Habari Za Kitheokrasi
Kuwekwa Wakfu kwa Majengo Mapya ya Ofisi ya Tawi: Katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1997 tulijulishwa kwamba kazi ya ujenzi kwenye ofisi ya tawi yetu mpya inakaribia kumalizika. Kufikia wakati mtakapopokea toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu twatumaini kwamba wengine tayari wameanza kuhamia kwenye majengo mapya. Hivyo, wengi wanajiuliza kuhusu programu ya kuwekwa wakfu. Kama ilivyotajwa katika barua yetu ya Aprili 14, 1997, wale waliobatizwa 1975 au mapema zaidi ya hapo wataalikwa kwenye programu ya kuwekwa wakfu Oktoba 25, 1997. Lakini vipi wengine wote? Programu ya pekee imepangwa kufanywa Jumapili, Oktoba 26, 1997, Jamhuri Park, ambapo wote wanaotaka wanaweza kuhudhuria. Programu hiyo itakazia mambo makuu kutoka katika programu ya kuwekwa wakfu ya siku iliyotangulia. Ndugu Henschel, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, atakuwepo naye atatoa hotuba kuu. Ndugu na dada wengine ambao wamekuwa wakitumikia katika Afrika Mashariki pia watakuwepo.
Kwa hiyo, twawaalika nyinyi nyote mlio na fursa mhudhurie programu hii. Hakutakuwa na mipango ya kutalii Betheli mpya Jumamosi, Oktoba 25, isipokuwa mtu awe ana mwaliko wa pekee. Ndugu na dada wengine wote wanatiwa moyo waje watalii makao mapya kuanzia Jumatatu, Oktoba 27, na kuendelea.
Limekuwa jambo lenye kufurahisha kuona baraka za Yehova katika kazi ya ujenzi wa ofisi ya tawi mpya na twatazamia mbele kwa hamu kuwa pamoja kwa ajili ya programu ya pekee Jumapili, Oktoba 26, 1997. Mambo zaidi kuhusu wakati na mipango mingine yatawasilishwa kwenu kwa wakati ufaao.
Ripoti ya Utumishi ya Machi: TULIFAULU! Mradi wetu wa mapainia-wasaidizi 2,500 tayari ulifikiwa katika mwezi wa Machi. Jumla kubwa ya mapainia-wasaidizi 3,497 walishiriki katika kazi ya upainia-msaidizi katika Afrika Mashariki mwezi wa Machi. Hongera, akina ndugu na dada! Sasa twatazamia kwa hamu nyingi matokeo ya kampeni inayobaki ya mwezi wa Aprili na Mei. Hakuna shaka kwamba utendaji huu ulioongezwa utaleta baraka nyingi zaidi miezi inayokuja.