Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 12/15 kur. 16-20
  • Wanahitajiwa kwa Haraka—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wanahitajiwa kwa Haraka—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwatokea Mavuno Makubwa
  • Uharaka Mkubwa Zaidi Leo
  • Sasa Maelfu Wanaitikia
  • Imani Inaondoa “Milima”
  • Iweni Wavunaji Wenye Furaha!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Endeleeni Katika Kazi ya Kuvuna!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Shiriki Kwa Furaha Pamoja Na Yesu Kristo Katika Kazi ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 12/15 kur. 16-20

Wanahitajiwa kwa Haraka​—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!

“Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake”​—LUKA 10:2.

1. Huenda wewe ukawazaje juu ya maneno ya Yesu katika Luka 10:2, lakini ungearifiwa vema kufanya nini?

UNAPOYASOMA maneno hayo ya Yesu, je, unajisikia kwamba yanakuhusu wewe pia? Kwa kuwa yalinenwa zaidi ya karne 19 zilizopita, huenda ukaelekea kuwaza kwamba hayana maana tena. Kukata shauri haraka haraka hivyo kungekuwa kosa. Ili kuuona uzito kamili wa maneno hayo ya Yesu, acheni tutazame nyuma tuone ni jambo gani lililotokea wakati yaliposemwa mara ya kwanza, kisha tuchunguze hali yetu wenyewe leo.​—Linganisha 1 Wakorintho 10:11.

2. Ni hali gani iliyomtaka sana Yesu achukue hatua ya haraka mwaka 32 W.K., naye aliikabili namna gani?

2 Mwaka 32 W.K., Sikukuu ya Vibanda ilipokuwa imepita, ni miezi sita tu iliyobaki kabla Yesu hajakabili kifo akiwa juu ya mti wa mateso. Ili asaidie kuharakisha mwendo wa kazi ya kuhubiri, Yesu alituma wanafunzi 70 wakiwa “wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe. Wakaenda na maneno ya Yesu yakiwa yanalia masikioni mwao hivi: “Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”​—Luka 10:1, 2.

Kwatokea Mavuno Makubwa

3. Eleza mengine ya matokeo yaliyotokana na kuzidisha mahubiri wakati wa miezi michache ya mwisho wa huduma ya Yesu.’

3 Yalikuwa ni matokeo gani ya jitihada hiyo ya kuhubiri iliyoongezwa? Tunasoma hivi: “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.” Huo ulikuwa wonyesho mzuri kama nini wa uwezo wa Mungu juu ya mashetani! Hakika hiyo ripoti ya utumishi iliyo nzuri ilimsisimua Yesu, kwa maana alisema: “Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.” (Luka 10:17, 18) Yesu alijua kwamba hatimaye Shetani na mashetani wake wangetupwa nje ya mbingu baada ya kuzaliwa kwa Ufalme wa Kimasihi katika mbingu. Lakini Yesu alipokuwa angali duniani, mtupo huo wa mashetani wasioonekana na wanadamu duni ulimpa yeye uhakikisho zaidi juu ya tukio hilo linalokuja lenye furaha. Basi Yesu alinena juu ya anguko hilo la wakati ujao la Shetani kutoka mbinguni kuwa uhakika.​—Ufunuo 12:5, 7-10.

4. Ni nini lililokuwa kusudi la kazi ya mavuno iliyofanywa na Yesu na wanafunzi wake kabla ya Nisani 14, 33 W.K.?

4 Mavuno aliyoyanena Yesu hayakuwa ya nafaka wala matunda bali ya watu, watu wenye mfano wa kondoo ambao wangeitikia ujumbe wa Ufalme bila kusitasita. Tayari matunda ya mavuno hayo yalikuwa yakidhihirika. Lakini, ‘uvunaji’ uliofanywa na Yesu na wafuasi wake katika miezi hiyo michache iliyobaki kabla ya Nisani 14, 33 W.K., ulikuwa wa kuweka msingi tu wa mavuno makubwa zaidi ambayo yangefanywa baada ya kufa na kufufuliwa kwa Yesu.​—Linganisha Zaburi 126:1, 2, 5, 6.

5. Ni matukio gani ya kusisimua yaliyotukia Pentekoste, 33 W.K., nayo yalikuwa na matokeo gani juu ya kazi ya mavuno ambayo ingefuata?

5 Sasa ilifika siku ya Pentekoste, 33 W.K. Karibu watu 120 walio wafuasi wa Yesu walikuwa wamekutana pamoja katika Yerusalemu. “Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. . . . Wote wakajazwa [roho takatifu], wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama [roho ilivyowajalia] kutamka.” Huo ndio uliokuwa mwanzo wa mavuno makubwa ajabu! “Siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.” (Matendo 1:15; 2:1, 4, 41) “Siku baada ya siku wakawa katika hudhurio la daima hekaluni wakiwa na upatano mmoja, . . . wakisifu Mungu na kupata upendeleo wa watu wote. Wakati ule ule Yehova aliendelea kila siku kuwaunga wawe pamoja nao wale wenye kuokolewa.” (Matendo 2:46, 47, NW) Baadaye tunakuta hivi: “Walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake.” Baadaye tena: “Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.”​—Matendo 5:14; 6:7.

6. Upinzani kwa kazi ya kuhubiri ulikuwa na matokeo gani juu ya matunda ya Ufalme?

6 Sasa upinzani ukaongezeka sana kwa ujumbe wa Ufalme. Je, kazi ya mavuno ilipungua mwendo kwa sababu ya upinzani? Hapana, kwa maana “wale waliokuwa wametawanywa walipita katika nchi wakizitangaza habari njema za lile neno.” Filipo alienda mji wa Samaria, makutano ya watu wakamsikiliza kwa hamu nyingi; waliopagawa na mashetani, waliopooza, na hata viwete waliponywa. Si ajabu kwamba “ilitokea furaha kubwa sana katika mji huo.”​—Matendo 8:1-8, NW.

7. Amri ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake katika Matendo 1:8 ilitekelezwaje mwishowe?

7 Yesu aliyefufuliwa alikuwa amewaambia wanafunzi wake hivi: “Mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Yudea yote na katika Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8, NW) Ukubwa wa shamba la utendaji ulifanya wafanya kazi zaidi wahitajiwe​—kwa haraka! Lo, sasa ni mavuno makubwa kama nini ya wanafunzi yaliyotazamiwa! Na tayari yalikuwa yakifanyika​—chini ya uongozi wa roho takatifu ya Mungu. Baada ya kuongolewa kwa Sauli mwenye fikira za uuaji, tunapewa masimulizi haya: “Basi kanisa likapata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha [Yehova], na faraja ya [roho takatifu].” (Matendo 9:31) Uvunaji wa watu wenye mfano wa kondoo ulipoendelea kupata nguvu, bila shaka wanafunzi hao wa kwanza-kwanza waliyakumbuka daima maneno ya Yesu: “Mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.” Je, Yehova, “Bwana wa mavuno,” aliijibu sala hiyo? Kweli kweli! Au sivyo, ingaliwezaje kuandikwa hivi: “Tumaini la habari njema zile mlizozisikia [lilihubiriwa] katika uumbaji wote ulio chini ya mbingu”?​—Wakolosai 1:23, NW.

Uharaka Mkubwa Zaidi Leo

8. Ni kwa sababu gani katika miaka ya 1980 uhitaji wa wafanya kazi wa Ufalme ni mkubwa zaidi ya nyakati zote zilizotangulia?

8 Leo, katika miaka ya 1980, uhitaji wa wafanya kazi zaidi wa mavuno ya Ufalme ni mkubwa kuliko nyakati zote zilizotangulia. Kwa sababu gani? Kwa sababu mweneo wa shamba la ulimwengu ni mkubwa zaidi. Matokeo yake ni kwamba, mazao yanayotazamiwa kuvunwa na kukusanywa ni mengi zaidi sana. Jambo hilo linapatana na alilotabiri Yesu. Alisema kwamba wafuasi wake wangefanya kazi kubwa kuliko zile ambazo yeye alifanya duniani, kwa kuzihubiri habari njema.​—Yohana 14:12.

9. (a) Uharaka wa kazi ya kuhubiri leo unakaziwaje katika njozi ya Yohana inayosimuliwa katika Ufunuo 7:1-3? (b) Ni shauri gani la maana linaloweza kukatwa kutokana na maneno haya, “malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo” katika Ufunuo 14:4?

9 Uharaka uliopo katika kazi ya kuhubiri leo unaonyeshwa waziwazi katika hali ya kutazamisha inayosimuliwa katika njozi aliyopewa Yohana kama ilivyoandikwa katika Ufunuo sura ya 7:1-3. Humo, ‘malaika wanne waliosimama katika pembe nne za dunia’ wanaonwa “wakishika pepo nne za dunia ili upepo usivume hata kidogo.” Wataendelea mpaka wakati gani kushika “pepo nne” hizo? Ni mpaka tu ‘watumishi wa Mungu wetu watakapokwisha kupigwa muhuri katika paji la uso.’ Jambo hilo litachukua muda gani? Kionyesho fulani kinatolewa na uhakika wa kwamba kwenye sherehe ya Ukumbusho katika Aprili 15, 1984, ni watu 9,081 tu waliodai kuwa washiriki wa wale 144,000. Leo wapakwa mafuta ndio washiriki wa mwisho wa wale wanaosimuliwa katika Ufunuo 14:4 kuwa “wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.” Kwa hiyo ingeonekana kwamba mengi ya “malimbuko” hayo yamekwisha kukusanywa yakaletwa ndani. Lakini je, neno “malimbuko” (“matunda ya kwanza,” NW) linamaanisha kwamba kuna matunda mengine yatakayofuata? Bila shaka! Jambo hilo lilifananishwa vizuri na mazao tele ya matunda mengine yaliyokusanywa mwishoni mwa mwaka wa ukulima wa Kiyahudi wakati wa Sikukuu ya Vibanda.​—Kumbukumbu la Torati 16:13-15.

10. Ni mavuno gani mawili yamekuwa yakiendelea katika nyakati za kisasa, na jambo hilo linakaziaje uhitaji wa haraka wa wafanya kazi zaidi wa mavuno?

10 Basi inakuwa wazi kwamba, kuvunwa kwa mabaki wapakwa-mafuta kulipokuwa kukikaribia kumalizika, mkusanyo mwingine wa mavuno ulikaribia kuanza. Je, jambo hilo halionyeshwi na lile ambalo Yohana aliona katika njozi baada ya hapo? “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha.” Yohana aliambiwa: “Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu.” (Ufunuo 7:9, 14) Ni wakati mchache tu uliobaki wa kumaliza ukusanyaji wa “mkutano mkubwa.” Zile “pepo nne za dunia” zikiisha kuachiliwa, na hivyo zionyeshe mwanzo wa “dhiki kubwa,” itakuwa ni kuchelewa mno! Je, basi wewe huoni kwamba kuna uhitaji wa haraka wa wavunaji zaidi ili walete ndani umati wa watu ambao bado watapatikana?

Sasa Maelfu Wanaitikia

11. (a) Ni kwa kadiri gani “kondoo wengine” wa Yesu wanayashiriki mavuno? (b) Ni nini linaloonyeshwa na hudhurio la Ukumbusho wa mwaka 1984?

11 Yesu alitabiri mpanuko huo wa kazi ya kuvuna watu wenye mfano wa kondoo aliposema: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.” (Yohana 10:14, 16) Tayari kuna zaidi ya 2,800,000 wa hao “kondoo wengine” ambao wamejitambulisha kwa bidii kuwa ni wa lile “kundi moja.” Kati ya hesabu hiyo walikuwako 179,321 waliobatizwa katika mwaka wa utumishi wa 1984! Hata hivyo, hudhurio kwenye sherehe ya Ukumbusho lilikuwa 7,416,974. Jambo hilo linatuambia nini? Kwamba kuna wengine wengi ambao wameisikia sauti ya Mchungaji lakini, kwa sababu fulani, mpaka sasa hawajauitikia ule mwaliko wenye uchangamfu, “Uwe mfuasi wangu.”​—Luka 5:27, NW.

12. Ni maulizo gani ya maana yanayotupasa tujiulize wenyewe sasa?

12 Wewe una msimamo gani kuhusiana na kazi hii ya maana sana ya uvunaji katika ‘umalizio wa mfumo huu wa mambo’? (Mathayo 13:39, NW) Je, wewe umehesabiwa kati ya misongamano ya watu ambao sasa wanashiriki furaha za mavuno? Au ungali mtazamaji, ukiwa na akili inayoelekea kujiondoa usiukubali waziwazi mwaliko huu wa Mchungaji Mwema: J‘Uwe mfuasi wangu”? Hakika hakuna mtu leo angetaka kutoa udhuru wa namna mbalimbali kama wale watu watatu katika Luka sura ya 9, waliozungumzwa katika makala yetu iliyotangulia. Fikiria mambo waliyoyakosa watu hao watatu​—furaha ya utumishi wa Ufalme, labda kutia ndani pia sehemu ya kushiriki kuwafungua wengine wa wale waliokuwa wamepagawa na mashetani!—Luka 9:57-62; 10:17.

13. Imani inatusaidiaje sana kuwa wafanya kazi wa mavuno wenye moyo wa kupenda?

13 Mtume Paulo alisema: “Pasipo imani haiwezekani kumpendeza [Mungu] vema.” (Waebrania 11:6, NW) Oh, ndiyo, imani inahitajiwa kwa upande wa kila mmoja ili aweze kuweka kando mapendezi yake mwenyewe na kuyaweka wakfu maisha yake kwa moyo wa kupenda ili awe mfanya kazi wa mavuno. Kwa mfano, huenda ikawa kwamba wewe una tatizo kubwa la afya; labda washiriki fulani wa jamaa yako wanawapinga vikali Mashahidi wa Yehova; huenda ikawa unajisikia u mzee mno usiweze kufanya maishani mwako mabadiliko yanayohitajiwa; kwa upande mwingine, huenda ukawa unajifikiria huwezi kuvumilia mkazo unaokupata kutokana na vijana wa rika lako shuleni. Hata hali zako ziweje, usisahau kamwe kwamba Yehova anayafahamu matatizo yako vizuri kuliko mtu mwingineye yote. Pia, yeye yuko tayari kukukaribia wewe na kulitia nguvu azimio lako la kumtumikia ikiwa tu utachukua hatua fulani za lazima wewe mwenyewe.​—Zaburi 103:3, 14; Yakobo 4:8.

Imani Inaondoa “Milima”

14. Eleza Yesu alikuwa na maana gani kwa maneno yaliyoandikwa katika Mathayo 17:20.

14 Yesu alisema: “Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.” Ndivyo wameona wengi wa yale mamia ya maelfu ambao wameuitikia mwito wa kwamba wavunaji zaidi wajitokeze wakati wa hii miaka ya 1980. Matatizo na magumu ya kibinafsi yaliyoonekana wakati mmoja kuwa ‘milima’ kwao yameshindwa kwa msaada wa Yehova. (Mathayo 17:20; 19:26) Fikiria mambo haya yaliyoonwa:

15, 16. Simulia jinsi mwanamume kijana katika United States na mume mmoja Mkatoliki katika Brazili walivyoshinda matatizo makubwa yaliyokuwa yakiwazuia wasibatizwe.

15 Mwanamume kijana katika Kalifornia, U.S.A., alikuwa mwenye ugonjwa wa polio, akawa hawezi sana, na sikitisho ni kwamba jamaa yake ilimwachilia. Ndipo mmoja wa Mashahidi wa Yehova mwenye kwenda nyumba kwa nyumba alipompata. Funzo la Biblia likaanzishwa. Lakini yeye alikuwa mwenye haya sana hivi kwamba, Shahidi alipofika kuliongoza funzo, mtu huyo alikuwa akisukuma kigari chake cha kukalia kwenye pembe ya nyumba kisha angeelekeza uso wake ukutani usije ukaonekana. Miezi mingi ilipita ndipo mwanamume huyo kijana akaweza kushinda mengine ya matatizo yake. Lakini, aliyashinda na sasa ni Shahidi mwenye furaha, aliyebatizwa.

16 Mume na mke Wakatoliki katika Brazili hawakuridhishwa na dini yao na mwishowe wakaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Walijisikia kwamba mahitaji yao ya kiroho yalikuwa sasa yakitoshelezwa, lakini kulikuwako tatizo kubwa kama mlima: Mume mwenyewe, Antonio, alikuwa mtu aliyekolewa na uvutaji sigareti. Alikuwa amevuta kwa miaka 48, tangu alipokuwa na umri wa miaka saba! Muda wa miaka yote alikuwa amejaribu kulivunja zoea hilo, lakini wapi. Lakini, safari hii mambo yalikuwa tofauti, kama Antonio anavyosimulia: “Sasa nikajua kwamba ikiwa nilitaka kumpendeza Mungu na kujiweka wakfu nifanye mapenzi yake, ningelazimika kuacha. Baada ya kusali sana, mwishowe niliweza kuacha.” Alifurahi kama nini kuweza kuonyesha wakfu wake kwa Yehova kwa kubatizwa katika maji.​—Zaburi 66:19; Marko 11:24.

17. (a) Ni mavutano gani maovu aliyokabili Yesu na wanafunzi wake yaliyo na nguvu nyingi kuliko wakati wo wote uliotangulia? (b) Kupagawa na mashetani kulishughulikiwaje na Yesu na wanafunzi wake katika karne ya kwanza, na kunashughulikiwaje sasa?

17 Yesu na wanafunzi wake waliendelea kulikabili tatizo la kwamba Wayahudi walikuwa wamepagawa na mashetani. Nguvu izo hizo mbovu zinafanya kazi leo, hasa wakati wa sasa ambao Shetani na majeshi yake ya kishetani wamekwisha kuvurumishwa watoke nje ya mbingu mpaka kwenye dunia hii. (Ufunuo 12:7-9, 12, 17) Tofauti na vile ilivyokuwa wakati Ukristo ulipokuwa mchanga, Yehova hakuwapa watu wake leo miujiza ya kutupa mashetani nje. Lakini, silaha za kiroho ambazo amewapa Wakristo zinaweza kuwa ulinzi wa kujikinga na mavutano ya kishetani, na zinaweza pia kutumiwa zifungue wengine katika uongozi kishetani. (Waefeso 6:10-18) Kutoka Ghana inakuja ripoti hii: “Kupitia jitihada nyingi sana za akina ndugu, watu wengi wanafunguliwa katika nguvu ya mashetani.” Shahidi mmoja alikuta mwanamke hudumani, na mara tu mazungumzo ya Biblia yalipoanza, “mwanamke huyo akaanza kulia.” Tatizo lilikuwa nini? Shahidi alisimulia hivi: ‘Roho fulani alikuwa akimpagaa, naye alipofanya hivyo, alimfanya mwanamke huyo alie, kisha pesa zo zote alizokuwa nazo mfukoni zilitoweka.’ Funzo la Biblia la kawaida lilisaidia mwanamke huyo kuwa huru na mnyanyaso huo wa kishetani, likamwezesha kujiweka wakfu kwa Yehova.​—Yohana 8:32.

18. Ni jambo gani lililoonwa linaloonyesha jinsi malaika wanavyofanya kazi kwa bidii wakielekeza kazi ya kuhubiri?

18 Matatizo kama hayo yaliyotangulia kuelezwa huenda yakaja kuonekana akilini mwa mtu kuwa makubwa sana hata afikirie kujiua. Chukua kisa cha mwanamke kijana katika New Zealand. Shahidi aliyemtembelea mara ya kwanza aliona kwamba mwanamke huyo ‘alikuwa na mambo mazito moyoni na kwa wazi alisumbuliwa sana na jambo fulani.’ Baadaye mtu huyo alikiri kwamba “alikuwa amekuwa akienda akajiue kisha akaamua kutolea Mungu sala kwanza ili kumwomba msaada.” Hapo ndipo Shahidi alipopiga hodi mlango wake, kwa hiyo mwanamke huyo ‘akashukuru Mungu kweli kweli kwa kujibu sala yake.’ Je, hayo yalijitokeza sawia yenyewe tu? Basi ni kwa sababu gani mambo ya namna hiyo yanatokea mara nyingi sana? Yesu alisema nini? “Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye . . . atawatenganisha watu kama vile mchungaji anavyowatenga kondoo mbali na mbuzi.” (Mathayo 25:31, 32, HNWW; ona pia Ufunuo 14:6.) Malaika wanamsaidia Yesu katika uchungaji, nao wanaelekeza “wafanyi kazi wenzi” wa Mkubwa wawafikie wale wanaomlilia Yeye ili wapate msaada.​—1 Wakorintho 3:6-9, NW; ona Matendo 8:26-39; 16:9, 10.

19. Ni hali gani iliyopo ulimwenguni pote leo, nayo inahitaji sisi tuchukue hatua gani?

19 Leo, hata tuwe tunaishi wapi, kuna maelfu ya watu waliolemewa na kushushwa moyo na matatizo yale yale ambayo wengi wa watu wa Yehova wamekwisha kuyashinda. Huenda wengine wao wakawa wanaishi karibu na nyumbani kwako! Wanahitaji msaada kwa haraka. Kwa kweli, kama vile Yesu alivyosema: “Mavuno ni mengi.” Sisi tunamwomba Mkubwa wa mavuno sasa atume wafanya kazi zaidi ndani ya mavuno yake wakati wa mwaka 1986. Moyo wako na ukusukume uitikie mwito huu: Wanahitajiwa kwa Haraka​—Wafanya Kazi Wengi Zaidi wa Mavuno!

Maulizo ya Kurudia

◻ Mkubwa wa mavuno ni nani?

◻ Ni mavuno gani mawili yamekuwa yakiendelea?

◻ N kazi gani zilizo kubwa zaidi ambazo Yesu alisema wafuasi wake wangefanya?

◻ Kwa sababu gani imani inahitajiwa na wafanya kazi wote wa mavuno?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki