Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/97 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 1/97 uku. 3

Matangazo

◼ Toleo la fasihi la Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1984 ambacho kutaniko laweza kuwa nacho akibani kitatolewa kwa nusu bei. Vichapo ambavyo vimechapishwa kwenye karatasi isiyochakaa au kugeuka rangi havipaswi kutiwa ndani ya toleo hili lililopunguzwa bei. Makutaniko ambayo hayana ugavi wa vitabu hivyo yaweza kutoa Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya au Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani.” Februari: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

◼ Watangazaji wote waliobatizwa walioko kwenye Mkutano wa Utumishi juma la Januari 6 watapewa kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na Kadi ya Utambulishi kwa watoto wao.

◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 2, hotuba mpya ya waangalizi wa mzunguko itakuwa “Tumia Elimu Kumsifu Yehova.”

◼ Makutaniko yanapaswa kufanya mipango inayofaa ya kusherehekea Ukumbusho mwaka huu Jumapili, Machi 23, baada ya jua kushuka. Ingawa huenda hotuba ikaanza mapema, kupitishwa kwa mifano ya Ukumbusho hakupaswi kuanza mpaka jua lishuke. Ulizeni vyanzo vya kwenu ili mjue kushuka kwa jua kutakuwa saa ngapi katika eneo lenu. Kwa kuwa hakuna mikutano itakayofanywa siku hiyo isipokuwa ya utumishi wa shambani, marekebisho yanayofaa yapaswa kufanywa ili Funzo la Mnara wa Mlinzi lifanywe wakati mwingine. Waangalizi wa mzunguko watahitaji kufanya marekebisho ya ratiba ya mkutano wao wa juma kupatana na hali za kwenu. Ingawa ni jambo linalotamanisha kila kutaniko kuwa na msherehekeo wao wa Ukumbusho, huenda hili lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au zaidi yanaweza kutumia jengo jingine jioni hiyo. Ukumbusho haupaswi kuanza kwa kuchelewa mno hivi kwamba watu wapya wanaopendezwa waone ugumu wa kuhudhuria. Wala ratiba haipaswi kupangwa kwa kufuatana na nyingine mno hivi kwamba hakuna wakati wa kusalimia wageni kabla na baada ya msherehekeo, kufanya mipango ya usaidizi wa kiroho yenye kuendelea kwa wapya wenye kupendezwa, au kufurahia badilishano la ujumla la kitia-moyo. Baada ya kufikiria kikamili mambo yote, wazee wapaswa kuamua ni mipango gani itakayosaidia vizuri zaidi wale wanaohudhuria Ukumbusho ili wanufaike kikamili kutokana na pindi hiyo.

◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho itatolewa Jumapili, Aprili 6. Muhtasari utaandaliwa. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko la mzunguko au siku ya kusanyiko la pekee mwisho-juma huo yatakuwa na hotuba ya pekee juma litakalofuata. Hakuna kutaniko lipaswalo kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 6.

◼ Baraza la wazee lapaswa kujua kwamba marekebisho yafuatayo yanahitajiwa wakati makutaniko yanapohudhuria makusanyiko ya kwenu: Wakati ambapo programu ya siku ya kusanyiko la pekee imeratibiwa, kutaniko lapaswa kuwa na mikutano yote ya kawaida juma hilo, isipokuwa kwamba Mkutano wa Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi huahirishwa. Linaporatibiwa kuhudhuria kusanyiko la mzunguko, kutaniko pia litaahirisha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi; ila Funzo la Kitabu la Kutaniko litafanywa juma hilo.

◼ Vidiokaseti Mpya Zinazopatikana:

To the Ends of the Earth—Kiarabu

◼ Compact Discs Mpya Zinazopatikana:

Kingdom Melodies Volume 3 (cdm-3)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki