Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Septemba: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? au Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Makutaniko ambayo yana ugavi wa Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani yanaweza kutoa kitabu hicho. Oktoba: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halikubaliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Novemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa kufuatia maangusho yote, tukiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani. Desemba: New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
◼ Ofisi ya tawi inayo akibani ugavi wa kutosha wa kichapo Jehovah’s Witnesses—Proclaimers of God’s Kingdom ya Kiingereza. Kila familia yatiwa moyo kuwa na angalau nakala moja katika maktaba ya familia. Makutaniko yaweza kutoa maombi yao pamoja na agizo lifuatalo la fasihi. Hii ni bidhaa ya kuombwa kipekee.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeagizwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo.
◼ Watangazaji wanaopanga kutumikia wakiwa mapainia-wasaidizi katika Oktoba wapaswa kutoa ombi mapema. Hili litaruhusu wazee wafanye mipango inayohitajiwa kwa ajili ya fasihi na eneo.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyotolewa kwenye kurasa 21-23 za Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu watu wowote waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wana mwelekeo wa kutaka kurudishwa.
◼ Toleo la baada ya kila miezi mitatu la Amkeni! katika Kihiri Motu litasimamishwa. Toleo la Julai-Septemba litakuwa la mwisho.
◼ Kuanzia na toleo la Oktoba-Desemba 1996, Amkeni! litatangazwa katika Kigeorgia likiwa toleo la baada ya kila miezi mitatu.
◼ Kuanzia Januari 1997, Amkeni! la Kimarathi litakuwa kichapo cha mara moja kwa mwezi.
◼ Kichapo cha Mnara wa Mlinzi cha mara mbili kwa mwezi katika Kigeorgia kitaanza kutangazwa katika Januari 1997.