Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi toa magazeti yote mawili. Broshua mpya, Mungu Anataka Tufanye Nini?, yaweza kutumiwa. Juni: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kazia kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zenye kurasa 32 zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je, Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, na Serikali Itakayoleta Paradiso.
◼ Kama ilivyoonyeshwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1996 tunayo akibani hapa kwenye ofisi ya tawi mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kuanzia mwaka wa 1951 hadi 1959 (ya Kiingereza.) Mabuku haya yapaswa kuwa katika maktaba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya kila kutaniko na vilevile katika maktaba yetu ya kibinafsi. Makutaniko yapaswa kutuma maagizo ya vifaa hivi vya kuagizwa kipekee.
◼ Kwa kuongezea 1951-1959 iliyo juu, tuna mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya miaka mingine, na vilevile disketi mbalimbali zilizo na utafiti wa programu za kompyuta. Wowote wanaohitaji vifaa hivi wanapaswa kutoa maagizo yao kupitia kutaniko.
◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kutuma maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haijazi maagizo ya watangazaji mmoja-mmoja ya fasihi. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga tangazo lifanywe kila mwezi kabla agizo la kila mwezi la fasihi la kutaniko halijatumwa kwa Sosaiti ili wote wenye kupendezwa kupata fasihi ya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani vilivyo vifaa vya kuagizwa kipekee.
◼ Compact Discs Mpya Zinazopatikana:
Kingdom Melodies Buku la 4 (cdm-4)