“Ni Nani Atakayekwenda kwa Ajili Yetu?”
Swali hili lilipotokezwa na Yehova, Isaya aliitikia haraka: “Mimi hapa, nitume mimi.” (Isa. 6:8) Kwa sababu mavuno ni mengi leo, mwito huohuo watolewa sasa. Wafanyakazi zaidi wa wakati wote—mapainia wa kawaida—wanahitajiwa kwa uharaka! (Mt. 9:37) Je, uko tayari kujitolea? Ikiwa ndivyo, Septemba 1, mwanzo wa mwaka wa utumishi wa 1998, ungekuwa wakati mzuri wa kujiandikisha uwe painia. Kwa nini usiombe wazee upate fomu ya ombi?