Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Machi: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi toa magazeti yote mawili. Broshua mpya, Mungu Anataka Tufanye Nini?, yaweza kutumiwa. Juni: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kazia kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa kushiriki katika kampeni ya mwaka huu ya maeneo ya mbali kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda wanaweza kutoa maombi yao sasa kupitia baraza la wazee (au halmashauri ya utumishi) la kutaniko lao. Katika mapendekezo yazo, halmashauri za utumishi zaombwa kutoa sababu za kupendekeza painia na kueleza kama yeye ni mseja au aliyeoa au kuolewa, mwanamume au mwanamke (ana watoto wangapi, ikiwa anao) na ikiwa mwenye kuomba yuko huru kuhamia maeneo yaliyo pekee kwa kipindi cha miezi mitatu. Halmashauri za utumishi zitaelewesha wazi mambo hayo na kupeleka barua za maombi pamoja na mapendekezo yazo kwa Sosaiti kufikia Aprili 15, 1997.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu za kutaniko Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho mwaka huu itatolewa kwenye makutaniko yote Jumapili, Aprili 6. Hotuba ina kichwa “Jiepushe na Mambo ya Kilimwengu Yenye Kunajisi.” Sisi sote twapaswa kuhudhuria, na kusaidia wenye kupendezwa ambao wanakuja kwenye Ukumbusho wawepo kwenye hotuba hiyo. Tutakayosikia kwa hakika yatakuwa kichocheo cha azimio lililofanywa upya la kumpendeza Mungu.
◼ Katika kila jumuiya, nyakati tofauti-tofauti mwakani, kuna sikukuu za kilimwengu ambazo hupatia watoto ruhusa kutoka shuleni nazo hupa wakati wa pumziko kutoka kazi ya kuajiriwa. Hizo hutoa fursa bora kabisa kwa kutaniko kuongeza ushiriki katika huduma ya shambani. Wazee wanapaswa kufikiria kimbele wakati vipindi hivi vitakapotokea na kujulisha kutaniko mapema kuhusu mipango inayofanywa kutoa ushahidi wa kikundi katika vipindi vya sikukuu.