Je, Unaweza Kupanua Utumishi Wako?
1. Kuna uhitaji gani wa haraka kuhusiana na huduma ya shambani, na kwa nini?
1 Alipotambua kwamba watu wengi sana walitaka kusikiliza habari njema za Ufalme, Yesu aliwaagiza wanafunzi wake hivi: “Mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Mt. 9:37, 38) Kwa kuwa tunaishi katika kipindi cha mwisho cha majira ya mavuno, kazi yetu ni ya haraka sasa kuliko wakati mwingine wowote. Kwa hiyo, tunapaswa kufikiria jinsi tunavyoweza kufanya mengi zaidi katika huduma ya shambani, na kusali kuhusu jambo hili.—Yoh. 14:13, 14.
2. Baadhi ya ndugu na dada wameitikiaje mwito wa kuwa na wafanyakazi wengi zaidi shambani?
2 Njia za Kupanua Utumishi: Kwa msaada na mwongozo wa Yehova, wengi wamefanikiwa kuwa mapainia. (Zab. 26:2, 3; Flp. 4:6) Baadhi yao wamejitahidi kuwa mapainia wasaidizi mwezi mmoja au zaidi katika mwaka. Hiyo ni njia nzuri ya kupanua huduma. Wengi kati yao wamefurahia sana utumishi huo hivi kwamba wameamua kuwa mapainia wa kawaida.—Mdo. 20:35.
3. Ikiwa ulikuwa painia hapo awali, unaweza kufikiria kufanya nini?
3 Je, Unaweza Kuwa Painia Tena?: Ikiwa wewe ulikuwa painia hapo awali, bila shaka ulifurahia utumishi huo. Je, umefikiria na kusali kuhusu uwezekano wa kujiunga tena na utumishi wa painia? Hali zilizofanya uache utumishi wa painia huenda hazipo wakati huu. Labda unaweza kufurahia tena pendeleo hili la pekee.—1 Yoh. 5:14, 15.
4. Kila mmoja wetu ana fursa gani ya pekee?
4 Kazi ya mavuno imeendelea kwa muda mrefu na hivi karibuni itakuwa imemalizika. (Yoh. 4:35, 36) Sote na tuchunguze kama tunaweza kupanga shughuli zetu za kila siku ili tupanue utumishi wetu. Hali zisipoturuhusu kupanua utumishi wetu, je, tunaweza kutafuta njia za kutimiza huduma yetu vizuri zaidi? (Marko 12:41-44) Wale ambao hali zao zinawawezesha kushiriki katika utumishi wa painia wana pendeleo kubwa sana!—Zab. 110:3.