Nitasema Nini?
Tunapokutana na watu wanaoitikia vizuri katika huduma, twatamani kurudi tuwatolee ushahidi zaidi. Hata hivyo, huenda tusiwe na uhakika wa jambo la kusema ili kuchochea mazungumzo yatakayofuata. Labda ujaribu mfikio huu: Tokeza swali lenye kupendeza, kisha fungua kitabu Kutoa Sababu uonyeshe jibu la Kimaandiko. Ingesaidia kuwa na orodha ya maswali ambayo katika hayo ungeweza kuchagua moja unalohisi huenda likapata itikio bora zaidi kwenye ziara mahususi. Orodha iliyo chini, ambayo imetungwa kutoka kitabu Kutoa Sababu, yaonyesha nambari ya ukurasa ambapo kila swali lapatikana:
◼ Kwa nini tunazeeka na kufa? (100)
◼ Je! kuna sababu timamu za kuitikadi kwamba kuna Mungu? (218)
◼ Je! Mungu kweli anajali yanayotupata sisi wanadamu? (219)
◼ Je! ni lazima mtu aende mbinguni ili awe na wakati ujao wenye furaha kweli kweli? (190)
◼ Kwa nini ni jambo la maana kujua na kutumia jina la kibinafsi la Mungu? (425)
◼ Ufalme wa Mungu utatimiza nini? (327)
◼ Ni nini lililo kusudi la uhai wa kibinadamu? (341)
◼ Kwa nini kuna dini nyingi sana? (67)
◼ Mtu awezaje kujua ni ipi iliyo dini ya kweli? (73)
◼ Shetani ni mtu mwenye nguvu jinsi gani katika ulimwengu wa leo? (287)
◼ Sababu gani Mungu anaruhusu kuteseka? (132)
◼ Kwa nini kuna uovu mwingi sana? (369)
Ungeweza kuweka orodha hiyo ya maswali katika Biblia yako au kitabu chako cha Kutoa Sababu ili kurejezea haraka. Kuwa na jambo hususa akilini la kusema kwenye ziara za kurudia kutakutia moyo uwe mwaminifu katika kufuatia kupendezwa kote unakopata.