Iweni wa Kawaida Katika Utumishi wa Shambani
1 Je! sisi huchukua hatua chanya ili kushiriki katika utumishi wa shambani kwa ukawaida? Je! tuna bidii-nyedelevu ya kutoa haraka ripoti yetu ya huduma ya shambani kwenye Jumba la Ufalme kila mwezi? Ni jambo ambalo kila mmoja wetu anapaswa kujitahidi kufanya, kutoruhusu mwezi upite kamwe bila kueleza hadharani imani yetu.—Rum. 10:9, 10.
2 Zaidi ya kuwa wa kawaida sisi wenyewe, tunataka kuwa chonjo kusaidia wengine washiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani. (Flp. 2:4) Twaweza kufanyaje hivyo? Tunaweza kualika wahubiri wasiobatizwa ambao ndipo wanaanza kazi ya huduma pamoja nasi. Ratiba isiyogeukageuka ya utumishi itasaidia kukaza imara kweli katika mioyo yao.
3 Iweni wa kawaida katika utumishi wa shambani. Toa ripoti yako kila mwezi kwa uaminifu. Saidia wengine washiriki katika ufumishi wa shambani kwa ukawaida. ‘Penda ndugu.’—1 Pet. 2:17.