Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/02 uku. 8
  • Je, Wewe Hutoa Ripoti Iliyo Sahihi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Hutoa Ripoti Iliyo Sahihi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Ripoti Utumishi wa Shambani kwa Usahihi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Iweni wa Kawaida Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Msaidie Mwangalizi Wenu wa Funzo la Kitabu la Kutaniko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 12/02 uku. 8

Je, Wewe Hutoa Ripoti Iliyo Sahihi?

1 Masimulizi mengi ya Biblia hutia ndani idadi hususa, ambazo husaidia kueleza waziwazi lililotokea. Kwa mfano, Gideoni alishinda kambi ya Wamidiani akiwa na watu 300 tu. (Amu. 7:7) Malaika wa Yehova aliua askari wa Ashuru 185,000. (2 Fal. 19:35) Kwenye Pentekoste 33 W.K., watu 3,000 hivi walibatizwa, na muda mfupi baada ya hapo idadi ya wenye kuamini iliongezeka hadi watu 5,000. (Mdo. 2:41; 4:4) Ni dhahiri kwamba kulingana na masimulizi hayo watumishi wa kale wa Mungu walijitahidi sana kukusanya ripoti iliyo kamili na sahihi.

2 Leo tengenezo la Yehova hutuagiza kutoa ripoti ya utumishi wa shambani kila mwezi. Kushirikiana kwetu kwa uaminifu na mpango huo huboresha usimamizi wa kazi ya kuhubiri. Ripoti zinaweza kuonyesha sehemu moja ya huduma inayohitaji kufanyiwa kazi au kuonyesha kwamba wafanyakazi zaidi wanahitajiwa katika sehemu fulani. Katika kutaniko, ripoti za utumishi wa shambani husaidia wazee watambue wale wanaoweza kupanua huduma yao na wale ambao huenda wakahitaji msaada. Na ripoti zinazoonyesha jinsi kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme inavyoendelea zinatia moyo udugu wote wa Kikristo. Je, wewe ni mmoja wa wale ambao hutoa ripoti sahihi?

3 Daraka Lako Mwenyewe: Je, wewe hujipata mwishoni mwa kila mwezi ukisahau kile ulichofanya katika huduma? Ikiwa ndivyo, kwa nini usiandike utendaji wako kila mara unaposhiriki katika utumishi wa shambani? Wengine hutumia kalenda au kitabu cha kumbukumbu. Wengine nao hubeba karatasi ya kujazia ripoti wanapokwenda kuhubiri. Mwishoni mwa kila mwezi, mpe mwangalizi wa funzo lenu la kitabu ripoti yako bila kukawia. Au ukipenda, unaweza kuiweka ripoti yako ndani ya sanduku lililo katika Jumba la Ufalme. Ukisahau kutoa ripoti yako, mtafute mwangalizi wa funzo lenu la kitabu badala ya kumngoja aje kukutafuta. Unapotoa ripoti yako ya utumishi kwa kudhamiria, unaonyesha heshima kwa mpango wa Yehova na upendo wako kwa ndugu waliopewa mgawo wa kukusanya na kujumlisha ripoti.—Luka 16:10.

4 Daraka la Mwangalizi wa Funzo la Kitabu: Akiwa mchungaji aliye macho na mwenye kujali, mwangalizi wa funzo la kitabu hupendezwa na utendaji wa kikundi chake mwezi wote. (Mit. 27:23) Yeye anajua kama kila mhubiri anahubiri kwa ukawaida, ifaavyo, na kwa shangwe, na anatoa msaada wa haraka kwa yeyote ambaye hajahubiri mwezi mzima. Mara nyingi anahitaji tu kuwatia-moyo, kuwapa dokezo linalofaa, au kuwaalika wahubiri naye katika utumishi wa shambani.

5 Mwishoni mwa kila mwezi mwangalizi wa funzo la kitabu huhakikisha kwamba wote katika kikundi chake wametoa ripoti zao za utumishi ili mwandishi aweze kutuma ripoti sahihi kwenye ofisi ya tawi kufikia tarehe sita ya mwezi ufuatao. Mwisho wa mwezi ukaribiapo, huenda ikasaidia akiwakumbusha watu wa kikundi chake na kuwe na karatasi za ripoti mahali pa funzo la kitabu. Kama kuna watu ambao husahau kuripoti utumishi wao, anaweza kuwakumbusha na kuwatia moyo.

6 Kutoa ripoti zetu za utumishi bila kukawia husaidia kujumlisha ripoti sahihi ya kazi iliyotimizwa shambani. Je, utafanya sehemu yako kwa kutoa ripoti yako ya utumishi kila mwezi bila kukawia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki