Pata Manufaa za Kitabu Reasoning
1 Ni kazi kubwa mno jinsi gani ambayo Yehova amewapa utume watu wake waliojitoa wakfu waitimize katika siku hizi za mwisho! (Mt. 24:14; 28:19, 20) Bila msaada wa kimungu kutekeleza kampeni hiyo ya ulimwenguni pote, hiyo ingekuwa kazi ngumu sana. Jinsi tunavyoshukuru kuwa na msaada wa malaika katika kutangaza habari njema za milele!—Ufu. 14:6, 7.
2 Hiyo inahitaji jitihada ya kikweli kwa upande wa waeneza evanjeli ili kufikia mioyo ya watu wa “kila taifa na kabila na ndimi.” Lakini kupitia kwa tengenezo lake la kidunia, Yehova ameandaa msaada unaohitajiwa kwetu sisi ili tufanye hivi. Mojapo ya uandalizi huo ni kitabu Reasoning From the Scriptures, ambacho kina habari nyingi juu ya vichwa 76 ambayo inaweza kutumiwa pamoja na watu wanaotoka katika malezi na namna mbalimbali za maisha.
3 Bila shaka kuzungumzia kitabu hicho katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kunakunufaisha wewe kiroho. Lakini je! wewe unajitahidi kutumia habari hii katika huduma yako? Je! wewe unaweza kuona maendeleo katika uwezo wako wa kutolea watu sababu? Ingawa wewe binafsi huenda ukajibu ndiyo, imeripotiwa kwamba akina ndugu na dada wengi hawatumii kitabu Reasoning, na wengine hawakibebi wanaposhiriki katika huduma. Kwa nini iko hivyo? Labda ni kwa sababu hawajafahamiana na sehemu zenye thamani za kitabu hicho. Wengi ambao wametumia kitabu Reasoning wamepata kwamba wanaweza kukitegemea kwa msaada wakati unaofaa, kikitoa majibu kwa maswali mengi ambayo watu wanauliza.
4 Sehemu moja yacho yenye msaada sana ni fahirisi inayoanza kwenye ukurasa 439. Hakiorodheshi kila pande ya kichwa kikuu, lakini kinaandaa marejezo mengi ambayo utapata kuwa yenye manufaa wakati unaposhughulikia hali fulani.
5 Mathalani, nyakati nyingine tunakutana na watu wanaotilia mashaka utegemeo wa Biblia. Huenda wakajaribu kupuuza Maandiko au itikadi za Mashahidi wa Yehova. Huenda wakauliza swali kama hili, “Kaini alipata wapi mke wake?” Ingawa hutapata jambo hili likiwa limeorodheshwa chini ya “Vichwa Vikuu” upande wa mbele wa kitabu, ukiangalia katika fahirisi chini ya “Kaini,” utapata kwamba jibu la swali hilo linapatikana kwenye kurasa 301-2. Au huenda mtu akasema kwamba upendo wa Mungu unavunjwa kwa uharibifu wa waovu. Ukiangalia chini ya “Upendo” katika fahirisi, unarejezwa kwenye ukurasa 48, ambamo utapata njia ya kusababu na mtu huyo.
6 Sehemu nyingine yenye msaada, inayopatikana kwenye ukurasa 445, ni “Maandiko Ambayo Mara Nyingi Yanatumiwa Vibaya.” Mwenye nyumba anaweza kuzusha swali kuhusu andiko la Biblia au ajaribu kulitumia kuunga mkono itikadi fulani isiyo ya kweli. Huenda yeye akanukuu 1 Wathesalonike 4:13-18 kwa kuunga mkono itikadi yake ya kwamba watu fulani watapaa mbinguni bila kufa hapa duniani. Rejezo linafanywa kwenye ukurasa 312 kwa kuzungumzia mistari hiyo. Ikiwa mtu anabisha kwamba dunia itachomwa na kurejeza kwenye 2 Petro 3:7, habari yenye kueleza wazi inaweza kupatikana kwenye kurasa 113 na 436. Kwa hiyo ikiwa unaulizwa kueleza andiko, uwe na kitabu chako Reasoning mkononi, na uone kama andiko hilo limeorodheshwa katika sehemu hii ya kitabu.
7 Wote vijana na wazee wanaweza kupata manufaa ya kichapo hiki. Kukitumia si jambo gumu, lakini inahitaji jitihada na mazoezi. Fahamiana na matangulizi 41 yanayotolewa kwenye kurasa 9-15. Pia, kuna njia 47 za kufanyia kazi vipinga mazungumzo ambavyo vimeorodheshwa kwenye kurasa 15-24. Je! wewe unajitahidi kutumia nyingine zazo, hasa zile ambazo zingeweza kuwa na matokeo katika kuzungumza pamoja na watu katika eneo lako?
8 Tunafurahishwa sana na pendeleo la kuhubiri katika wakati huu wa mwisho. Hakika Yehova ametupa kile tunachohitaji ili kufanya kazi yetu iwe na matokeo. Na tuendelee kutumia mojapo ya vyombo vyetu vyenye thamani sana, kitabu Reasoning.