Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zenye kurasa 32 zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je, Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?, na Serikali Itakayoleta Paradiso. Septemba: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Oktoba: Toa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi toa nakala mojamoja za magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Kuanzia sehemu ya mwisho ya mwezi huu, trakti Habari za Ufalme Na. 35 itagawanywa.
◼ Ukiwa na miisho-juma kamili mitano, mwezi wa Agosti waweza kuwa wakati unaofaa wengi kufanya upainia-msaidizi.
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Itumaini Nguvu ya Yehova Yenye Kuokoa.”
◼ Likiwa kikumbusha, orodha ya fasihi ya kila mwaka haitakiwi tena Septemba 1 kila mwaka. Habari hii itatakiwa Januari 1 kila mwaka. Hivyo, fomu ya Orodha ya Fasihi S-AB-18-SW, itapelekwa kwa makutaniko mwezi wa Novemba.
◼ Broshua Mapokeo haiko akibani na haichapwi. Agizo lolote la kutaniko linalongojea litafutwa.