanaovunja sheria.” Hiyo ingetia yule “mtumwa mwovu,” wale ‘wanawali wapumbavu’ na yule ‘mtumwa mbaya na mlegevu.’ (Mt. 24:48-51; 25:1-12, 14-30) ‘Kufungwa katika matita’ kwa magugu yakiwa tayari kuteketezwa kwa moto hakufananishi kuwekwa kwayo katika vikundi na madhehebu mbalimbali ya Jumuiya ya Wakristo, kwa maana haiwezi kusemwa hata kidogo kwamba malaika ndio wenye hatia ya mifumo (systems) hiyo ya makanisa ya uasi-imani. Na zaidi, kufungwa na kuwekwa katika matita kunatokea wakati wa “kipindi cha mavuno,” katika “wakati wa mwisho,” na ambapo dini nyingi za Ukristo wa bandia (udanganyifu) zimekuwapo kwa karne nyingi. Kufungwa katika matita kwa “magugu” kunamaanisha kwamba tangu mwaka 1919 kutenga Wakristo wa kweli na wa kuigisha kumekuwa wazi zaidi na zaidi katika akili za watu na kwa kutenga halisi kumeonekana wazi zaidi na zaidi. Yale “magugu,” au wale “wana wa yule mwovu,” ‘wanafungwa’ kwa kuwa malaika wanahakikisha kwamba hawarudi kuingia katikati ya “ngano,” au “wana wa ufalme” wa kweli.

12. “Joko lenye moto” linafananisha nini, na “magugu” yatatupwa ndani yalo wakati gani?

12 Akisema juu ya yale ambayo malaika wangefanya kwa “magugu” baada ya kuyafunga, Yesu aliongeza hivi: “Nao watayatupa katika joko lenye moto. Hapo ndipo kulia na kusaga meno yao kutakapokuwa.” (Mt. 13:42, NW) Kumbuka kwamba tunachunguza mfano. Ikiwa “ngano” na “magugu” ni ya mfano, ndivyo na “joko lenye moto,” kule “kulia” na kule “kusaga meno.” Mathayo 25:41, 46, NW, inaonyesha kwamba “moto wa milele” unafananisha “kukatiliwa mbali milele,” na Ufunuo (20:14; 21:8) unasema kwamba lile “ziwa la moto” linamaanisha “mauti ya pili,” uharibifu usio na tumaini la ufufuo. Kwa hiyo “magugu” yanaelekea kuharibiwa.

13. Wale wanaofananishwa na magugu wamelia na kusaga meno yao wakati gani na namna gani, walakini wataomboleza zaidi wakati gani?

13 Kwa kuwa lile “joko lenye moto” linafananisha uharibifu kamili, kule “kulia na kusaga meno yao” kwa “magugu” lazima kutokee kabla hawajaharibiwa. Kwa miongo mingi ya miaka (makumi mengi ya miaka) sasa, Wakristo bandia, na sana-sana yule “mtu wa kuasi,” viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wamekuwa wakilia kwamba wale “wana wa ufalme,” mashahidi waliotiwa mafuta wa Yehova wamekuwa wakiwapiga kwa kweli za Kimaandiko zenye kupiga kwa nguvu, kwa kuwafunua wazi namna walivyo, “wana wa yule mwovu.” (Mt. 13:38, NW; Ufu., sura 8, 9b) Viongozi wa kidini wenye kuasi imani wamesaga meno yao juu ya Mashahidi wa Yehova kwa ajili ya kutangaza bila kuogopa “mwaka wa nia njema” wa Yehova na pia ‘siku yake ya kisasi.’ (Isa. 61:1, 2) Hata hivyo, “magugu” hayo yote yatalia zaidi na kusaga meno zaidi wakati “Mwana wa mtu” atakapokuja hivi karibuni na kuwaharibu wao pamoja na sehemu nyingine ya ulimwengu wa Shetani.​—Mt. 24:30.

‘WENYE HAKI WANG’AA KWA UANGAVU KAMA JUA’

14. “Ngano” inakusanywa wapi, na hao “wenye haki” wanafanya nini?

14 Baada ya kuwaagiza “wavunaji” wafunge katika matita yale “magugu” ili yaharibiwe “Mwana wa mtu” anawapa malaika zake amri hii inayofuata: “Kisha mkusanye ngano katika ghala yangu.” (Mt. 13:30, NW) Na Yesu alimalizia maneno yake ya mfano huo kwa kusema, “wakati huo wenye haki watang’aa kwa uangavu kama jua katika ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na asikilize.”​—Mt. 13:43, NW.

15, 16. (a) Kwa sababu gani “wenye haki” hawang’ai wakiwa mbinguni? (b) “Wenye haki” wanang’aa wakiwa wapi na kwa namna gani, nao wanakusanywa wapi?

15 Ufunuo 21:23 unasema hivi juu ya hiyo serikali ya Ufalme ya kimbinguni, huo Yerusalemu Mpya: “Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru na taa yake ni Mwana-Kondoo.” Kwa hiyo huo ufalme wa kimbinguni hautegemei nuru ya “wana wa ufalme” waliofufuliwa. Umejawa sana na nuru tukufu ya kimungu. Ni tofauti kama nini kati ya mataifa hapa duniani! (Efe. 4:17, 18; 5:8) Akieleza yale Yehova anafanya kwa “wana wa ufalme” wanapokuwa bado duniani, Paulo anaandika hivi: “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.”​—Kol. 1:13.

16 Kwa hiyo, “wenye haki” wanaong’aa “kwa uangavu kama jua katika ufalme wa Baba yao” maana yake ni hali ya kupewa maarifa na ya utumishi mtukufu ya Wakristo hao waliotiwa mafuta duniani, ambapo wao ‘wanang’aa kama vimulikaji katika ulimwengu.’ (Flp. 2:15, NW; Mt. 5:14) Ile “ghala” ambayo wamekusanywa ndani yake tangu 1919 yaweza kusemwa kuwa ni “ufalme wa Baba yao,” kwa kuwa kundi la Kikristo ni tengenezo la Kitheokrasi linaloitambua enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova. Hilo ni tengenezo safi, kwa maana ni kutoka kwalo malaika wanakusanya “vitu vyote vinavyoleta kukwazika na watu wanaovunja sheria.”​—Mt. 13:30, 41, 43, NW.

‘MAVUNO YA DUNIA’ YAENDELEA

17. Ni “wana wa ufalme” wangapi wanaovunwa, walakini ni kwa sababu gani kazi ya kukusanya inaendelea?

17 Yote haya yanakuhusuje wewe? Kumbuka kwamba Yesu aliumalizia mfano huo kwa maneno haya: “Yeye aliye na masikio na asikilize.” (Mt. 13:43, NW) Ni kweli kwamba mfano huo unaonyesha kukusanywa kwa hesabu yote ya “wana wa ufalme” wanaotakiwa wajumuishwe (wafanyizwe) kuwa serikali ya kimbinguni ya Kristo. Sura iyo hiyo (14) ya Ufunuo inayosema juu ya ‘mavuno ya dunia inaonyesha wazi hesabu ya wale wanaovunwa kwa njia hiyo ili watawale pamoja na “Mwana-Kondoo” katika “Mlima Sayuni” wa kimbinguni kuwa 144,000. Walakini sura hiyo inaongeza hivi: “Hao walinunuliwa kutoka katikati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-kondoo.” (Ufu. 14:1, 4 NW) Kuvunwa kwa “matunda ya kwanza” kunaonyesha kwamba kungekuwa matunda mengine ya kukusanywa baadaye kama inavyoonyeshwa na kukusanywa kwa yale matunda mengine ya lile shamba mwishoni mwa mwaka wa mavuno. Kwa hiyo kukusanywa huko kunaendelea, nako kunakuhusu wewe.

18. Pamoja na kuvunwa kwa wale “wana wa ufalme,” ni kazi gani nyingine ya kutenga inayofanywa?

18 Kukusanywa kwa “wana wa ufalme” kulianza tangu mwaka 1919 na kuendelea mpaka miaka ya 1930 na kitu. Kwa sababu Wakristo hao waaminifu waliotiwa mafuta ‘wameacha nuru zao ziangaze’ wengine wengi wenye masikio yenye kusikiliza wamekubali watengwe na “magugu” au Wakristo wa bandia waliomo katika makanisa na madhehebu ya Jumuiya ya Wakristo. (Mt. 5:16) Kazi hii ya kutenga vilevile ilitabiriwa na Yesu katika unabii unaohusu “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mt., sura 24, 25) Yeye alisema hivi: “Wakati Mwana wa mtu atakapofika katika utukufu wake, na malaika zote wakiwa pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha enzi. Na mataifa yote yatakusanywa mbele yake, naye atatenga watu mmoja kutoka kwa mwingine, kama vile mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. Naye ataweka kondoo kwenye mkono wake wa kulia, lakini mbuzi kwenye mkono wake wa kushoto. Na hawa [mbuzi] wataondoka waende kwenye kukatiliwa mbali kwa milele, bali wenye haki kwenye uzima wa milele.”​—Mt. 25:31-33, 46, NW.

19. Katika wakati wake Mungu, ni jambo gani litakalowapata waliobaki wa jamii ya “ngano” na ule “mkutano mkubwa”?

19 Basi, kwa kadiri kuvunwa kwa jamii ya “ngano” ya Wakristo waliotiwa mafuta kunavyokaribia mwisho wake, kukusanywa kwa wale “kondoo” kunaendelea. Katika wakati wake Mungu, wanaobaki wa jamii ya “ngano” wataumaliza mwendo wao wa kidunia na kujiunga na “Mwana wa mtu” wawe sehemu ya ufalme au serikali yake ya kimbinguni. Wao ‘wataupokea ufalme’ pamoja na wale wengine wa 144,000 “watakatifu.” (Dan. 7:18, 22, 27, ZSB) Kwa habari ya ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo” wanaokusanywa sasa, wataiokoka “dhiki ile iliyo kuu” ambayo ndiyo itauleta mwisho (telos) wa mfumo wa mambo (system of things) wa Shetani uliopo sasa nao watakuwa sehemu ya “watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote” watakakomtumikia “Mwana wa mtu” duniani, chini ya uongozi wa “mamlaka ya milele” yake au ufalme wa kimbinguni.​—Ufu. 7:4, 9, 10, 14; Dan. 7:13, 14, ZSB.

20. Uhakika wa kwamba mavuno yameendelea sana unathibitisha nini; kwa hiyo unapaswa kufanya nini, na kwa sababu gani?

20 Wewe unasimama wapi kuhusiana na utimizo wa mfano wa “ngano” na “magugu”? Uhakika wa kwamba “mavuno” ya wale “wana wa ufalme” yameendelea sana unathibitisha kwamba “umalizio [synteʹleia] wa mfumo wa mambo” unakaribia mwisho (telos) wake. Maoni yako kuwaelekea “ndugu” wa Kristo waliotiwa mafuta wenye mfano wa ngano na namna unavyowatendea yatakuwa mambo yenye kuamua kama utakwenda kwenye “kukatiliwa mbali milele” au kupokea “uzima wa milele.” (Mt. 25:34-46) Jithibitishe mwenyewe kuwa mwenzi mshikamanifu wa jamii ya “ngano” waliotiwa mafuta, “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” ambaye Kristo amemweka ili atoe ‘chakula cha kiroho kwa wakati wake.’ (Mt. 24:45) Endelea kutenda katika kazi ya kukusanya, kwa maana kumbuka, “habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho (telos) utakapokuja,” na “yeye ambaye amevumilia mpaka mwisho [telos] ndiye atakayeokolewa.”​—Mt. 24:13, 14, NW.​—Kutoka The Watchtower, August 1,1981.

[Maelezo ya Chini]

a Kitabu A Greek-English Lexicon of the New Testament and Other Early Christian Literature, W. Bauer, kilichotafsiriwa na W. F. Arndt na F. W. Gingrich.

b Tazama sura 16 na 17 za kitabu “Then Is Finished the Mystery of God,” kilichochapishwa na Sosaiti mwaka 1969.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki