Onyesha Hangaiko la Kweli Katika Kupendezwa Kote Kunakopatikana
1 Upigaji-mbiu wa Ufalme ulimwenguni pote karibuni utafikia mwisho, ambapo wale wote “wasiomjua Mungu” wataharibiwa. (2 The. 1:7-9) Hivyo, hangaiko la kweli kwa maisha ya wengine lasukuma watu wa Yehova wafikie watu wengi iwezekanavyo wakiwa na ujumbe wa Ufalme.—Sef. 2:3.
2 Kila mwezi, mamilioni ya saa hutumiwa katika kutafuta wale wanaotaka kusikia “habari njema ya mambo mema.” (Isa. 52:7) Kwa kuitikia toleo la fasihi la karibuni, wengi wamekubali Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Hangaiko la kweli kwa watu hawa lapaswa kutuchochea tujitahidi kusitawisha kupendezwa kote kunakopatikana.—Mit. 3:27.
3 Andika Maandishi Yaliyo Sahihi: Mengi yatatimizwa ukiandika kikamili na kwa usahihi habari ya wenye kupendezwa na ya maangusho. Habari kama vile jina na anwani ya mwenye nyumba, siku na wakati ulipomtembelea, fasihi iliyoangushwa, na somo lililozungumziwa itakusaidia uwe mwenye matokeo zaidi unaporudi. Pia, ukiandika maelezo fulani yaliyotolewa na mwenye nyumba katika mazungumzo yenu ya kwanza, huenda ukaweza kuyarejezea kwa matokeo unaporudia mazungumzo kwenye ziara ya kurudia.
4 Usikawie Kufanya Ziara za Kurudia: Ni wangapi kati ya wale waliokubali fasihi kutoka kwako mwezi uliopita ambao umejaribu kuwatembelea tena? Je, majuma kadhaa yamepita kabla hujawafikia? Hangaiko la kweli kwa hali njema yao idumuyo milele yapaswa kukuchochea urudi upesi iwezekanavyo, hasa kwa muda wa siku chache, ili mazungumzo yawe bado yamo akilini. Kwa kurudi bila kukawia ili kuendeleza kupendezwa kwao, huenda ukaweza kuzuia jitihada za Shetani kabla ‘hajaja na kuliondoa neno lililopandwa ndani yao.’—Mr. 4:15.
5 Matayarisho Ni Muhimu: Matokeo yako katika kufanya ziara za kurudia yanategemea hasa jinsi unavyotayarisha. Panga mfikio wako kabla ya kwenda. Ukurasa wa mwisho wa Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1997 waandaa utoaji mbalimbali ambao waweza kutumiwa kwa mafanikio mazuri unapotoa andikisho au broshua Anataka. Jambo lifuatalo ni kuwa na mawazo kadhaa akilini ya kushiriki unaporudi. Ni nini kiwezacho kusemwa unapojitahidi kusitawisha kupendezwa? Funzo la Biblia laweza kuanzishwaje?
6 Unapositawisha mazungumzo juu ya kile kihitajiwacho kufanywa ili kusafisha dunia na kuifanya mahali pazuri zaidi pa kuishi, unaweza kusema hivi:
◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tulikubaliana kwamba hatua kubwa zahitajiwa kabla ya dunia kufanywa kuwa paradiso yenye amani. Je, wafikiri wanadamu wana kile wanachohitaji kutimiza kazi hii? [Ruhusu itikio.] Tafadhali ona ni kwa nini itakuwa lazima Mungu aingilie mambo ya mwanadamu.” Soma Zaburi 37:38. Kisha fungua somo la 5 katika broshua Anataka, na utumie sehemu zilizochaguliwa za fungu la 4-5 kuonyesha jinsi Mungu atakavyotimiza unabii huu. Endelea kwa kumtolea funzo la Biblia kwa kutumia hiyo broshua.
7 Ikiwa mlizungumzia Ufalme wa Mungu na ukaangusha broshua “Anataka” kwenye ziara ya kwanza, unaporudi unaweza kusema jambo kama hili:
◼ “Tulipoongea wakati uliopita, tulitambulisha Ufalme wa Mungu kuwa serikali halisi itakayotawala dunia yote. Biblia huonyesha kwamba Kristo Yesu atakuwa mtawala wayo. Je, waweza kuona manufaa zozote za kuwa na serikali na kiongozi wa aina hii?” Ruhusu itikio. Fungua broshua Anataka kwenye somo la 6. Ukitumia mambo yaliyochaguliwa katika fungu la 6-7 na picha kwenye ukurasa wa 13, onyesha kile ambacho Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu wakati ujao. Soma Danieli 2:44, na ikifaa, toa kitabu Ujuzi na funzo la Biblia.
8 Ukipata mtu aliyekubali kwamba dini za ulimwengu zimesababisha matatizo kwa jamii ya binadamu, unaweza kuuliza hivi kwenye ziara ya kurudia:
◼ “Je, umepata kujiuliza jinsi tunavyoweza kujua dini iliyo na kibali cha Mungu? [Ruhusu itikio.] Broshua hii Mungu Anataka Tufanye Nini? hutoa ishara za kutambulisha dini ya kweli.” Fungua somo la 13, na ukazie mambo matano ya herufi mlazo za italiki katika fungu la 3-7. Unaweza kuendelea kwa kusema: “Kwa kuongezea kupata dini ya kweli, lazima tujue yale ambayo Mungu anataka sisi watu mmoja-mmoja tufanye.” Soma na uzungumzie Yohana 4:23, 24. Fungua somo la 1 katika broshua hiyo, na uonyeshe jinsi tunavyojifunza.
9 Unaporudi kuendeleza mazungumzo kuhusu furaha ya familia, unaweza kusema jambo kama lifuatalo:
◼ “Tulipokutana mara ya kwanza, nilishiriki nawe siri ya kupata furaha ya familia, ambayo ni kutumia shauri lipatikanalo katika Neno la Mungu, Biblia. Kwa habari ya kushughulikia mahitaji ya familia ya kisasa, unaamini kwamba Biblia ni ya kikale au yafaa hali za wakati wa sasa?” Ruhusu itikio. Toa kitabu Ujuzi. Fungua sura ya 2, na usome nukuu lililo katika fungu la 13. Ukitumia mambo yaliyo katika fungu la 3, fanya toleo la funzo la Biblia la familia.
10 Broshua Anataka imethibitika kuwa msaada mzuri katika kusaidia wengine wajifunze matakwa ya Mungu. Ufupi na uwazi wa ujumbe wayo, na usahili na uzuri wa utaratibu wayo, huifanya iwe rahisi kuanzisha na kuongoza mafunzo. Upesi iwezekanavyo, ikitegemea kupendezwa na uwezo wa mwanafunzi, funzo laweza kuhamishwa kwenye kitabu Ujuzi. Mpito mzuri unaweza kutia ndani kutumia Yohana 17:3 kueleza uhitaji wa kutwaa ujuzi wenye maendeleo juu ya Mungu, ambao kitabu hicho kitauandaa.
11 Acheni tutumie kwa manufaa kila fursa kuonyesha hangaiko la kweli kwa wote wenye kupendezwa tunaopata katika eneo letu tunalotolea ushahidi. Kwa kuandika maandishi sahihi, kufanya matayarisho, na kurudi bila kukawia ili kuongezea kupendezwa kwao, twaweza kuonyesha aina ya upendo wa jirani ambao utawavutia kuelekea njia ya wokovu.—Mt. 22:39; Gal. 6:10.