Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/93 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 7
  • Juma Linaloanza Juni 14
  • Juma Linaloanzia Juni 21
  • Juma Linaloanza Juni 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 6/93 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Juma Linaloanza Juni 7

Wimbo 162

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Onyesha umuhimu wa kuwa na magazeti tayari ili kuyatumia kwa ushahidi wa vivi-hivi.

Dak. 15: “Saidia Wengine Wajifunze Juu ya Yule Mtu Mkuu Zaidi.” Mazungumzo ya maswali na majibu.

Dak. 20: “Shiriki Ujuzi Sahihi Juu ya Yesu Kristo.” Maswali na majibu. Toa wonyesho wa kutumia trakti kama inavyopendekezwa kwenye mafungu 2 na 4. Wakumbushe wahubiri kutoa magazeti ya karibuni mwenye nyumba asipokubali toleo.

Wimbo 205 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 14

Wimbo 196

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. na matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Dokeza mambo makuu yanayofaa kuongewa katika magazeti ya karibuni ili yatumiwe katika huduma ya shambani juma hili.

Dak. 15: Sanduku la Swali. Hotuba ikitolewa na mzee. Onyesha daraka letu la kujiendesha ifaavyo tunapohudhuria ubatizo. Tia ndani mambo yanayohusiana na hayo kutoka kwenye Sanduku la Swali la Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1991.

Dak. 20: “Sababu kwa Nini Trakti ni Zenye Thamani Katika Huduma Yetu Leo.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Baada ya fungu la mwisho, panga wonyesho mfupi kuonyesha jinsi ilivyo rahisi kutumia trakti kutoa ushaihidi wa vivi-hivi.

Wimbo 126 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanzia Juni 21

Wimbo 31

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja mambo makuu ya Ripoti ya Utumishi ya Februari. Pia taja sehemu ambayo kundi lenu lilifanya katika utumishi wa shambani mwezi huo. Tia ndani ripoti ya hesabu na usome shukrani zozote za utoaji wa hiari. Onyesha uthamini kwa tegemezo la kifedha la kundi la kwenu pamoja na ule wa kazi ya ulimwenguni pote ya Sosaiti.

Dak. 15: “Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Kitabu Mtu Mkuu Zaidi.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Baada ya fungu la 2, onyesha jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu hicho. Mhubiri aanza kwa kusoma mafungu matatu ya kwanza katika sura 111 ya kitabu hicho kisha endelea na utoaji uliopendekezwa kwenye fungu la 2 la makala hiyo.

Dak. 20: Hotuba ya Uumbaji, ikitegemea kitabu Kutoa Sababu, kurasa 397-401. Msemaji apaswa kuwa mchaguzi kwa kutumia mambo ya kutosha tu kadiri yawezavyo kuzungumzwa katika wakati aliogawiwa.

Wimbo 79 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 28

Wimbo 130

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Toa uangalifu kwenye mambo machache ya kuzungumzwa katika magazeti ya karibuni ambayo yanaweza kutumiwa katika huduma ya nyumba kwa nyumba au kwa kutoa ushahidi wa vivi-hivi.

Dak. 20: “Iweni wa Kawaida Katika Utumishi wa Shambani.” Hotuba ikitolewa na mwangalizi wa utumishi au ndugu aliye na sifa za ustahili. Pitia habari iliyo katika Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 106-10, wakati ukiruhusu. Kazia uhitaji wa wote kushiriki kwa ukawaida katika huduma na kutoa haraka ripoti ya utumishi wa shambani mwisho wa mwezi.

Dak. 15: Kufanya Mpango kwa Ajili ya Kampeni Yetu ya 19 ya Makedonia. Mwangalizi wa utumishi aeleze mipango ya kufikia maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida ya kundi na mipango ya kampeni ya maeneo yaliyo pekee. Makundi yaliyo mengi yatapokea migawo hususa ya “Makedonia.” Tumieni vizuri siku za soko na muwe na ugavi wa kutosha wa fasihi, hasa broshua za lugha mbalimbali. Kila kundi linatiwa moyo kufika mbali katika sehemu zilizotapakaa. Tia moyo kila mtu ashiriki kikamili ili kufikia sehemu ambazo ushahidi hautolewi kwa ukawaida.

Wimbo 71 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki