Amerika Kaskazini Kuwa Wakaribishaji wa Mikusanyiko ya Kimataifa 1998
Kama ilivyotangazwa Jumamosi, Oktoba 5, 1996, kwenye mkutano wa kila mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, Baraza Linaloongoza linapanga kuwa na mikusanyiko mwaka wa 1998. Pamoja na mikusanyiko ya kawaida ya wilaya, mikusanyiko kadhaa ya kimataifa itafanywa katika Amerika Kaskazini pamoja na Afrika, Asia, Ulaya, Amerika ya Latini, eneo la Karibea, na Pasifiki Kusini.
Mikusanyiko kadhaa kati ya hii itafanywa Amerika Kaskazini, na wajumbe kutoka ulimwenguni pote wataalikwa. Pia, twaweza kutazamia kuwa na wamishonari kwenye mikusanyiko hii. Wamishonari pamoja na wengine walio katika utumishi wa pekee kwa angalau miaka mitatu ambao wanastahili wataalikwa kuhudhuria mojawapo ya mikusanyiko hii katika au karibu na nchi za nyumbani kwao.
Habari ya ziada kuhusu tarehe, mahali, sifa za ustahili za wajumbe, na mambo mengine yahusuyo yatafuata baadaye. Kutakuwa na fursa ya idadi kidogo ya wajumbe kutoka Marekani kuhudhuria mikusanyiko katika nchi nyingine. Watangazaji wale wanaofikiria kujaza maombi ya kuchaguliwa kwa wajumbe wanaweza kuanza kuweka fedha wakitazamia matukio haya ya pekee.