Sanduku La Swali
◼ Kwa nini twapaswa kuripoti utendaji wetu wa utumishi wa shambani bila kukawia kila mwezi?
Sisi sote twahisi shangwe tunaposikia kuhusu mambo mazuri yanayotimizwa katika kuhubiri ujumbe wa Ufalme. (Ona Mithali 25:25.) Matendo 2:41 yaripoti kwamba baada ya hotuba yenye kusisimua ya Petro siku ya Pentekoste, “wakaongezeka watu wapata elfu tatu.” Muda mfupi baadaye, idadi hiyo ikaongezeka hadi “kama elfu tano.” (Mdo. 4:4) Lazima iwe ripoti hizo zilikuwa zenye kuteremesha kama nini kwa Wakristo wa karne ya kwanza! Twaitikia vivyo hivyo kwa ripoti zenye kutia moyo leo. Tunasisimuka kusikia kuhusu mafanikio ambayo ndugu zetu hufurahia katika kuhubiri habari njema ulimwenguni pote.
Kwa kuwa wakati na jitihada nyingi zahusika katika kukusanya ripoti hizo, ushirikiano wa kila mtangazaji wa Ufalme ni wa muhimu. Je, wewe ni mwangalifu sana kuhusu kutoa ripoti yako bila kukawia kila mwezi?
Ripoti za maongezeko hutuletea shangwe nyingi. Kwa kuongezea, ripoti husaidia Sosaiti kuchunguza maendeleo ya kazi ya ulimwenguni pote. Maamuzi lazima yafanywe kuhusu mahali panapohitaji msaada zaidi au aina ya fasihi na kiwango kitakachotolewa. Wazee katika kila kutaniko hutumia ripoti za utumishi wa shambani kuamua ni wapi panapoweza kuboreshwa. Ripoti nzuri ni zenye kujenga, hutuhamasisha sote tuchunguze huduma yetu wenyewe ili tufanye maendeleo yawezekanayo.
Watangazaji wote wanahitaji kung’amua daraka lao wenyewe la kutoa ripoti ya utumishi wa shambani bila kukawia kila mwezi. Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanaweza kukumbusha watangazaji juu ya daraka hili, kwa kuwa wao pia wako chonjo kutoa usaidizi wa kibinafsi kwa wale ambao wana ugumu katika kushiriki katika utumishi wa shambani kwa ukawaida kila mwezi. Kikumbusha hiki chaweza kutolewa kwenye funzo la kitabu la mwisho kila juma au wakati mwingine unaofaa. Ikiwa hakuna fursa ya kutoa ripoti za utumishi wa shambani kwenye Jumba la Ufalme, kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko anaweza kuzikusanya na kuona kwamba mwandishi anapewa hizo kwa wakati ufaao ili zitiwe ndani pamoja na ripoti ya kawaida ya kila mwezi ya kutaniko kwa Sosaiti.
Bidii yetu yenye kundelea ya kuripoti kwa uaminifu utendaji wetu wa utumishi wa shambani bila kukawia hufanya mzigo uwe mwepesi kwa wale wenye madaraka kwa hali nzuri yetu ya kiroho.