Tumia Kitabu Reasoning Katika Sehemu Zote za Huduma Yako
1 Je! wewe umekuwa ukitumia kitabu Reasoning katika huduma yako? Bila shaka tayari umekwisha kufikiria vishemu mbalimbali vyacho na umekiona kuwa chenye msaada sana. Bila shaka kungekuwa na manufaa kukisoma chote na kuzoeleana na habari yote nzuri iliyomo. Ndugu mmoja painia aripoti kwamba yeye na mke wake wamekuwa wakijifunza kisehemu fulani chacho kila siku.
2 Hata hivyo, si lazima uwe umekisoma kitabu chote kusudi ukitumie katika kazi ya nyumba kwa nyumba au wakati wa kufanya ziara za kurudia na kuongoza mafunzo ya Biblia.
KUSHUGHULIKIA VIPINGAMIZI
3 Yaelekea kuna vipingamizi fulani unavyokabili kwa ukawaida unapoenda nyumba kwa nyumba. Huenda hivyo vikakuzuia katika jitihada zako za kuvutia upendezi wa mwenye nyumba. Huenda wakasema: “Mimi sipendezwi,” “Mimi nina shughuli sana,” au “Mimi nina dini yangu mwenyewe.” Wakati vikomesha mazungumzo hivyo vinapokuwa kizuizi, kwa vyovyote chukua dakika katikati ya milango utie katika akili yako dokezo moja au mawili kwenye kurasa 15-24 za kitabu Reasoning.
4 Maarifa yako kuhusu watu katika eneo yatakuwezesha uchague jibu litakalokusaidia uendeleze mazungumzo yako. Jaribu kutumia mpangilio wa maneno kama ulivyo katika kitabu Reasoning. Umefikiriwa sana na kutumiwa kwa kufaulu na ndugu wenye ujuzi. Muda si muda, utaweza kutoa majibu bora kwa vikomesha mazungumzo mbalimbali.
ZIARA ZA KURUDIA
5 Kwenye ziara yako ya kwanza, huenda ukaweza kuamua kwamba mwenye nyumba apendezwa hasa na habari fulani. Katika kujitayarisha kwa ajili ya ziara ya kurudia, chunguza habari hiyo katika faharisi ya kitabu Reasoning. Ikiwa jambo hilo limefikiriwa, utakuta ama dokezo ambalo laandaa mfikio wa moja kwa moja lakini uliosawazika au habari zaidi ya Kimaandiko itakayomfaidi mtu huyo.
6 Ikiwa swali latokea kwenye funzo la Biblia nawe waamua kwamba ingefaa zaidi kulijibu kabla hujaondoka, chunguza ama faharisi upande wa nyuma wa kitabu Reasoning au orodha ya habari kuu upande wa mbele. Kwa kielelezo, huenda ikawa mtu fulani alimwambia huyo mwenye kupendezwa kwamba Mashahidi wa Yehova ni dhehebu au wanafuata mtu fulani. Habari unayohitaji imetolewa kwenye ukurasa 202. Yapatikana kwa urahisi kwa kutafuta “Jehovah’s Witnesses” chini ya “Principal Subjects.” Habari hususa hupatikana kwa urahisi hata zaidi kwa kutafuta “Cult” au “Sects” katika fahirisi. Jione huru kujibu swali hilo sawa na ilivyo katika kitabu na kuizungumzia zaidi pamoja na mwanafunzi huyo wa Biblia. Usihangaike kwamba mwanafunzi akuona ukitafuta habari ya ziada kwa njia hiyo.
7 Akieleza juu ya shukrani zake kwa ajili ya kitabu Reasoning, dada mmoja aliandika hivi: “Mfikio wenu wenye busara lakini wenye ujasiri wa habari mbalimbali ambazo mara nyingi ni vigumu kuzitaja ni baraka halisi kwetu sisi.” Tunapozoeleana na chombo hiki kizuri na kukitumia shambani, tutafanikiwa zaidi kufikia mioyo ya wale waliomo katika eneo letu.