Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Aprili 7
  • Juma Linaloanza Aprili 14
  • Juma Linaloanza Aprili 21
  • Juma Linaloanza Aprili 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili

Juma Linaloanza Aprili 7

Wimbo 100

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Taja mambo ya kuongea yaliyo katika magazeti ya karibuni.

Dak. 15: “Halaiki Inaongezwa.” Maswali na majibu. Pitia madokezo ya msingi yanayoshughulikiwa katika Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1993, ukurasa wa 12-17.

Dak. 18: “Saidia Wasio na Uzoefu Waelewe.” Maswali na majibu. Pitia sehemu za broshua Anataka: njia ya funzo iliyo sahili, maswali ya wakati ufaao, picha zenye kuvutia, marejezo tele ya Maandiko. Kazia mradi wa kuanzisha mafunzo ambayo hatimaye yanaongoza kwenye kitabu Ujuzi. Panga mtangazaji mwenye uwezo atoe wonyesho wa jinsi ya kuanzisha funzo akitumia mfikio unaoonyeshwa katika fungu la 4. Tia moyo wazazi wote katika kutaniko wajifunze broshua hiyo pamoja na watoto wao wachanga.

Wimbo 130 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 14

Wimbo 107

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.”

Dak. 15: “Kuelekeza Wanafunzi Kwenye Tengenezo Linalomaanishwa na Jina Letu.” (Mafungu ya 1-6) Maswali na majibu. Soma mafungu ya 5-6 na maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa. Simulia mambo yaliyoonwa kwenu juu ya itikio la wanafunzi wa Biblia la kuona ile vidio Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name au kuhudhuria mkutano wao wa kwanza kwenye Jumba la Ufalme.

Dak. 20: “Fundisha Wengine Yale Ambayo Mungu Anataka.” Mazungumzo na wasikilizaji ya mafungu ya 1-4. Panga utoaji mbalimbali katika fungu la 5 uonyeshwe, ukitumia vikao vinne tofauti-tofauti—barabarani, kwenye nyumba, mahali pa biashara, na kwenye bustani. Kumbusha wote wachukue broshua na magazeti kwa ajili ya utumishi wa shambani kabla ya kuondoka kwenye Jumba la Ufalme.

Wimbo 126 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 21

Wimbo 113

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Eleza kwamba si kuchelewa mno kuleta ombi la painia-msaidizi katika Mei. Pitia Sanduku la Swali, na julisha kutaniko kama vitabu fulani vyahitajiwa ili kujaza maktaba ya Jumba la Ufalme.

Dak. 15: “Kuelekeza Wanafunzi Kwenye Tengenezo Linalomaanishwa na Jina Letu.” (Mafungu ya 7-14) Maswali na majibu. Panga mwalimu mwenye uwezo atoe wonyesho wa jinsi ya kuwa na mazungumzo ya moyo mweupe pamoja na mwanafunzi juu ya uhitaji wa kuhudhuria mikutano.

Dak. 15: Kutumia Kikamili Fasihi Yetu. Hotuba itolewe na mzee. (Ona Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1995, kurasa za 3-5.) Ripoti zaonyesha kwamba makutaniko mara nyingi huagiza magazeti mengi zaidi kuliko vile wanavyoyagawanya kila mwezi. Yapata asilimia 50 hayaripotiwi kamwe kuwa yameangushwa. (Onyesha takwimu zaonyesha nini kwenu.) Ni nini huyapata magazeti haya? Mengi hudumu kwenye rafu au hutupwa. Jambo hili laweza kuepukwaje? Kila mtangazaji apaswa kukadiria kwa uangalifu mahitaji yake na aagize tu yale anayoweza kuangusha. Fanya liwe zoea la kuwatolea magazeti wote tunaokutana nao. Tumieni matoleo ya zamani. Shiriki katika utumishi wa magazeti angalau mara moja kila juma, ama Jumamosi ama siku ya soko.

Wimbo 128 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 28

Wimbo 121

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote walete ripoti zao za utumishi wa shambani za Aprili. Tangaza majina ya wale watakaofanya upainia msaidizi katika Mei. Onyesha mipango mingine ya ziada inayofanywa kwenu kwa ajili ya mikutano ya shambani. Wakati wa Mei jitihada ya pekee yapasa kufanywa ya kufuatia maangusho ya broshua kukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo. Dokeza kifupi njia tunazoweza kuomba kwa busara jina na anwani ya watu tunaowatolea ushahidi wa vivi hivi. Unaweza kumpa jina na anwani yako kwanza nawe uulize wanakoweza kufikiwa. Alika wasikilizaji watoe madokezo mengine ambayo yamekuwa na matokeo kwao.

Dak. 15: “Kwa Nini Wao Hufanya Hivyo?” Mzee azungumzia makala pamoja na mapainia wa kawaida wawili au watatu. (Ikiwa hawapatikani, tumia wale ambao hujiandikisha mara nyingi wakiwa mapainia-wasaidizi.) Tia ndani mambo makuu kutoka makala “Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka,” katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1994. Panga kila mmoja wao aeleze kwa nini amechukua utumishi wa painia. Waombe wasimulie mambo yaliyoonwa kuonyesha jinsi ambavyo wamebarikiwa kwa kufanya hivyo.

Dak. 15: “Msaada Katika Wakati Ufaao.” Maswali na majibu. Onyesha mambo makuu yenye thamani kutoka katika kila ya vichapo vipya.

Wimbo 129 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki